October 26, 2017

Applikesheni ya VSOMO yawa suluhisho uchumi wa viwanda

Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kulia) akipata Maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa ufundi umeme Hamadan Omary (kushoto) wakati wa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wanaopata mafunzo ya ufundi stadi kupitia applikesheni ya VSOMO ambayo inaendesha na Airtel kwa kushirikiana na VETA. Katikati ni mkufunzi wa Tehama VETA Kipawa Abdul Mollel.
XXXXXXXXXXX

DAR ES SALAAM

Applikesheni ya VSOMO ambayo inaendeshwa na kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania kwa kushirikiana na VETA imetaja kuwa moja ya soluhisho ya Tanzania kuelekea kuwa nchi ya viwanda.

Hayo yamesemwa na mkufunzi wa Tehama wa chuo cha VETA Kipawa Abdul Mollel wakati wa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi ambao wamekuwa wakipata mafunzo ya ufundi kupitia applikesheni ya VSOMO ambayo inalenga kuwawezesha vijana nchni  kujiendeleza kielimu kupitia application ya VSOMO kwa kupata masomo ya ufundi stadi ya VETA kupitia simu zao za mkononi ili kuongeza ujuzi wao.

‘Tunao wanafunzi wengi hapa Tanzania ambao wangetaka kupata elimu ya VETA. Wengine wako huko vijijini ambao huduma zetu hazipatikani. Lakini hata hivyo inakuwa ni vugumu kwa wao wote pamoja kupata nafasi hapa kwetu. Hata hivyo, kwa kupitia Applikesheni ya VSOMO imekuwa ni rahisi kutimiza azma yao, alisema Mollel.

Ili kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa viwanda, ni muhimu kuwa na wataalam wengi wenye elimu ya ufundi stadi. Huu mradi umekuwa ni muhimu sana kwani hata wale ambao hawana nafasi ya kuhudhuria mafunzo ya darasani wanayo nafasi ya kusoma, aliongeza Mollel.

Wanafunzi wanapata mafunzo kupitia simu zao za mkononi. Baada ya hapo ndio wanakuja hapa kwa ajili ya mafunzo ya vitendo. Wengi hapa leo wanafanya mafunzo ya ufundi umeme, simu na kompyuta. Kitu kikubwa tumeona ya kuwa vijana wanapata mafunzo kwa haraka lakini kikubwa wanakosa kujiamini. Sisi kama waalimu ndio kitu kikubwa kwanza tunakifanya, aliongeza Mollel.

Mafunzo ya vitendo yanachukua takriban masaa 60 baada ya hapo tutawapa mtihani wa mwisho pamoja vyeti. Ni vyema kwa vijana wengine huko mitaani kujiunga na applikesheni hii kwani itawaongezea ujuzi na ufanisi zaidi, aliongeza Mollel.

Akiongea wakati mafunzo hayo ya vitendo yakiendelea, Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema kuwa Airtel imeamua kushirikiana na VETA kutoa mafunzo ya ufundi stadi kupitia applikesheni ya VSOMO baada ya kungundua ya kwamba kuna vijana wengi mtaani ambao wana nia ya kupata mafunzo hayo lakini wanakosa nafasi ya kuhudhuria darasani.

‘Tunatambua kwa Watanzania wengi ambao wana nia ya dhati kabisa kujiunga na VETA lakini wanakosa nafasi ya kuhudhuria darasani. Kupitia VSOMO ni fursa kwao kupata mafunzo kwa njia rahisi na nafuu. Pia tunatambua ya kwamba serikali imedhamiria kufanya Tanzania kuwa uchumi wa viwanda. Kuwa na vijana wengi wenye ujuzi wa fundi stadi ni moja ya njia ya kufanikisha hilo, aliongeza Mmbando.

VSOMO imepata mafanikio makubwa tangu kuanzisha kwake kwani mpaka sasa kuna vijana zaidi ya 30,000 ambao wamepakua applikesheni ya VSOMO kati yao 9,000 wamejiandikisha ili kusoma kwa mtandao. Tunatoa wito kwa watanzania hususani vijana kuchangamkia fursa hii kwa kupakua application ya VSOMO kwenye simu zao na kusoma kozi hizi za ufundi ambazo gharama yake ni 120,000/= hadi kumaliza na kupata cheti, alisema Mmbando.

Kozi zinazopatikana katika application ya VSOMO ni pamoja ni  Huduma ya chakula na mbinu za kuhudumia wateja, Matengenezo ya kompyuta,umeme wa viwandani, ufundi Bomba wa Majumbani, Umeme wa magari. Vilevile Ufundi umeme wa manyumbani, Ufundi pikipiki, Ufundi wa simu za mkononi, Ufundi Alluminium,  Utaalamu wa maswala ya urembo pamoja ma Ufundi wa kuchomea vyuma.


VSOMO proves to be solution for the country’s industrialization drive

The VSOMO application which is a e-learning programme being implemented by Airtel Tanzania in partnership with the Vocational Education and Training Authority (VETA) has proven to be one of the key solutions towards the country’s drive on industrialization.

This has been said by the VETA-Kipawa ICT Instructor Abdul Mollel during the practical sessions for the students who have enrolled and register for courses offered by VETA through the VSOMO application.

VSOMO application allows students to get vocational training through their mobile phones and they only attend classes during practical sessions.

‘We have a lot of students wishing to get vocational training but we cannot accommodate them at once. VSOMO is now our solution to that. The government is currently pushing for industrialization in order to support the country’s economy. Courses offered through VSOMO will expand the reach to studies willing to take vocational training leading them to self-employment. More so, the courses also sharpen and equip them with knowledge on small entrepreneurs. This is the most crucial area as they can lead them towards on small scale industries’ said Mollel.

‘Confidence is the key for success. Most of our students are youth who are dedicated on taking our country on next level. We have been able to make them believe in their skills and as you can see, most of them here have enrolled themselves for the courses in less than six months but now they are able to perform practical’s themselves, added Mollel.

What Airtel Tanzania has done to support this programme clearly indicates the firm’s commitment in supporting government initiative towards industrialization, said Mollel.

The ICT instructor said that after the practical session which last for 60 hours, the students will be awarded with certificates which will enable to get employment or employ themselves.

Speaking at the same event, Airtel Tanzania Public Relations Manager Jackson Mmbando said Airtel decided to partner with VETA in providing vocational training skills to Tanzanians interested in joining VETA through e-learning as they understand that there are many of them out who want to get the skills but don’t have enough time to attend classes.

‘VSOMO application allows students to acquire vocational skills without physically attending to classes. All one needs to register to the programme and pay tuition fee then will be able to start enjoying classes even without internet buddle’s, said Mmbando.
The programme has so far attracted over 30,000 studies that have been able to register and 9,000 out of that number have registered for the studies. Each course is 120,000/- and a student is issued with certificate after completion of the course.


Courses offered through VSOMO are Cake Baking and Decoration, Catering and Food Service Techniques, PC Maintenance, Industrial Electrical Installation, Domestic Plumbing and Auto-electric.

No comments:

Post a Comment