Tangazo

June 30, 2012

TBL Family Day yafana Dar

Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), pamoja na ndugu zao wakishindana katika mchezo wa kuvuta kamba kwenye bonanza la kufurahi pamoja na familia zao, katika ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi Beach,Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Ofisa Mnasihi wa VVU wa AMREF, Peace Kayoza (kushoto), akimchukua kipimo cha  damu Zaina Mohamed, mmoja wa wanafamilia ya TBL katika bonanza hilo.

 Wanafamilia wa TBL wakimuangalia mcheza sarakasi wa kikundi cha Black Texas, wakati akitembea juu ya waya.

 Meneja Uhusiano wa TBL, Editha Mushi akijadiliana jambo na viongozi wenzake wakati wa bonanza hilo.

Meneja Usambazaji na Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Kusini, James Bokela (kulia), akimkabidhi zawadi ya vifaa vya shule, mmoja wa mtoto wa wanafamilia ya TBL baada ya kushinda katika michezo wa mbio kwa watoto wa kiume bonanza la kufurahi pamoja na familia zao, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

                                                      Watoto wa familia ya TBL wakiogelea.

                                    Wafanyakazi wa TBL wakiwa wameshika zawadi za fulana.

Ofisa wa TBL Salvatory Rweimamu (kulia) akimkabidhi zawadi mtoto wa wanafamilia ya TBL aliyeshinda mbio.

 Mtoto wa moja ya familia ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambaye hakufahamika jina lake akitoa shoo ya bure katika bonanza la wafanyakazi hao kufurahi pamoja na familia zao, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

No comments: