Tangazo

September 11, 2012

MAUAJI YA KIKATILI YA DAUDI MWANGOSI: Waandishi wa Habari wafanya maandamano ya Amani jijini Dar

Waandishi wa Habari wakiwa katika maandamano katikati ya Jiji la Dar es Salaam leo wakielekea kwenye viwanja vya Jangwani, ikiwa ni sehemu ya kulaani vikali mauaji ya kikatili ya mwandishi wa habari wa Channel ten mkoani Iringa, marehemu Daudi Mwangosi yaliyofanywa na askari polisi wakati wa vurugu dhidi ya wafuasi wa Chadema huko Nyololo wilaya ya Mufindi hivi karibuni.


Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Nchimbi ambaye aliibuka katika viwanja vya Jangwani alijikuta akilakiwa kwa mabango yenye ujumbe mbalimbali wa kulaani matendo ya polisi, hususani mauaji ya raia wasio na hatia. Hata hivyo waandishi wa habari kwa umoja wao walimtimua waziri huyo na kutamtaka asionekane katika eneo hilo kwani shughuli ilikuwa haimhusu.

Mwandishi wa Habari Mwandamizi na Wakili wa Kujitegemea, Nyaronyo Kicheere akitema cheche.

Manyerere Jackton ni miongoni mwa Wahariri Waandamizi waiotema cheche pale Jangwani.

Umoja ni nguvu na mshikamano.

No comments: