Tangazo

September 12, 2014

WANAWAKE VAENI NGUO SASA, KAMA KUVUA MUMESHAVUA IMETOSHA


MOJA ya sifa ya mwandishi ni kusoma, na katika kusoma huko na kupekua pekua hapa na pale unaweza kujifunza na kupata la kuandika kupitia maandiko ya watu wengine na kutoa elimu kwa umma. Leo nimepita pita katika kurasa za marafiki zangu huko katika uso wa kitabu ‘Facebook nikakutana na nasaha ya ndugu yangu Victory Richard, juu ya kuwasihi wanawake kwamba  sasa wavae nguo.

Ndugu yangu yule amechoshwa na tabia za dada zetu, wake zetu na hata mama zetu wakati mwingine wanavyotembea uchi, ndio! utavaaje nguo fupiii au skintight halafu useme umevaa nguo?. Binafsi naomba radhi kama nitakuwa nimemkwaza mtu hasa hao mama zetu, Ah! Lakini potelea mbali Anko Kidevu sijali kitu si wamejitakia.

Hivi akina mama na dada zetu kweli jamani katika yooote ambayo mnalilia usawa na sisi tunakubali kuwa sawa, hili la kutembea uchi au kuvaa mavazi nusu uchi mbona mnapitiliza?

Ndio mmepitiliza Anko nimebaini kuwa mmetupita maana sisi tukivaa sana ni kaptura au bichkoma na kawosh au singlendi lakini sasa naona mmepita katika sketi na sasa mna vimini na kuacha vifua wazi.

Ni nani awezaye kuona aibu yenu zaidi yangu mimi Anko Kidevu na kaka yenu Victor Richard, tafadhalini tunawasihi, hebu vaeni nguo sasa na jamii itawaheshimu maana hakuna heshima kwa mwanamke hata kidogo. Na kama mnahisi mnaheshimika kwa hilo ni bure kabisa. SOMA ZAIDI FATHER KIDEVU BLOG

No comments: