Tangazo

July 15, 2015

Wateja wa Airtel kujishindia Mamilioni ya Pesa

Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde (kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya ya Airtel ‘Jiongeze na Mshiko’ itakayomwezesha mteja wa mtandao huo kujishindia mamilioni ya pesa kwa njia ya sms. Katikati ni Meneja wa Huduma za Ziada wa Airtel, Prisca Tembo na Afisa Huduma za Ziada, Fabian Felician.


Meneja wa Huduma za Ziada wa Airtel, Prisca Tembo (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya ya Airtel ‘Jiongeze na Mshiko’ itakayomwezesha mteja wa mtandao huo kujishindia mamilioni ya pesa kwa njia ya sms. Kushoto ni na Afisa Huduma za Ziada, Fabian Felician na Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde.
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

*  Yazindua sms promosheni na kuwazawadia wateja wake nchi nzima
*  Promosheni itadumu kwa zaidi ya  siku 120

Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel leo imezindua promosheni kwa wateja wake yenye lengo la kuboresha uhusiano pamoja na kuwazawadia wateja wake nchi nzima  kila wiki  kwa muda wa siku 120.

Promosheni hiyo ijulikananyo kama " Jiongeze na Mshiko" ni ya kipekee kwani inampatia mteja kujiunga na kushiriki bure kwa kujibu maswali na kujishinda shilingi milioni 1 kila wiki na  mwisho wa promosheni kujishindia shilingi milioni 2.

Na ikiwa mteja atapenda kujishindia zawadi kubwa zaidi  ataweza kujiunga na ngazi ya Premium  kwa kuchajiwa  shilingi 300 kwa siku na kupata nafasi ya kujishindia shilingi milion 3 kila wiki na mwisho wa promosheni kujishindia shilingi milioni 50.

Akiongea wakati wa Uzinduzi wa promosheni hiyo, Meneja huduma za ziada wa Airtel, Bi Prisca Tembo, alisema"  promosheni hii inathihirisha lengo letu la kuwawezesha watanzania kufikia ndoto zao na huku tukiendelea kutoa huduma bora  za kibunifu zinazokithi mahitaji yao.

Promosheni ya "Jiongeze na Mshiko" itawawezesha watanzania wengi kujishindia mamilioni ya pesa kila wiki na kuwawezesha kupata fedha kwaajili ya kuendesha shughuli zao za kijamii na kiuchumi pindi watakapoibuka washindi kwa muda wa wote wa mienzi minne.

Mteja atatakiwa kujibu maswali na kujikusanyia pointi zitakazomwongezea nafasi ya ushindi na kuweza kujishindia zawadi ya pesa taslimia kupitia promosheni hii ya " Jiongeze na Mshiko"  natoa wito kwa watanzania kujiunga na kupata nafasi ya kujishidia pesa taslimu kila wiki.

Akiongea jinsi ya kujiunga na kushiriki , Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde  alisema "wateja wataweza kujinga na promosheni hii bure kwa kutuma ujumbe wenye neno "BURE"  kwenda namba 15470, na kasha kuanza kupokea maswali kwenye simu zao na kujibu maswali bure bila gharama yoyote na kujikusanyia pointi.

Mteja atakapomaliza kujibu maswali ya bure atapata ujumbe utakaomuuliza kama angependa kujiunga na ngazi ya premier, ili kuwezeshwa kufunguliwa maswali zaidi na kujikusanyia pointi nyingi kwa zawadi zenye thamani kubwa.

Aliongeza kwa kusema maswali yatakayoulizwa ni ya kawaida hivyo tunategemea wateja wetu watafurahia kuyajibu na kupata nafasi ya kujishindia shilingi milioni 108  ikiwa ni moja ya njia ya kuwazawadia kwa kutumia huduma zetu.

Alitoa wito kwa Tanzania kuwa waangalifu  na kuhakiki taarifa zozote wanazopewa kuhusu Ushindi kwa kupiga 100, namba yetu ya huduma kwa wateja.

No comments: