Tangazo

April 5, 2017

AIRTEL NA MAENDELEO BENKI WAZINDUA HUDUMA ZA MIKOPO KWA VIKOBA KUPITIA SIMU

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Beatrice Singano na Mkurugenzi Mtendaji wa  Maendeleo  Bank  Ibrahim Mwangalaba wakisaini makubalianao ya  uzinduzi wa huduma ya Timiza Vikoba kwa ajili ya kutoka mikopo kwa vikundi vidogo bila dhamana.
xxxxxx
·        -  Airtel Money na Maendeleo Benki kuviwezesha Vikundi vya Vikoba nchini
    Vikundi vya vikoba kupata njia ya kisasa na salama zaidi ya kuendesha shughuli zao za kifedha

Dar es Salaam, Jumanne 4, Aprili 2017, Airtel Tanzania kwa kushirikiana na benkiya Maendeleo leo wamezindua huduma mpya ijulikanayo kamaTimizaVikoba yenye lengo la kuviwezesha vikundi vya vikoba nchini kutumia njia ya kisasa na salama itakayorahisisha ukusanyaji wa michango, kutoa mikopo na marejesho ya mikopo kwa urahisi kabisa.

Huduma hii yaTimiza Vikoba inawawezesha wateja wa Airtel walio katika vikundi vya kuanzia watu 5 hadi 50 kupata huduma za kifedha masaa 24 siku saba za wiki kwa gharama nafuu kwa kupiga  *150*60# na kisha kuingia kwenye menu ya Airtel Money na kusajili kikundi na kufungua akaunti ili kufaidika na huduma ya kutuma michango yao ya kila wiki, kuomba mikopo na kufanya marejesho ya mikopo wakiwa nyumbani au mahali popote pale kwa usalama na urahisi zaidi.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel , Bi Beatrice Singano Mallya alisema” huduma ya Airtel Money imekuwa ikiongoza kwa huduma za kibunifu na kisasa zaidi na leo hii tunazindua ushirikiano wa kipekee na benki ya Maendeleo kupitia huduma ya Airtel Money ili kuwawezesha wafanyabishara katika vikundi vya Vikoba nchi nzima kufanya miamala yao ya kifedha kwa njia salama, uhakika na urahisi zaidi.

Huduma hii italeta uwazi na kuwawezesha vikundi vya vikoba kuhakiki taarifa zao kwa kupata taarifa za miamala mbalimbali kwa wakati kupitia simu zao za mikononi.  Tunaamini huduma hii itachochea wafanyabiashara bila kujali maeneo walioko kujiunga na kutengeneza vikundi vya vikoba ili kunufaikana kukuza biashara zao
Timiza Vikoba ni udhibitisho wa dhamira yetu ya kutoa huduma za kibunifu zinazoendana na mahitaji ya wateja wetu hasa kuleta unafuu na urahisi kupitia huduma yetu ya kifedha aliongeza Bi Singano.

Kwa upande wake , Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank ,Ndugu Ibrahim Mwangalaba alisema “  Maendeleo benki ni benki inayokuwa kwa kasi nchini kwa kutoa huduma mbalimbali zenye gharama nafuu,zenye uraisi wa kutumia ikiwemo ile ya akaunti za kuweka akiba , kutoa mikopo na huduma nyingine nyingi.

Maendeleo benki leo tunajisikia fahari kushirikiana na Airtel katika kuleta huduma yaTimizaVikoba, huduma hii itasaidia wajasiliamali wadogo na wakati kuweza  kuweka akiba zao kupitia simu zao za mkononi. Huduma hii pia  inawawezesha wateja wetu kukopa kupitia simu zao za mkononi ili kufungua fursa mpya katika huduma za kifedha nchini.

Mwangalaba alieleza “kupanuka kwa huduma za kifedha na kuwafikia wale watumiaji  wenye kipato cha chini ndio lengo halisi la Maendeleo benki. Mikakati yetu tuliojiwekea ili kuwafikia wateja kama hao ni kuwapatia huduma nzuri na nafuu zinazoendana na utoaji wa mikopo kwa makundi ili kuwapa uwezo wao wenyewe waweze kudhaminiana kwenye makundi yao. Lengo letu Maendeleo Benki ni kuhakikisha tunaendelea kuleta na kurahisisha zaidi huduma za kifedha kwa kuweka mikakati kama hii itakayoleta tija katika maendeleo ya jamii nchini.


“Dhamira yetu ni kuendeleza tabia ya kujiwekea akiba katika jamii na pia kuwapa wateja uwezo wa kukopa na kupokea mkopo kupitia simu zao za mikoni kwa kuwa tunaamini ni njia bora na rahisi zaidi kuliko ile iliyozoeleka. Mteja ukitumia huduma hii ya mikopo ya Timiza Vikoba unajitengenezea   historia yako ya mkopo kidogo kidogo na baadae kujipatia mkopo mkubwa  kwa masharti rahisi zaidi “. Alimaliza kwa kusema Mwangalaba.

No comments: