Tangazo

August 22, 2017

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu ashiriki Katika Ujenzi wa Taifa wa Skuli ya Msingi Uzi Ngambwa

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akiwa na Wananchi wa jimbo lake katika kisiwa cha uzi ngambwa wakishangilia wakati wa ujenzi wa Taifa wa kujenga madarasa saba ya Skuli ya Msingi  katika Kijiji cha Ngambwa kutowa elimu kwa watoto wa kijiji hicho kupata elimu ya msingi karibu na makaazi yao. Madarasa hayo yanajengwa kwa nguvu za Mwakilishi na Mbunge kwa Wananchi wa Jimbo lao.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akizungumza na wananchi wa Kisiwa cha Uzi Ngambwa wakati wa ujenzi wa madarasa ya Skuli ya Msingi Ngambwa Uzi inayojengwa na Mbunge na Mwakilishi na nguvu Wananchi wa kijiji hicho. 
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akiwahutubia wananchi wa kisiwa cha Uzi Ngambwa jimbo lake wakati wa ujenzi wa Taifa wa madarasa ya Skuli ya Msingi Ngambwa. 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Ramadhani Abdallah akizungumza na wananchi wa kisiwa cha Uzi Ngambw wakati wa ujenzi wa Skuli ya Msingi ya Ngambwa. inayojengwa na Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo la Tunguu na Nguvu za Wananchi wa Kijiji hicho.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akishiriki katika ujenzi wa skuli ya msingi uzi ngambwa. 
Wananchi wa Ngambwa wakiwa katika ujenzi wa Skuli yao ya Msingi.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar akishiriki katika ujenzi huo wa Skuli ya Msingi Ngambwa Uzi.
Mwananchi wakishiriki katika ujenzi huo wa skuli ya msingi katika kisiwa cha Uzi kijiji cha Ngambwa.
Wananchi wa kijiji cha Ngambwa wakifuatilia hafla hiyo ya ujenzi wa Skuli yao mpya ya msinga katika kijiji chao. 
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohamed Said akiwa na bero likiwa na mchanga akishiriki katika ujenzi wa Skuli ya Msingi Ngambwa katika kisiwa cha Uzi Wilaya ya Kati Unguja.
Jengo la madarasa ya Skuli ya Msingi Ngambwa likiendelea na ujenzi wake.
Wananchi wa kijiji cha Ngambwa Uzi wakishiriki katika ujenzi wa madarasa katika kijiji hicho.
Wananchi wa kijiji cha Ngambwa kisiwa cha Uzi wakiwa katika ujenzi wa madarasa ya Skuli ya Msingi Ngambwa inayojengwa kwa nguvu na Mbunge na Mwakilishi kwa kushirikiana na Wananchi wa Kijiji hicho.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu ZanzibarMhe. Simai Mohamed Said akizungumza na Mwananchi wa jimbo lake mkaazi wa Ngabwa Uzi Bi. Mwanaacha Khatib mkulima wa mwani wakati wa hafla ya ujenzi taifa wa skuli ya msingi ngambwa kisiwani humo.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com
Zanzines.com.
othmanmaulid@gmail.com.

No comments: