Tangazo

September 21, 2017

Ecobank yazindua njia salama ya malipo kwa mtandao

Mkurugenzi  Mtendaji wa Benki ,Ecobank Tanzania, Mwanaiba Mzee, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa Uzinduzi  huduma ya Malipo kwa njia ya Mtandao, inayayojulikana kama MasterPass na MVISA .Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki  hiyo, Respige  Kimati  na Mkuu wa Kitengo cha wateja wa Reja reja, Ndabu Sware (kushoto).
XXXXXXXXXXXXX

DAR ES SALAAM
Ecobank yaja na suluhisho la kufanya malipo salama kwa njia mtandao kupitia MASTERPASS na MVISA .
Ecobank katika kuendeleza dhamira yake ya kutoa huduma bora na kuwa suluhisho kwenye sekta ya biashara ya huduma za kibenki hapa nchini leo imezindua applikesheni ya simu za mkononi itakayojulikana kama Ecobank Mobile App – MASTERPASS NA MVISA ili kusaidia wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali kufanya Malipo kwa njia rahisi na kwa usalama zaidi mahali popote.
 
Mtanzania yeyote ataweza kutumia teknolojia hii ya mpya ya MASTERPASS QR na MVISA kulipia gharama mbali mbali kwa kutumia simu zao za mkononi kwa kupitisha Quick Response (QR) kwa wauzaji mbalimbali wa bidhaa au watoa huduma ndani na nje ya nchi.
 
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania Bi, Mwanahiba Mzee alisema “applikesheni ya Ecobank Mobile App ilizinduliwa Februari mwaka huu lakini kwa sasa imeboreshwa zaidi ili wateja wa Ecobank na wale wasio wateja wa bank hii waweze kutumia applikesheni hii duniani kote”.
 
‘Applikesheni ya Ecobank Mobile App ni njia rahisi ya kujipatia huduma za kibenki ndani ya nchi 33 ambazo Benki yetu inafanya biashara lakini pia unaweza kuitumia ukiwa kokote duniani. Wateja wanaweza kupakua applikesheni Ecobank Mobile App na papo hapo kujifungulia akaunti ya Ecobank kwa njia ya mtandao na kuanza kupata huduma za kibenki kama vile kufanya malipo au kuhamisha fedha bila kutembelea tawi lolote la Benki”, alisema Bi Mzee.
 
“Tunayo furaha kwamba applikesheni yetu ni sulushisho la huduma za haraka za kibenki kupitia mtandao wa simu za mkononi na bado inaendea kuboreshwa  zaidi na zaidi na sasa tunatumia teknolojia ya Masterpass QR na Mvisa kwa kufanya malipo mbali mbali, aliongeza.
 
Bi Mzee aliongeza kuwa Masterpass QR na Mvisa ni njia za mtandao (kidigitali) ambazo humfanya mteja kulipa kwa kadi ya Benki au akaunti zake za benki ambazo pia zimeunganishwa katika mtandao huu kwa kugusisha na kufanya malipo. ‘Hii ni njia ya kutumia simu za mkononi ambapo mnunuzi ataweza kumlipa muuzaji au mtoa huduma yeyote na hivyo  inakuwa ni suluhisho kwa wajasiriamli wadogo, wa kati na wakubwa’, aliongeza Bi Mzee.
 
Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi Swere Ndabu alisema “Ili kutumia huduma hii wateja wa Ecobank na wasio wateja wa Ecobank wanatakiwa kupakua Applikesheni ya Ecobank Mobile App kwenye smartphone zao kisha wanajisajili kwa kutumia kadi ya Visa au Master , au kufungua akaunti ya Ecobank Xpress papo hapo na kuanza kufanya miamala ya malipo. Kwa wale ambao ni wateja wanatakiwa kupakua na kuanza kutumia applikesheni kwa kutumia debit card au Ecobank Retail internet banking.”
 
“Kwa kutumia applikesheni hii wakati wa kufanya Malipo, mteja atanufaika kwa kuokoa muda wake na  kupunguza gharama za kutembelea tawi la Benki, ataweza pia kufanya Malipo kwa haraka na kwa usalama zaidi pamoja na kuongeza mauzo kwa vile njia hii itachochea matumizi au manunuzi salama. Vilevile itamsaidia muuzaji sana kwani ni njia rahisi ya kutunza kumbu kumbu za mauzo.” alisema Swere.
 
Swere aliongeza kuwa kwa kutumia applikesheni ya Ecobank Mobile App mteja anaweza akahamisha fedha kwenye akaunti yake ya Ecobank akiwa hapa nchini au nje ya Tanzania, pia ataweza kuhamisha fedha kwenda Benki nyingine hapa nchini au kwenda kwenye kadi za Visa duniani kote na pia kwenye mitandao ya simu za mkononi ya M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
XXXXXXXXXX

Ecobank unveil mobile payment solution – MASTERPASS and MVISA for easier retail payment.
 
In its drive to promote financial inclusion among Tanzanians, Ecobank Tanzania has unveiled payment solutions – MASTERPASS and MVISA for easier retail payment using the Ecobank Mobile APP.
 
MASTERPASS QR and MVISA are digital payment solutions that offer customers the convenience of doing digital payments at retail outlets much cheaper, more securely and conveniently. Customers pay through their smart phones by scanning the unique Quick Response (QR) code at the retail outlet.
 
Speaking today in Dar es Salaam, Ecobank Tanzania Managing Director,  Ms. Mwanahiba Mzee said that the Ecobank Mobile App that was launched in February this year has  now been modified to include more features which will be beneficial not only to Ecobank customers but also to non-customers across the world.
 
‘Ecobank Mobile App is a one of a kind banking application that is activated in all 33 countries where Ecobank is present and is accessible worldwide. Customers can just download the app and open an Ecobank digital account, make payments and transfer funds without physically visiting the branch,’ said  Ms Mwanahiba Mzee. 
We are now back with enhanced unique features of the mobile app and we are pleased to bring to you Masterpass QR and Mvisa payment solutions, she added.
 
The Ecobank MD, Mwanahiba Mzee said that MASTERPASS QR and MVISA are digital payment services that allow consumers to pay with their cards or accounts anywhere, on any connected device through a simple click, tap, or touch.  To add on that Ms. Mzee said, this is a mobile driven, person to merchant payment solution designed to address payment challenges within the Micro, Small and Medium Scale Enterprise segment. 
 
‘Both Ecobank and Non-Ecobank customers simply need to download the App on their smartphone then register using a debit Visa/Master card, or Open Ecobank Xpress account and transact.  Existing customers need only to download and activate the app using either their debit card or Ecobank Retail internet banking credentials’, the bank’s the Head of Personal Banking, SWERE Ndabu said.
 
The Head of Personal Banking said that Merchants  enrolling on these payment solutions will benefit by lower infrastructure costs, fast cash-like settlement, Lower risk  and boosts sales growth as it encourages spending. They also assist merchants to easily keep record and reconciliation for sales and stock.
 
Ms. Swere added that by using Ecobank mobile app customers can transfer funds within Ecobank locally and internationally, other banks in Tanzania, to any Visa Card worldwide and to mobile wallets (M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money).
 
This is a unique digital product that regards Ecobank as most digitalized bank in Tanzania  and Africa at large and therefore I call upon Tanzanians to come and make use of it and  xperience the difference, said Ecobank MD, Mwanahiba Mzee.

No comments: