Tangazo

September 11, 2017

KAIRUKI HOSPITALI YAZINDUA KITENDO CHA KUCHUJA DAMU KWA WAGONJWA WENYE MATATIZO YA FIGO

SPIKA Mstaafu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda, amewataka watanzania kutumia Mfuko wa Taifa wa Bima hiyo ili kupata unafuu wa matibabu pindi wanapougua.

Wito huo alitoa jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti huyo wakati alipozindua kitengo cha kusafisha damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo katika Hospitali ya Kairuki.

Alisema, kutokana na gharama ya matibabu kupanda kila siku,kadi za  bima ya afya zitasaidia kwa kiasi kikubwa kupata unafuu wa matibabu kipindi mgonjwa anapokuwa hana fedha.

Makinda, alisema bima hiyo inatoa fursa kwa wanachama kupata huduma za matibabu katika hospitali wanazoona zinatoa huduma nzuri na kumjali mgonjwa.

“Vituo vyenye huduma ya NHIF vinapaswa kutibia wagonjwa kwa kuwajali , kuwapenda pamoja na kuwa wakarimu kwa wagonjwa kwani huduma hii inasaidia sana watu hasa wale wanaougua magonjwa yenye kulipia  gharama kubwa,”alisema Makinda.

 Aidha alisema ni watu wachache ambao wanauwezo wa kujitibu bila bima ya afya lakini watu wengi wanategemea huduma hiyo kulingana na gharama kubwa za matibabu katika baadhi ya magonjwa.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kairuki Dk. Asser Mchomvu, alisema nchini Tanzania watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa  na magonjwa yanayosababishwa na matatizo ya figo.

“Kwa hivi sasa ugonjwa huo umeonekana kuathiri  kati ya asilimia 7 hadi 13 ya watanzania, wengi wao wakiwa wagonjwa wa  kisukari (Diabetes Mellitus)na shinikizo la damu(Acute Kidney  injury) ,”alisema.

Alisema kwa muda mrefu hospitali yao  imekuwa ikipokea wagonjwa wenye matatizo ya figo na kulazimika kuwapa rufaa kwenda nje ya hospitali hivyo kupitia kitengo hicho kitaweza kutibu wagonjwa 40 kwa siku.

Alisema kuwa kutakuwa na mashine  10 zenye uwezo wa kuwahudumia wagonjwa na hadi kufikia sasa wamepata kibali cha wizara husika ambapo miongoni mwa mashine hizo ipo ya  kuchuja damu itakayosaidia kuzuia uharibifu wa figo wa kudumu na wa muda hivyo kuokoa gharama.

Dk. Mchomvu, alisema hospitali hiyo inatarajia  kuongeza idadi ya mashine ili kuweza kuwahudumia wagonjwa wengi  pamoja na kutoa huduma ya kupandikiza figo na kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHJF), Anne Makinda (katikati), akiongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kairuki Hospitali, Kokushubila Kairuki (kushoto), wakati wa uzinduzi wa Kitengo cha kuchuja Damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo cha Kairuki Hospitali. 
Mkurugenzi Mkuu wa Kairuki Hospitali Dk. Asser Mchomvu, akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Kitengo cha kuchuja Damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo cha Kairuki Hospitali.
Baadhi ya madaktari waliohudhuria hafla hiyo wakisikiliza hotuba za viongozi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Kairuki Hospitali, Kokushubila Kairuki akitoa hotuba yake.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda (kushoto), akikata utepe wakati wa uzinduzi wa Kitengo cha Kuchuja Damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo cha Hospitali ya Kairuki Mikocheni jijjini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kairuki, Kokushubila Kairuki.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda (kushoto), akipata maelezo alipotembelea kitengo cha kuchuja damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo.
 Dk. Muga akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda.
Dk. Muga akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda (katikati), akipata maelezo kutoka kwa Muuguzi wa Kitengo cha Kuchuja Damu, Eva Beatus.
 Jengo la Kitengo hicho.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne Makinda, akitoa hotuba yake.

No comments: