Tangazo

February 14, 2018

Airtel yagawa Simu za Smatiphone kwa washindi SHINDA NA SMATIKA Intaneti

Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiongea na washindi wa SHINDA NA SMATIKA Intaneti wakati wakuchezesha droo leo jijini Dar es Salaam ambapo washindi 3000 walijishindia 1GB bure, watano simu tano za smartphone na tano modem.
xxxxxxxxxxxxxx
  • Washindi wengine 3,000 wajishindia kifurushi cha intaneti 1GB kila mmoja

Kampuni inayoongoza kwa kutoa huduma bora za smartphone Airtel Tanzania imewazadia washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya SHINDA NA SMATIKAIntaneti katika droo iliyochezwa leo jijini Dar es Salaam.

Katika droo hiyo ya leo, washindi 10 wameweza kujishindia simu za kisasa  za smartphone pamoja na modem huku wengine 3,000 wakijishindia kifurushi cha intaneti cha 1GB BURE. Hii ni droo ya tatu tangu kuzinduliwa kwa promosheni hiyo ambapo mpaka leo jumla ya washindi 8,000 tayari wamezawasiwa  zawadi ya kifurushi cha intaneti cha 1GB BURE.

Akizungumza baada ya droo ya leo, Meneja Uhusiano Airtel Jackson Mmbando alisema kuwa promosheni ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti ni maalum kwa  wateja wote wa Airtel wanaotumia huduma ya Yatosha Intaneti nchi nzima.

‘Promosheni yetu ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti bado inaendelea, ni muhimu kufahamu kuwa mteja haitaji kujisajili kwa ajili ya promosheni ya SHINDA NA SMATIKA Intaneti. Kile anachotakiwa kufanya ni kupiga *149*99# halafu changua namba 5 Yatosha SMATIKA Intaneti, hapo atanunua bando aidha ya siku, wiki au mwezi na kuwa mmoja wa washindi wa zawadi zetu kambambe’, alisema Mmbando.

No comments: