Tangazo

April 30, 2018

DK. KIGWANGALLA ATOA OFA YA MAPUMZIKO YA FUNGATE YA ALI KIBA KATIKA HIFADHI ZA WANYAMAPORI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa ofa maalum kwa Mwanamuziki, Ally Kiba, mke wake na wasaidizi wake ambao ni mdogo wake Abdu Kiba na mkewe kupumzika katika Hifadhi ya Taifa atakayoichagua wakati wa fungate yake ili aweze kufurahi vivutio vya utalii vilivyopo na hivyo kuhamasisha utalii wa ndani. Ametoa ofa hiyo jana wakati wa harusi ya msanii huyo iliyofanyika katika ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa sherehe hiyo na Waziri wa Afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mbunge wa Viti Maalum, Neema Mgaya.
 Picha ya pamoja katika sherehe hiyo iliyojumuisha Bwana Harusi, Ali Kiba, mke wake na wapambe wake na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali akiwemo Mbunge wa Viti Maalum, Mama Salma Kikwete, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimum, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na Mwenyekiti wa UVCCM Kheri James.
Picha ya pamoja ya maharusi na viongozi wa chama na Serikali pamoja na Gvana wa Jiji la Mombasa, Rashid Bedzima (wa pili kulia).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiteta jambo na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde na  Wanamuziki, Ommy Dimpoz na Hamisi Mwanjuma MwanaFA.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifurahia jambo na Msemaji wa Klabu ya Simba, Haji Manara na Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa sherehe hiyo.

Usalama Mahala pa Kazi, TANESCO yaibuka Kidedea yakabidhiwa Ngao, IRINGA

 
Shirika la Umeme TANESCO, limeibuka Kidedea Kwa Kupata Ushindi Kwenye Shindano la Usalama Mahali pa Kazi lililoendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya IRINGA.

TANESCO imepata Ushindi huo Kupitia Sekta ya Huduma, ambapo imekabidhiwa Ngao na Cheti ikiwa ni Heshima ya Kutambuliwa Kama Taasisi ambayo imefanya Vizuri Kwa Kuzingatia Usalama Mahala pa Kazi.

Baada ya Shirika hilo la Umeme Kutangazwa Mshindi na Kukabidhiwa Ngao, Afisa Afya na Usalama Makao makuu NELSON MNYANYI amesema Elimu ya Afya na Usalama imekuwa Kichocheo Kikubwa katika Kupunguza Ajali kwa Wafanyakazi wa TANESCO pamoja na Wananchi kwa Ujumla.

Kwa Upande wake Afisa Afya na Usalama FRED KAYEGA akielezea Ushindi huo amesema licha ya Kupokelewa kwa Faraja, ni Motisha kwa TANESCO kuendelea Kufanya Vizuri zaidi Kwenye Sekta ya huduma Kwa Kuzingatia Usalama Mahala pa Kazi.

Katika Banda la TANESCO elimu mbalimbali kuhusu Afya na Usalama na Elimu Kuhusu Matumizi Bora na Sahihi ya Umeme iliweza Kutolewa kwenye Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.
Waziri wa Viwanda, Biashara ya Uwekezaji CHARLES MWIJAGE akiangalia Baada la TANESCO mara Baada ya Kulitembelea Katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa, ambapo Shirika hilo limeibuka Mshindi Kwenye Sekta ya Huduma Kupitia Mashindano ya Usalama Mahala pa Kazi yaliyoendeshwa na Taasisi ya OSHA.
Maaofisa wa Shirika la Umeme TANESCO, Kutoka Kushoto Sylvester Matiki ( Afisa Masoko ), Nelson Mnyanyi ( Afisa Usalama ), Fred Kayenga ( Afisa Muandamizi Usalama na Afya Mahali pa kazi ) pamoja na Hassan Athumani (Mwenyekiti wa majadiliano TUICO TANESCO) wakifurahia Ushindi wa Ngao na Cheti Baada ya Kukabidhiwa Kama Washindi Kwenye Sekta ya Huduma Kupitia Mashindano yaliyoendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.
Wananchi Mbalimbali Katika Manispaa ya Iringa Waliofika Katika Banda la TANESCO katika Viwanja vya Kichangani Wakipewa Elimu Kuhusu Afya na Usalama pamoja na Matumizi Bora na Sahihi ya Umeme.
Afisa wa TANESCO, Kitengo cha Huduma kwa Wateja ENIDY ELSON akitoa Elimu ya matumizi Bora ya Umeme kwa Wanafunzi na Wananchi Waliofika Kwenye Banda la Shirika hilo Wakati wa Shindao la Usalama Mahala pa Kazi lilioendeshwa na Taasisi ya OSHA katika Viwanja vya Kichangani Manispaa ya Iringa.

April 27, 2018

COCA-COLA NYANZA BOTTLERS YAMWAGA ZAWADI ZA PROMOSHENI YA 'MZUKA WA SOKA'

Kampuni ya Coca-Cola Nyanza Bottlers ya Mwanza imemwaga zawadi kwa washindi wa promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka inayoendelea.Wakazi 16 wa kanda ya ziwa wiki hii wameweza kukabidhiwa zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki 7,luninga bapa 7,na 2 fedha taslimu.

Zawadi hizo zimekabidhiwa na Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni hiyo,Samwel Makenge,ambaye alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia vinywaji vinavyotengenezwa na kampuni ya Coca-Cola iliwaweze kujishindia zawadi kwa kuwa bado ziko nyingi.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Baadhi ya washindi katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa zawadi zao.

WAZIRI KIGWANGALLA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA SAUDI ARABIA, KUWAIT NA MSIMAMIZI WA JUMUIYA YA MAKAMPUNI YA ALBAWARDI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Msimamizi wa Makampuni ya Albawardi, Fouad Mustafa ya Umoja wa Falme za Kirabu ofisini kwake Jijini Dodoma jana ambapo walijadili uwekezaji wa kuimarisha sekta ya utalii na uhifadhi nchini. Umoja huo umeahidi kutoa ushirikiano wa ujenzi wa barabara inayounganisha Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
.........................................................................
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ameonana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Saudi Arabia na Kuwait pamoja na Msimamizi wa Jumuiya ya Makampuni ya Albawardi inayoendesha hoteli mbalimbali za kitalii nchini ikiwemo Hyatt Regency  na Four Season Serengeti ofisini kwake Jijini Dodoma jana.
Mazungumzo hayo yaliyolenga kujadili mambo mbalimbali ya kuimarisha sekta ya uhifadhi na utalii kwa maslahi ya nchi hizo tatu. Mabalozi hao ni Bandar Abdulla wa Saudi Arabia, Mohammad Rashed Alamiri wa Kuwait na Fouad Mustafa Msimamizi wa Makampuni ya Albawardi ya Umoja wa Falme za Kirabu kwa upande wa Tanzania na Afrika ya Mashariki.
Dk. Kigwangalla aliwaomba mabalozi hao kupitia jumuiya zao za uwekezaji kuwekeza katika miundombinu ya hoteli za kitalii Jijini Dodoma na kwenye Mapori ya Akiba katika Sakiti ya Kaskazini, Kusini na Magharibi hususan Pori la Akiba la Burigi.
Naye Msimamizi wa Jumuiya ya Makampuni ya Albawardi, kwa upande wa Tanzania na Afrika ya Mashariki, Fouad Mustafa alisema jumuiya hiyo ipo tayari kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika ujenzi wa miundombinu ya barabara inayounganisha Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Alisema mbali na uwekezaji uliopo hivi sasa jumuiya hiyo inajenga hoteli nyingine za kitalii tatu katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Hifadhi ya Ngorongoro na katikati ya Jijini la Arusha ambapo ameiomba Serikali kuzifungua kupitia viongozi wake wa juu pale ujenzi wake utakapokamilika hususan Mhe. Rais.Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Msimamizi wa Makampuni ya Albawardi, Fouad Mustafa ya Umoja wa Falme za Kirabu ofisini kwake Jijini Dodoma jana ambapo walijadili uwekezaji wa kuimarisha sekta ya utalii na uhifadhi nchini. Umoja huo umeahidi kutoa ushirikiano wa ujenzi wa barabara inayounganisha Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Balozi wa Kuwait hapa nchini, Mohammad Rashed Alamiri (kushoto) ofisini kwake Jijini Dodoma jana ambapo walijadili namna ya kuimarisha sekta ya utalii na uhifadhi nchini. Wa pili kulia ni Msimamizi wa Makampuni ya Albawardi, Fouad Mustafa ya Umoja wa Falme za Kirabu ambao wameahidi kutoa ushirikiano wa ujenzi wa barabara inayounganisha Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.Mazungumzo yakiwa yanaendelea.Waziri Kigwangalla akizungumza katika kikao hicho.Waziri Kigwangalla akiagana na msafara huo.

April 26, 2018

STEVE NYERERE AMTANGAZIA NEEMA MZEE MAJUTO KWA MATIBABU NCHINI INDIA

Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza Steve Mengele 'Steve Nyerere' akimsalimia Mzee Majuto ambaye amelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza Steve Mengele 'Steve Nyerere' akiongea machache mara baada ya kumtembelea Mzee Majuto ambaye amelazwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam. Mzee Majuto akitoa shukrani zake mara baada ya kutembelewa na kuonyeshwa mwanga wa matibabu zaidi nchini India.
Msanii Aunty Ezekiel akimsalimia Mzee Majuto.
Kicheko kidogo...
Mtoto wa Mzee Majuto, Hamza akitoa shukrani kwa wasanii waliofika kumsalimia baba yake.
Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza Steve Mengele 'Steve Nyerere' akiteta jambo na Mzee Majuto.

MSANII DIAMOND KUTUMBUIZA KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI

 Msanii Diamond akiongea katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es alaam (katikati) ni Sealouise Shayo, Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini (kulia) ni Meneja wake Sallam SK.
 Msanii Diamond na Nahreel katika mkutano wa waandishi wa habari, wengine ni maofisa wa Coca-Cola na mameneja wa msanii Diamond.
Maofisa wa Coca-Cola wakiwa katika picha ya pamoja na Diamond na Nahreel baada ya mkutano na waandishi wa habari. Msanii nguli wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz, kwa kushirikiana na kampuni ya Coca-Cola ametangaza kuwa ameshiriki kuimba wimbo utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 uitwao Colours. 

Wimbo huo uliotungwa na mwanamuziki Jason Derulo wa Florida, Marekani, Diamond ameshiriki kuweka maudhui ya lugha ya Kiswahili na umetayarishwa na prodyuza Nahreel kwa kushirikiana na maprodyuza kutoka nchi nyingine chini ya udhamini wa kampuni ya Coca-Cola. 

 Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, amesema anayo furaha kupata fursa ya kushiriki kuimba kuimba wimbo wa mashindano haya makubwa ya kidunia na kuitangaza Tanzania na lugha ya Afrika bila kusahau tasnia ya muziki kwa ujumla. 

 “Kwangu hii ni nafasi nyingine ambayo najivunia kuipata ya kutangaza muziki wa kitanzania sambamba na lugha ya Kiswahili kwa kuwa sehemu niliyoshiriki kuimba nimetumia lugha ya taifa la Tanzania ambayo inazidi kupata umaarufu mkubwa duniani”alisema Diamond. 

 Kwa upande wake Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola ambayo ni moja ya mdhamini wa mashindano haya makubwa ya soka duniani inayo furaha kwa msanii kutoka nchini Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano haya. 

“Tuna imani watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano haya”alisisitiza. Prodyuza nguli wa muziki nchini na kanda ya Afrika Mashariki, Nahreel, ambaye ameshiriki kutengeneza wimbo huu aliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa jitihada mbalimali ambazo imekuwa ikifanya kuwanyanyua wasanii wa hapa nchini ambapo mbali na Diamond naye ameshiriki kwenye tukio hili kubwa. 

“Ninayo furaha ya kufanya kazi na Diamond kwa mara nyingine katika tukio hili kubwa la mashindano ya Kombe la Dunia na najivunia heshima kubwa tuliyopewa”

TANGA: INAVYOKUA KIVUTIO CHA UTALII NCHINI TANZANIA

Na Jumia Travel Tanzania

Miongoni mwa mikoa maarufu nchini Tanzania ni pamoja na Tanga. Ukiachana na ukaribu wake na jiji la Dar es Salaam, mkoa wa Tanga una utajiri wa utamaduni wa Waswahili wanaopatikana katika pwani ya bahari ya Hindi, makumbusho ya kihistoria, shughuli za uchumi na kibiashara, pamoja na wanasiasa na wanasanaa mbalimbali mashuhuri wanaolipeperusha vema jina la mkoa huu.   
Hivi karibuni mkoa wa Tanga umekuwa ni eneo mojawapo la kitalii linalokua kwa kasi na kuwavutia watalii wengi ndani na nje ya Tanzania. Watalii wengi kupendelea kwenda Tanga kunaweza kusababishwa na sababu kadhaa zikiwemo miongoni mwao tayari wamekwishatembelea sehemu zingine, kupata simulizi kutoka kwa watu wao wa karibu pamoja na vivutio vingine ambavyo havipatikani sehemu zingine isipokuwa Tanga.
Jumia Travel imekukusanyia baadhi ya sababu ambazo zimepelekea watu wengi kupendelea kwenda kutalii mkoa wa Tanga:  

Jiografia. Asilimia kubwa ya watalii hupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere uliopo katika jiji la Dar es Salaam. Umbali uliopo kati ya jiji hili na mkoa wa Tanga sio mkubwa, huchukua muda wa takribani masaa 6 kitu ambacho watalii wengi huweza kumudu. Hii imerahisisha shughuli za kitalii kwa urahisi kwa sababu watalii wanaweza kwenda na kurudi kwa urahisi. 

Vivutio vya kitalii. Mkoa wa Tanga umebarikiwa kuwa na vivutio mbalimbali ambavyo haviwezi kupatikana sehemu nyingine. Tanga inazo mbuga kama vile Saadani, Mkomazi, na Jozani ambazo unaweza kujionea wanyama, ndege na mimea ya aina mbalimbali lakini pia ina maeneo kama vile mapango ya Amboni na makumbusho ya kale ambayo yamebeba historia na urithi wa mkoa huo tangu enzi za wakoloni.   

Hali ya hewa. Miongoni mwa mji mashuhuri kwa shughuli za kitalii hivi sasa mkoani Tanga na Tanzania kwa ujumla ni Lushoto. Hali ya hewa nzuri, mandhari ya kuvutia na hoteli za kitalii katika eneo hili zimekuwa ni hamasa kubwa kwa wasafiri wengi. Eneo la Lushoto ambalo linapatikana kwenye safu ya milima ya Usambara limejizolea umaarufu kutokana na shughuli tofauti za kitalii kama vile matembezi na kupanda milima, shughuli za uvuvi, kuendesha baiskeli, kutembelea makumbusho ya kale, nakadhalika. Na kwa kuongezea eneo hili limewekezwa kwa hoteli za kisasa za kitalii.   

Hoteli za kitalii. Kutokana na kuwepo kwa shughuli nyingi za kitalii, kumekuwa na uwekezaji mkubwa katika huduma ya malazi. Miongoni mwa changamoto kubwa inayoikumba sekta ya utalii nchini na duniani kote ni huduma ya malazi. Malazi ni huduma ambayo huwa ghali ukilinganisha na huduma nyingine kama vile usafiri wa kwenda na kurudi, viingilio na makato mengineyo. 

Mkoa wa Tanga umejitahidi kwa hilo, wafanyabiashara wengi wamejenga hoteli ili kuweza kukidhi haja ya kila aina ya mtalii. Si jambo la kushangaza kukuta hoteli za kitalii karibu na vivutio vya kitalii.        
Gharama nafuu. Miundombinu kama vile barabara imewavutia watu wengi kwenda kwa urahisi kutalii vivutio vya mkoa wa Tanga kwani imerahisisha gharama za usafiri. Ukiachana na usafiri wa mabasi yanayokwenda na kurudi kila siku, watu wengi siku za hivi karibuni wamekuwa wakitumia usafiri wao binafsi. Unafuu pia upo kwenye huduma ya malazi ambayo kila mtu anaweza kumudu pamoja na gharama za kuishi kwenye jiji hilo kwa ujumla.  

Ukarimu wa watu wake. Watu wa Tanga wanasifika kuwa na haiba ya ukarimu kama walivyo watanzania wengi nchini. Hiki nacho kimekuwa ni kivutio kingine kwa watalii wengi kutembelea eneo hilo. Ukarimu huwavuta watalii wengi, kuwajengea hali ya usalama na kujifunza mengi kutoka kwa wenyeji wao. Wakazi wa Tanga wanatoa mchango mkubwa katika kulitangaza jiji lao kitalii kwa kuwapokea wageni na kuwafunza mambo yanayopatikana mkoani mwao.  
Kama ulikuwa unafikiria sehemu ya kwenda kutalii tofauti na sehemu ulizozizoea, Tanga itakuwa ni chaguo sahihi kwa hivi sasa. Ni miongoni mwa sehemu zinazofikika kwa urahisi na unaweza kufanya shughuli nyingi ndani ya muda mfupi na kurejea kwenye majukumu yako ya kawaida.

KONCEPT yawajengea uwezo wa kujitambua wanafunzi wa kidato cha sita

Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele akitoa nasaha kwa wanafunzi wa shule ya wavulana Kibiti Boys .Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.
Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele akitoa nasaha kwa wanafunzi wa shule ya wavulana Kibiti Boys .Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.

Wanafunzi wa kidato cha sita wapatao 451 wa  shule ya wavulana Kibiti Boys  iliyopo wilaya  ya kibiti  Mkoani  wakisikiliza kwa makini nasaha zilizokuwa zikitolewa na Mkurungezi wa KONCEPT Krantz Mwantepele alipotembelea shule hii mapema wiki katika kuwajengea uwezo katika maandalizi yao ya mitihani ya mwisho na pia kuwapa dondoo za mafanikio katika maisha kwa ujumla.

Mmoja wa wanafunzi akiuliza swali kwa Mkurungezi wa KONCEPT  Krantz  Mwantepele  Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.

Wanafunzi wa kidato cha sita wa shule ya wavulana Kibiti wakionesha kuwa wamehamasika na nasaha zilizotolewa na Mkurungezi mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele .Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.
Mkuu wa shule ya wavulana ya Kibiti Boys Dismas Njawa akifafanua jambo kabla ya kufunga kongamano hilo lililoendeshwa na Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele . Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.

Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT akifurahi jambo na Mkuu wa shule ya wavulana Kibiti Boys  Dismas Njawa mara baada ya kumaliza kongamano.Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.



Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya wavulana Kibiti Boys .Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.

Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT Krantz Mwantepele akiwa katikaa picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya wavulana ya Kibiti Boys mara baada ya Kongamano.Kongamano lililokutanisha wanafunzi wa kidato cha sita wa  shule ya wavulana ya Kibiti Boys wapatao 451 ambapo walipata nafasi ya kujengewa uwezo wa kujiamini na nasaha za maisha ya mafanikio kwa ujumla.Kongamano hilo lilifanyika shuleni hapo wilayani Kibiti mkoani Pwani mapema wiki hii.