Tangazo

October 4, 2017

Airtel yapiga tafu mashindano ya mpira ya Vijana wilaya ya Kinondoni

Meneja Mauzo Kanda ya Dar es Salaam Airtel Tanzania Brighton Majwala (kulia) akimkabidhi vifaa vya mchezo Katibu Mkuu wa Chama cha Soka wilaya ya Kinondoni (KIFA) Funia A. Funia (kushoto) kwa ajili ya mashindano ya Chipukizi Cup yanayotarajiwa kuanza Octoba 8 kwenye viwanja vine vya wilaya hiyo. Wa pili kushoto ni Katibu wa mashindano ya vijana wa wilaya hiyo Abdallah Singano na Meneja Miradi Airtel Tanzania, Jane Matinde.
………………………………………………………

DAR ES SALAAM

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetoa msaada wa vifaa vitakavyotumika kama zawadi katika mashindano ya vijana chini ya umri  wa miaka 17  yajulikanayo kama Chipukizi Cup yanayotegema kutimua vumbi tarehe 8 october 2017  katika wilaya ya kinondoni.

Mashindana hayo yanayoshirikisha timu 64 kutoka katika wilaya ya Kinondoni yatatoa fursa kwa vijana kuchuana vikali , kujifua na kujiweka sawa katika kuchezea vilabu mbalimbali  na hatimae kukuza kiwango cha mpira nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Meneja Masoko kanda ya Dar es saalam , Brighton Majwala alisema “ leo hii tunaungana na chama cha mpira wa soka wilaya ya Kinondoni katika kudhamini mashindano haya kwa lengo la kuwapatia vijana jukwaa la kuonyesha vipaji vyao na kujiweka sawa katika mchezo wa Soka.  Kwa miaka 7 mfululizo tumekuwa tukiendesha mashindano ya mpira kwa  vijana kupitia program yetu ya Airtel Rising Stars na leo tumeona ni vyema kuwafikia vijana mitaani kwa kudhamini mashindano ya mpaira wa miguu katika ngazi ya wilaya ili kuwezesha vijana wengi kuonyesha vipaji vyao na kutumiza ndoto zao”.

“Tunaushukuru uongozi wa mpira wa wilaya ya kinondoni kwa kutualika kushiriki nao ni matumaini yetu kupitia mashindano haya tutaweza kuwaunganisha vijana pamoja, kuchochea kukua kwa mpira wa soka nchini lakini pia kuamashisha mashindano ya mitaani yaweze kufanyika na kuwa na mvuto Zaidi huku vijana wengi Zaidi wakipata nafasi ya kushiriki.

Tunatoa wito kwa vijana na timu zilizojiandikisha kutumia fursa hii vyema kwani mpira wa miguu ni ajira na njia ya kupata kipato.  Airtel tutaendelea kushirikiana na viongozi wa soka katika wilaya mbalimbali nchini katika kuhakikisha tunatoa nafasi kwa vijana kushiriki mashindano kama haya na kuwajenga Zaidi na kuwafanya wawe wanasoka bora ndani na nje ya nchi.”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa soka la vijana wilaya ya Kinondoni, Abdallah Singano alisema “Tunawashukuru sana Airtel kwa kukubali kudhamini mashindano haya kwa kutoa zawadi za washindi.

Ushiriki wa Airtel umeongeza mvuto wa mashindano haya na mwitikio umekuwa mkubwa sana. Hadi sasa tunazo timu 64 ambazo zimekwisha jiandikisha siku ya Jumamosi na Jumapili ili kushiriki mashindano haya, usajiri huu ulifanyika katika viwanja vya KIFA Mburahati, Msasani CCM magunia, Mwananyamala ETIHAD pamoja na uwanja wa Tegeta.

Timu zote ziko tayari na sisi kama wasimamizi wakuu wa mashindano haya tumejipanga kusimamia vyema mashindano haya ili yaweze kuendelea kuleta tija katika soka letu”

Napenda kutoa wito kwa wapenzi wa mpira mashabiki kujitokeza kwa wingi kufatilia michuano hii pindi itakapoanza kutimua vumbi hapo tarehe 8 octoba katika viwanja mbalimbali wilayani Kinondoni, ratiba kamili ya mashindano hayo itatolewa pindi itakapokamilika”

Katika michuano hiyo Airtel imetoa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Jezi, kombe, Soksi , shin guard,  Tshirts, medali,  pamoja na zawadi mbalimblai kwa  wachezaji bora wa michuano hiyo.  Jumla ya Zaidi hizo zina dhamani ya shilingi millioni tano.

Airtel supports youth tournament in Kinondoni district

Airtel Tanzania has donated sports gear to Kinondoni Football Association (KIFA) which will be used during the U-17 Chipukizi tournament scheduled to kick off on October 8 within the district.

The tournament which is expected to feature 64 teams is aimed to give the youth an opportunity to showcase their talents and expose them to coaches who will select a combine youth team for the district.

Speaking in Dar es Salaam during the event to handover the sports gear, Airtel Tanzania Sales Manager for Dar es Salaam region Brighton Majwala said ‘today is a special for us Airtel as we have decided to extend our reach for the youth. As you are aware, Airtel Tanzania has been sponsoring the Airtel Rising Stars for seven years and thus we have decided to sponsor youth teams within district level so that we can have a reach to as many young footballers as possible’.
We appreciate the Kinondoni Football Association (KIFA) for welcoming us to support Chipukizi Cup and I’m sure through this competition we will be able to bring the youth together, said Majwala.

I call upon the teams that have registered to participate the tournament to make full use of the opportunity in order to excel. Airtel Tanzania will continue partnering with other districts and regions in order to make sure that youth football is recognized and supported, added Majwala.

We appreciate Airtel Tanzania for sponsoring this tournament. Airtel presence has added a great happiness and the attendance has been excellence. So far we have a total of 64 teams which have registered and we are ready for kick off on October 8, said Kinondoni District Chairman of youth tournament Abdallah Singano.

I call upon football fans to come up offer motivations to the players during the tournament, added Singano.


In supporting the tournament, Airtel has donated Jerseys, socks, shin guard, Tshirts, medals all worth Tzs 5 million.

No comments: