Tangazo

Showing posts with label BIASHARA. Show all posts
Showing posts with label BIASHARA. Show all posts

June 6, 2018

KAMPUNI YA REGUS YAFUNGUA KITUO KIPYA CHA BIASHARA DAR ES SALAAM

Kampuni ya kimataifa ya Regus, ambayo inajihusisha na kupangisha ofisi za kisasa za muda na za kudumu imefungua kituo kipya cha nne cha ofisi za kupangisha jijini Dar es Salaam. 

 Jengo jipya la ofisi za Regus kwa ajili ya matumizi ya kupangisha ofisi zisizo na usumbufu wa masharti liko eneo la Msasani Penisula, na linazo ukubwa wa mita za mraba 590 kwa ajili ya matumizi ya ofisi za kisasa. 

 “Tumefungua jengo la nne la kituo cha biashara lenye maeneo ya ofisi za kupangisha,hii ni fursa pekee kwa Mashirika Yasio ya Kiserikali,na makampuni ya kimataifa kujipatia sehemu za ofisi za kisasa. Eneo hili la biashara limelenga makundi yote ikiwemo wajasiriamali wanaoanza biashara kwa kuwa bei zake za pango ni za kawaida na rahisi kuzimudu” alisema Joanne Bushell, Meneja wa Regus nchini. 

 Regus imepanua huduma zake kutokana na ongezeko la mahitaji ya ofisi kwa matumizi mbalimbali na kwa gharama nafuu bila kuhangaika kununua samani za ofisi, kuingia mikataba ya kipindi cha muda mrefu na kulipia huduma mbalimbali za matumizi ya ofisi kama umeme na maji.

 Kituo hicho cha biashara cha Regus kinazo ofisi za kupangisha, kumbi za mikutano zenye huduma mbalimbali ikiwemo mawasiliano ya uhakika kupitia mtandao wa internet na simu za mezani, majiko na sehemu za kupumzikia, huduma za usafi, huduma za mapokezi na utawala. Kampuni inao mpango wa kuendelea vituo vingine vya biashara katika siku za usoni kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya ofisi zisizo na masharti na usumbufu, Regus inaendesha vituo vya biashara katika miji ipatayo 900 kwenye nchi zaidi ya 120 duniani,ikiwa inahudumia wajasiariamali wa kawaida, watu binafsi na makampuni makubwa ya kimataifa.

May 23, 2018

Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza kuendelea kuboresha uhusiano wa kibiashara

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akizungumza na baadhi ya maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini, juu ya kuangalia njia bora za kudumisha uhusiano baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini, katika Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dokta Charles Kimei leo amekutana na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Dokta Juma Malewa ili kuangalia njia bora zaidi za kudumisha na kuboresha uhusiano baina ya pande zote mbili. Akizungumza katika mkutano huo ambao pia ulijumuisha maafisa waandamizi kutoka Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza, Dokta Kimei alilishukuru Jeshi hilo kwa kuwa mdau mkubwa wa Benki kupitia mikopo, akaunti za mishahara za askari na SACCOSS ya Magereza ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitoa huduma kwa askari Magereza.


“Nichukue fursa hii kulishukuru Jeshi la Magereza kwa biashara ambayo limekuwa likitupatia, niipongeze SACCOSS ya Magereza kwa uamuzi wa kuwa Wakala wa FahariHuduma, hii si tu itawaongezea kipato kupitia kamisheni za uwakala, pia itasogeza huduma za kibenki karibu na Maaskari Magereza”, alisema Dokta Kimei.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akizungumza katika kikao na uongozi wa Benki ya CRDB, uliomtembelea ofinisi kwake, Makao Makuu ya Magereza jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei. 

Akielezea juu ya fursa mbalimbali zinazotolewa na Benki ya CRDB kwa wafanyakazi Dokta Kimei alisema hivi karibuni Benki imeshusha riba inayo toza katika mikopo binafsi toka 20% mpaka 17%, muda wa marejesho umeongezwa toka miezi 72 hadi miezi 84, wakati kiwango cha kukopa kimeongezwa kutoka shilingi milioni 50 mpaka kufikia Shilingi Milioni 100 hivyo kuwapa wateja wigo mpana zaidi wa kukopa ili kufikia malengo.
Dokta Kimei pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha askari wa Jeshi la Magereza kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo huku akibainisha ya kuwa Benki ya CRDB imeanzisha utaratibu maalum wa kununua madeni na mikopo ya askari kutoka katika Taasisi zingine za Kifedha. Hivyo kutoa fursa kwa askari wenye mikopo Benki nyingine, kukopa toka Benki yao pendwa ya CRDB. Mpaka kufikia mwisho wa mwezi Aprili 2018 tayari Benki ya CRDB ilikuwa imeshakopesha zaidi ya maofisa 5,415 wa Jeshi la Magereza ambapo jumla ya shilingi 29.4 bilioni zilikuwa zimekopeshwa kwao.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa, wakati alipomtembelea ofisini kwake, Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Mkutano huo ulikuwa na lengo kudumisha uhusiano wa kibiashara baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini. 

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Dokta Juma Malewa alimshukuru Dokta Kimei kwa kutembelea Jeshi hilo na kuipongeza Benki ya CRDB kwa maboresho hayo katika huduma zake, huku akiisifu zaidi huduma ya Salary Advance ambayo alisema kwa kiasi kikubwa imesaidia kuboresha maisha ya askari. Dokta Malewa alisema katika maboresho hayo yanayoendelea Jeshi la Magereza lingependa kutumia mfumo wa kibenki katika kukusanya mapato yake katika miradi na huduma mbalimbali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.

“Nikuombe Dokta Kimei na uongozi mzima wa Benki ya CRDB kuona uwezekano wa kuweka huduma za kibenki kama ATM na Matawi kwenye maeneo ya Magereza yenye uhitaji mkubwa wa huduma hiyo”, aliongezea Dokta Malewa. Dokta Malewa pia aliiomba Benki ya CRDB kushiriki katika miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa na Jeshi hilo ikiwamo ujenzi wa hospitali ya Jeshi la Magereza Ukonga, miradi ya Kilimo cha kisasa na chenye tija, mradi wa kokoto Msalato pamoja na uwekezaji katika miradi ya viwanda vidogo vidogo.
Baadhi ya Maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini, wakiongozwa na Naibu Kamishna wa Jeshi hilo, Kamishna Festo Sanga (wa kwanza kulia) wakati wa kikao maalum na uongozi wa Benki ya CRDB, uliotembelea Makao Makuu ya Magereza, jijini Dar es salaam leo.
“Ningependa kuona pia Benki ya CRDB kuwa mteja wa bidhaa na huduma zinazotolewa na Jeshi la Magereza mfano Benki kutumia samani za ofisi na Magereza kupewa Kandarasi za ujenzi wa miradi ya Benki inayodhaminiwa au kumilikiwa na Benki”, aliongezea Dokta Malewa akionyesha fursa ya kibiashara iliyopo baina ya Benki na Jeshi la Magereza.


Dokta Kimei alimhakikishia Mkuu wa Jeshi la Magereza kuwa Benki ya CRDB ipo tayari kushirikiana na Jeshi hilo katika miradi mbalimbali ambayo wamepanga kuitekeleza, huku akihaahidi kutuma timu ya wataalam kutoka Benki ya CRDB kufanya upembuzi yakinifu juu ya kuweka ATM na kufungua vito vya kutolea huduma katika maeneo ya Jeshi la Magereza ilikufikisha huduma kwa akari kwa urahisi.

Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akieleza jambo kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Juma Malewa (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika Makao Makuu ya Magereza, jijini Dar es salaam leo.

“Matarajio yangu ni kuona uhusiano baina yetu ukikua zaidi, naihidi kuwa kupitia Wakurugenzi na Mameneja wetu wa matawi tutaweka utaratibu wa kutembelea ofisi za Magereza nchi nzima ili kuhakikisha haya tuliyokubaliana hapa yanatekelezwa”, alisema Dokta Kimei.


Mkutano huo ulimalizika kwa Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza kutengeneza kikosi kazi cha kufuatilia utekelezaji wa maazimio ambapo Kamishna Gaston Sanga Mkurugenzi wa Utawala, fedha na Rasimali watu wa Jeshi la Magereza alichaguliwa kuwa Mwenyekiti akisaidiwa na Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wakati wa Benki ya CRDB Bi. Jesica Nyachiro. Dokta Kimei pia alimuomba Mkurugenzi wa Masoko wa Benki ya CRDB Bi. Tully Mwambapa kuona namna ambavyo Benki ya CRDB itaweza kuunganisha shughuli zake za misaada kwa jamii na Jeshi la Magereza.


Katika mkutano huo Benki ya CRDB iliahidi kutoa msaada wa kompyuta na vitendea kazi vingine kwa Jeshi la Magereza ili kuongeza ufanisi wa Jeshi hilo. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi April 2018, Benki ilikuwa pia imeshafungua zaidi ya Akaunti elfu tatu (3,000) za mishahara kwa askari wa Jeshi la Magereza.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza.
Baadhi ya Maafisa wa Benki ya CRDB, wakiwa kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa, wakati alipomtembelea ofisini kwake, Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Mkutano huo ulikuwa na lengo kudumisha uhusiano wa kibiashara baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini.
Picha ya pamoja.

WATANZANIA WENGI HAWAFAHAMU KUFANYA MANUNUZI KWA NJIA YA MTANDAO

Na Jumia Tanzania

Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, biashara nyingi Tanzania na duniani kote zimehamia kwenye mifumo ya mtandao wa intaneti. Ni miongoni mwa sekta inayokua kwa kasi hivi sasa ikiwa imechangiwa na kuendelea kubadilika kwa tabia za wateja kila kukicha wakiwa na mahitaji mapya. 


Biashara kupitia mtandao wa intaneti inawaruhusu wateja kubadilishana taarifa mbalimbali juu ya huduma na bidhaa zinazouzwa mtandaoni kukiwa hakuna vikwazo vya muda au umbali. Inatarajiwa kuwa ndani ya kipindi cha miaka michache ijayo, makampuni mengi yatakuwa yamehamishia huduma zao katika njia ya mtandao. Wataalamu wanapendekeza kuwa, endapo biashara kwa njia hii zikifanyika kwa usahihi zina manufaa makubwa ikiwemo; uharaka, unafuu, na ni rahisi zaidi ukilinganisha na njia za kawaida zilizozoeleka.    


Tumekuwa tukishuhudia wafanyabiashara wengi wakitangaza kuhusu bidhaa na huduma wanazozitoa kupitia njia mbambali za mitandaoni kama vile Facebook, Twitter na Instagram. Wengi wao wamekuwa wakiwataka wateja wao kutembelea kurasa zao na kuchagua bidhaa zao kisha wapelekewe mpaka walipo. Lakini je, hii ndio maana halisi ya biashara kwa njia ya mtandaoni?


JUMIA ni kampuni inayojishughulisha na biashara tofauti kwa njia ya mtandao wa intaneti barani Afrika, ambapo kupitia tovuti yake huwakutanisha wauzaji na wanunuzi mbalimbali kwa urahisi. Kupitia tovuti yake, maelfu ya wauzaji na wanunuzi wanaweza kufanya biashara bila ya kuonana isipokuwa kubadilishana taarifa. 



Kwa mfano, mteja akiingia kwenye mtandao huu anachoweza kukiona ni orodha ya bidhaa nyingi kutoka kwa wauzaji tofauti, akachagua anazohitaji, akajaza taarifa zake binafsi, akachagua njia ya malipo na hatimaye kutaarifiwa ni lini mzigo wake utamfikia. Kumbuka, mlolongo wote huo unaweza kufanyika bila ya mawasiliano au kuonana uso kwa uso baina ya pande zote mbili.  


Makala haya yamejaribu kuangazia kuhusu uingiaji wa sekta hii nchini Tanzania na namna ilivyopokewa na wateja. Miongoni mwa mambo yatakayozungumziwa humu ni pamoja na nafasi ya kitengo cha huduma kwa wateja katika kutoa huduma na elimu kwa wateja. 


Akifafanua umuhimu wa kitengo cha huduma kwa wateja cha Jumia Tanzania, Mkurugenzi Mkuu, Bw. Zadok Prescott ameelezea kuwa wateja wengi bado hawafahamu huduma zinazotolewa na kampuni yake ukilinganisha na makampuni mengine yanayojihusisha na biashara za mtandaoni nchini Tanzania. 




“Jumia ni tovuti PEKEE ya biashara mtandaoni Tanzania inayomhakikishia mteja bidhaa mpya na halisi (orijino), au kurudishiwa pesa yake kama haitokuwa hivyo. Mteja akishafanya huduma mtandaoni na kujaza taarifa zake hupelekewa bidhaa zake mpaka alipo, ndani ya siku chache tu mara ya baada ya kufanya huduma. Pia ni tovuti PEKEE ya biashara mtandaoni Tanzania unayoweza kulipia pindi unapofikiwa na bidhaa yako kwa jijini Dar es Salaam, hivyo ni salama kwa mteja endapo atakuwa na hofu ya kutapeliwa. Kama haitoshi tunawaruhusu wateja kurudisha bidhaa bila ya makato yoyote, kama ni kinyume na walivyoagiza,” alifafanua zaidi Prescott.


Ni dhahiri kwamba Watanzania wengi bado ni wageni na teknolojia za kisasa hususani hii ya kufanya biashara kupitia mtandao wa intaneti. Miongoni mwa wengi wao wamezoea kwenda moja kwa moja dukani na kununua bidhaa wanazotaka au watakazoziona. Kwa hiyo hapa mteja anakuwa na fursa finyu ya kuonana na wauzaji mbalimbali kwa sababu itamlazimu kutumia muda mwingi.


Akifafanua hilo, Bw. Prescott amesema kuwa Jumia inayo timu maalum ya huduma kwa wateja. Timu hiyo imejikita katika kuwasaidia wateja kufanya na kufanikisha huduma kuanzia hatua ya kwanza mpaka ya mwisho. Kwa sababu wanafahamu kuwa wapo Watanzania wengi bado hawajajaribu kufanya manunuzi kwa njia ya mtandao. Na kuna uwezekano wengine walipojaribu kufanya hivyo walitaka kutapeliwa.


Amesema kuwa wameaona ni vema kuwa na timu hiyo kwa sababu wateja wengi hawana imani huku wengine wakiwa na hofu. Wengi wao bado wanaamini hawawezi kununua bidhaa bila ya kuiona kwa macho, kuikagua na kujiridhisha na pengine mpaka kuijaribisha kabisa.



“Kama walivyo wateja wengine duniani, Watanzania pia huzingatia bei pamoja na ubora. Wanahitaji bidhaa bora zenye bei nzuri na zinazowafikia kwa njia rahisi. Lakini kikubwa na cha msingi ni uaminifu. Haya ndiyo masuala ya msingi yanayozingatiwa na Jumia ambayo hayapatikani kwa kampuni zingine Tanzania.”



Kutokana na wateja wengi kujizoesha utamaduni huo, Jumia inakumbana na changamoto ya wengi kutokuwa na imani na mitandao inayoibuka kila kukicha. Katika kuhakikisha wanaaminiwa na wateja wake Jumia hufanya yafuatayo:   


“Watanzania bado hawaitumii ipasavyo huduma bora za manunuzi na uuzaji zinazotolewa na Jumia. Wengi wao bado wanashindwa kutofautisha kati ya kampuni ya biashara mtandaoni iliyojikamilisha kama Jumia, na mitandao mingine ya kawaida ambayo kila mtu anaweza kuuza na kununua bidhaa. Tofauti ya Jumia na mingineyo ni kwamba, mteja anapaswa kulipia bidhaa pale inapomfikia, tena ikiwa halisi na ubora alioutarajia.”


“Tunachoweza kuwaahidi wateja wetu ni kuwapatia idadi kubwa ya bidhaa tofauti kwa bei nzuri na kuwafikishia pale watakapohitaji,” aliongezea na kumalizia Bw. Prescott, “Jumia imejikita zaidi katika kuokoa MUDA na PESA kutoka kwa wateja wake - bidhaa adimu kabisa duniani!” 

May 22, 2018

UBA Restates Commitment to Growing Infrastructure, Deepens Financial Inclusion in Tanzania

UBA Tanzania, a subsidiary of the UBA Group, a pan African financial institution with presence in 20 African countries, Monday restated its commitment to support the Tanzanian government’s initiative to grow the country’s infrastructure, while also affirming the bank’s obligation to deepen the retail banking space in the country.

The assurance was given during a press conference addressed by the Bank’s Chief Operating Officer, Chris Byaruhanga in Dar Es Salaam, noting that as a member of UBA Group with asset of over $13 billion, the Tanzanian franchise has the capacity to finance any project irrespective of amount or size. “UBA Tanzania, relying on the strength of our group has capacity to finance any transactions irrespective of its size in either private or public sector. As a pan African with presence in key international markets of the world, we are positioned to provide the necessesary financial intermediation critical to the development of Tanzania,” says Byaruhanga.

Byaruhanga further informed the journalists of the key projects that have been financed by the Bank in Tanzania in recent times, including the provision of over $25 million facility for the construction of Kigogo Road in Dar Es Salaam and TZS15BN/- support Tanzania Electricity Supply Company (TANESCO), among other interventions. 

“Apart from these involvements, UBA Tanzania, a bank with strong retail base has come up with many innovations, especially in digital space to provide financial solutions to the needs of the banking consumers in this market,” the COO said while explaining the Bank’s strategy, claiming further that UBA Tanzania prioritises businesses whether they are small and medium scale enterprises (SMEs) or large corporates.

Speaking on the roles being played by UBA Group in the support of the economic development of the African continent, Nasir Ramon, Head, External Relations of UBA Plc, said UBA Group has continuously played big in the continent’s financial sector, saying that the UBA has committed over $5 billion into various projects on the continent in recent times.

United Bank for Africa is one of Africa’s leading financial institutions, with operations in 20 countries and 3 global financial centers: London, Paris and New York. From a single country operation in Nigeria, Africa’s largest economy, UBA has evolved into a pan-African provider of banking and related financial services through diverse channels globally.

UBA Tanzania is a subsidiary of UBA Plc and licensed by the Bank of Tanzania.  The Bank has been in Tanzania since 2009 and has continued to play a critical role in the Tanzania banking industry. UBA Tanzania offers a full range of banking products catering for large local corporates, public sector clients and multinational corporations that include trade finance lines, working capital facilities, collection solutions and robust payment platforms.

May 14, 2018

COCA-COLA BONITE YAZIDI KULETA RAHA YA MZUKA WA SOKA NA COCA KANDA YA KASKAZINI

 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
Mmoja wa washindi wa fedha taslimu akipokea zawadi yake Wakati mashindano ya kombe la Dunia 2018 yanakaribia, kampuni ya Coca-Cola Bonite Bottlers Limited ya mjini Moshi inazidi kumwaga zawadi za pikipiki,luninga za kisasa na fedha taslimu kwa wakazi wa Kanda ya Kaskazini kupitia promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka inayoendelea. Akiongea katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi 16 wa wiki liyopita, Meneja Mauzo wa Bonite, mkoa wa Arusha Bw. Boniphace Mwasi, alisema zaidi ya wateja 50 wamejishindia zawadi na zawadi bado ziko nyingi. “Bado tunazo zawadi nyingi hivyo natoa wito kwa wakazi wote wa kanda ya kaskazini kuchangamkia kunywa soda za Coca-Cola, ili waweze kujishindia zawadi”. Wakiongea muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi zao washindi waliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa kubuni promosheni zenye mwelekeo wa kuleta furaha kwa jamii hususani kwa kuwakwamua kiuchumi.

May 9, 2018

MKAZI WA ZANZIBAR ASHINDA BIDHAA ZENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 1 KUTOKA JUMIA


 MKAZI  wa visiwani Zanzibar, Bi. Patricia Philipo amejishindia vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka Jumia kupitia kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ katika mwezi uliopita wa Aprili.  

Mshindi huyo alipatikana kupitia kampeni iliyoendeshwa kwa jina la ‘Big Home Makeover’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. Wateja walitakiwa kupendekeza mtu wao wa karibu ambaye waliona anastahili nyumba yake kupendezeshwa na Jumia kwa kupatiwa ofa ya vyombo vya ndani.

Bi. Patricia Philipo aliibuka mshindi baada ya mchumba wake Bw. Mwalim Juma Kumpendekeza ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa.

“Mimi ni mteja mzuri wa Jumia kwa sababu naitumia mara kwa mara kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali ambazo zimekuwa zikinifika mpaka ninakoishi Zanzibar. Baada ya kuliona hili shindano, niliona ni vema nimpendekeze mwenzangu ashinde. Ukizingatia tupo kwenye maandalizi ya ndoa yetu, suala la mahari pamoja na vyombo vya ndani ni gharama hivyo ushindi wake ungekuwa na mchango mkubwa kwenye shughuli yetu,” alisema Bw. Juma ambaye ni mchumba wa mshindi wa kampeni hiyo, Bi. Patricia.

“Sikuwa na wasiwasi kwamba endapo angeshinda asingeweza kupatiwa zawadi zake. Kwa sababu hapo nyuma kulikuwa na mashindano kadhaa kama vile ‘Treasure Hunt’ kipindi cha Mobile Week, wateja walikuwa wanashinda simu na kukabidhiwa bila ya ubabaishaji wowote,” alimalizia Bw. Juma.

Akielezea furaha yake mara baada ya kutangazwa mshindi Bi. Patricia Philipo amesema kuwa, “kusema ukweli hapo mwanzo sikutarajia kama ningeweza kushinda kutokana na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wangu. Kuna wakati nilitaka kukata tamaa kwa sababu mwenzangu alikuwa ameniacha mbali, mashabiki wake walikuwa wanamuunga mkono na kuwashirikisha wengine kwa kiasi kikubwa.”

“Lakini niliongeza bidii na kumuomba Mungu ili niweze kufanikiwa. Na kweli ilifika mahala mpinzani wangu akakata tamaa. Hapo ndipo mimi nilipoongeza bidii zaidi na kufanikiwa kuibuka mshindi,” aliongezea Bi. Patricia na kuhitimisha, “nina furaha kubwa katika kipindi hiki kwani zawadi niliyoshinda ni kubwa. Vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni moja si jambo la kawaida. Jumia wameweka alama kubwa katika maisha yangu na nawaombea waendelee kuwajali wateja wao kwa bidhaa bora, ofa lukuki pamoja na kuwa waaminifu.”

Kampeni ya ‘Big Home Makeover’ kutoka Jumia iliyodumu kwa takribani mwezi mmoja, ilikuwa na dhamira ya kuwawezesha wateja wake kununua vyombo vya ndani kwa gharama nafuu. Lakini pia ilitoa fursa ya kumzawadia mteja mmoja aliyependekezwa na mtu wake wa karibu vyombo vya ndani vyenye thamani ya shilingi milioni mmoja. 

“Tunampongeza mshindi wetu Bi. Patricia kwa ushindi aliojipatia lakini pia tunawasihi wateja wetu kuchangamkia bidhaa mbalimbali kwenye mtandao wetu. Kupitia mtandao unaweza kuokoa muda na gharama pamoja na usumbufu wa kufuata bidhaa. Lakini cha muhimu ni njia salama na ya uhakika, Jumia inawapatia fursa wateja wake kufanya manunuzi na kisha kulipia baada ya kuridhika na mzigo aliofikishiwa,” alisema Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey.

“Hivi sasa kupitia mtandao wetu tunaendesha kampeni ya kutoa punguzo kubwa la bei ambalo hauwezi kupata sehemu yoyote. Kwa mfano, simu zinazouzwa Jumia ni pungufu ya shilingi 50,000 tofauti na ukienda kwenye maduka moja kwa moja, vivyo hivyo kwa bidhaa nyinginezo, kila bidhaa utakayoiona basi ujue imepunguzwa kiasi hicho! Tunawasihi watanzania wasicheze mbali na jumia ili kuweza kunufaika na mambo haya mazuri,” alihitimisha Geofrey.      
 Mchumba wa mshindi, Bw. Mwalim Juma aliyependekeza mchumba wake  ashinde zawadi ya vyombo hivyo ili kumrahishia asije kusumbuka kununua tena pindi watakapofunga ndoa akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa hundi iliyofanyika Dar es Salaam jana.
 Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey.
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa mshindi huyo akikabidhiwa hundi yake.
Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey 
( kulia), akimkabidhi Bi.Patricia Philipo mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 1 baada ya kuibuka mshindi. Katikati  Mchumba wa mshindi, Bw. Mwalim Juma aliyependekeza mchumba wake  ashinde zawadi ya vyombo hivyo.

May 4, 2018

WAZIRI MWIJAGE AKABIDHI TUZO ZA RAIS ZA VIWANDA(PMAYA)

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage,  akimkabidhi Tuzo ya Mshindi wa pili wawakilishi wa Kampuni ya PLASCO Ltd, kutoka (kushoto) Unguu Sulay, Edith James na Alimiya Osman, wakati wa hafla ya Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo mchana. Picha zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO)
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, (wa pili kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mshirika wa Taasisi ya Kaizen Tanzania, James Alva, wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho katika hafla ya utoaji Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, akimkabidhi Tuzo ya Mshindi wa jumla Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL Group, Roberto Jarrin, wakati wa hafla ya Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, akimkabidhi Tuzo ya Mshindi wa kwanza katika Makampuni matatu makubwa (TOP 3) Meneja wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Helene Weesie, wakati wa hafla ya Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Charles Kimei.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, akimkabidhi Tuzo Meneja Rasilimali watu  wa Kampuni ya Alaf Tanzania, Daphne Kakonge, wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Rais za Viwandani. 
Afisa Masoko wa Kampuni ya Alaf Tanzania, Theresia Mmasy, akipokea cheti cha shukrani wakati wa hafla hiyo.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, akimkabidhi Cheti cha kutambua mchango wa udhamini mwakilishi wa Kampuni ya IPP, Paul Urio, wakati wa hafla ya Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, akimkabidhi Cheti cha kutambua mchango wa udhamini Mwenyekiti wa Kampuni ya Montage, Nestory Mapunda, wakati wa hafla ya utoaji Tuzo za 13 za Rais za Viwanda, (PMAYA) iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
 Na Muhidin Sufiani, Dar

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amesema kuwa azma ya kukua kwa uchumi unategemea sekta ya viwanda na hakuna budi kuhakikisha wanatimiza vigezo vya uchumi ili ukue kwa asilimia 12 kwa mwaka, pato la taifa lisipungue chini ya asilimia 15 na ajira kuongeza kwa asilimia 40 ya ajira zote.

Mwijage amesema hayo wakati wautoaji tuzo za Rais za Viwanda (PMAYA) kwa mwaka 2017 zilizofanyika leo Jijini Dar es salaam na kuwataka Shirikisho la Viwanda (CTI) kuwa wabunifu na kuzitangaza bidhaa zao ili kuweza kuingiza mapato ya asilimia 25 ya fedha za kigeni.

Akizungumza wakati wa utoaji tuzo hizo, Mwijage amesema kuwa serikali ya awamu ya tano toka iingie madarakani imeweza kuendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara na kuwezesha kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

"Mpaka sasa toka Desemba 2015 tayari tumewahamasisha wawekezaji wa ndani na wa kujenga viwanda vipya 3,306 na tunawapongeza wawekezaji wa ndani nannje kwa kuchagua kuwekeza Tanzania na kuunga mkono serikali yetu ya kukuza uchumi wa viwanda kufikia 2025, " amesema Mwijage.

" Natambua kuwa baadhi yenu mna madai mbalimbali ya kurejeshewa malipo yenu yakiwemo ya ushuru wa forodha ya 15% ya ziafa kwenye uaguzaji wa sukari kwa ajili ya matumizi ya viwanda na malipo ya marejesho ya ongezeko la thamani," 
Mwijage amesema zipo changamoto zinazotokana na wenye viwanda wenyewe ikiwemo udhaifu wa kutafuta masoko ya ndani na nje ya nchi ya Tanzania unasababisha bidhaa za ndani kutokufahamika vizuti miongoni mwa watanzania na watuamiaji wa nje.

Mwijage amesema kupitia baraza la Taifa la Uwekezaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) itahakikisha watanzania wote wanashiriki katika ujenzi wa uchumi. Serikali kupitia baraza la uwezeshaji lina miradi ya kimkakati ya kusaidia viwanda vyetu na watanzania kwa ujumla kupata fursa mbalimbali zilizopo. 

Kwa upande wa Mwenyekiti wa CTI Dkt. Samwel Nyantahe ameishukuru serikali kwa kuweka mijadala ya kuwasaidia watanzania wafanyabiashara hasa wenye viwanda  na baada ya serikali ya awamu ya tano kuja na sera ya ujenzi wa viwanda watanzania wengi wamejitokeza kuanzisha viwanda mbalimbali kwa azma ya kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya tano ya kujenga uchumi wa viwanda.

Aidha ameeleza kuwa katika maadhimisho ya miaka 13 katika utoaji wa tuzo mwaka 2016 mheshimiwa Rais alipendekeza kuhusisha sekta zote na wasio wanachama  wahusishwe na tuzo ya matumizi bora nishati viwandani ilianzishwa.

Mashindano hayo yataleta ushindani mkubwa katika sekta ya viwanda hali itakayopelekea kukuwa kwa uchumi  na kuongeza pato la taifa.

Katika tuzo za mwaka 2017  kampuni ya bia ya Tanzania Breweries (TBL)  iliweza kupata ushindi wa jumla katika viwanda vyote vinavyozalisha bidhaa mbalimbali wakifuatiwa na Zenufa na mshindi wa tatu ni Plasco  Ltd

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

TTCL PESA YABADILI JINA NA NEMBO SASA NI T PESA

 Kampuni ya Mawasiliano Tanzania (TTCL), imebadili nembo na jina la iliyokuwa TTCL Pesa na sasa kujulikana kama T Pesa baada ya Uzinduzi uliofanyika jijini Dodoma leo. (Picha:Mroki Mroki-Daily News Digital)
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL CORPORATION), Waziri Kindamba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Nembo ya na jina lipya la TTCL Pesa.
 Meza Kuu ikifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
  Meza Kuu ikifuatilia matukio wakati wa uzinduzi huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL Corp, Omar Nundu akizungumza.
 Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilaino (Sekta ya Mawasiliano), Atashasta Nditiye akizungumza wakati wa usimduzi huo. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

May 3, 2018

UBA Shareholders Hail Performance, Higher Dividend Payout

Shareholders of United Bank for Africa (UBA) Plc on Monday hailed the board and management of the bank for the impressive performance recorded in 2017 and were highly pleased with the remarkable contributions of its African subsidiaries that accounted for over 45 percent of the group’s income.

The shareholders gave the commendation at the 56th annual general meeting in Lagos. UBA posted profit after tax (PAT) of USD237 million for the 2017 financial year and recommended a total dividend of 0.3 USD cents per share, which was ratified at the AGM. 

Speaking at the meeting, the Chairman, Progressive Shareholders Association of Nigeria, Mr. Boniface Okezie: “I want to specially commend the Board and Management of UBA, especially the Chairman, Tony Elumelu and Group Managing Director/CEO, Kennedy Uzoka, whose leadership, has brought tremendous progress to this great institution in the past two years. 

We, the shareholders, are impressed with results that you have recorded so far and the achievements that the bank has recorded under your leadership, especially the sterling contributions of our subsidiaries in Africa. We are impressed with the continuous penetration of the Group’s franchise and market share gain across Africa. 

UBA has further demonstrated that Africa can nurture great companies and great things can be originated from Africa. UBA has showcased a high level of ingenuity in the banking space, and we are glad with the attendant value creation for shareholders and the broader stakeholders.”

Another shareholder, Mr. Timothy Adesiyan, commended the Management for being the African bank to pioneer Artificial Intelligence technology, with the launch of UBA’s Virtual Banking Robot, named “Leo”, a Chatbot which enhances lifestyle banking, as it enables customers to carry out all forms of basic banking transaction through Facebook chat. 

Also, speaking at the General Meeting of Shareholders of the Group, Nonah Awoh, who commended the bank for the performance, equally tasked the management to do more to ensure that all the African subsidiaries contribute at least 50 per cent to the bottom-line of the Group in the near future.

In his address to shareholders, Elumelu, said the bank recorded strong growth in both top and bottom lines in 2017.

He said: “Overall, our bank grew profit before tax by 16.1 per cent to USD318 million. More importantly, the bank remains financially strong, with BASEL II capital adequacy ratio of 20% well ahead of the 15% regulatory requirement in Nigeria and the Group’s capital adequacy ratio of 25% ranks one of the highest amongst Sub-Sahara African banking groups. 

More importantly, the Group remains very liquid, reinforcing the strength of our balance sheet. 

We recently opened for business in Mali, as we see the economy of Mali to be very viable, with strong growth prospects for us and other corporates in that market. Mali is a strategic fit for our Group and this time and the corporates and SMEs in Mali will benefit from our expertise and banking capacity in varying sectors of the economy, in addition to our value proposition to the retail customers, who can efficiently leverage our digital banking offerings to facilitate their banking transactions with ease. 

Hence, we see us adding a lot of value to the Malian economy and we expect positive profit contribution to our Group from this new subsidiary, going forward.  

On his part, Uzoka, the Group Managing Director/CEO said: “UBA has built a great brand that is recognised all over the world, and because of this, we have decided to be customer centric. This means our focus is on putting our customers first in all we do by making sure that we do things from the customers’ standpoint.”
Group Managing Director/CEO, United Bank for Africa(UBA) Plc, Mr. Kennedy Uzoka, Group Chairman, UBA Plc, Mr. Tony Elumelu; Company Secretary, Mr. Bili Odum; and Group Deputy Managing Director, Mr. Victor Osadolor, at the 56th Annual General Meeting of the Bank held in Lagos
 Group Managing Director/CEO, United Bank for Africa(UBA) Plc, Mr. Kennedy Uzoka; Group Chairman, UBA Plc, Mr. Tony Elumelu; Company Secretary, Mr. Bili Odum; Group Deputy Managing Director, Mr. Victor Osadolor; and Director, Ambassador Adekunle Olumide, at the 56th Annual General Meeting of UBA Plc  held in Lagos on Monday

April 27, 2018

COCA-COLA NYANZA BOTTLERS YAMWAGA ZAWADI ZA PROMOSHENI YA 'MZUKA WA SOKA'

Kampuni ya Coca-Cola Nyanza Bottlers ya Mwanza imemwaga zawadi kwa washindi wa promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka inayoendelea.Wakazi 16 wa kanda ya ziwa wiki hii wameweza kukabidhiwa zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki 7,luninga bapa 7,na 2 fedha taslimu.

Zawadi hizo zimekabidhiwa na Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni hiyo,Samwel Makenge,ambaye alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia vinywaji vinavyotengenezwa na kampuni ya Coca-Cola iliwaweze kujishindia zawadi kwa kuwa bado ziko nyingi.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Washindi wa zawadi za Coca-Cola wakipokea zawadi zao kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Coca-Cola kanda ya ziwa,Samwel Makenge katika hafla iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza mkoani Mwanza.
Baadhi ya washindi katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa zawadi zao.