Tangazo

Showing posts with label dini. Show all posts
Showing posts with label dini. Show all posts

September 11, 2017

ASKOFU CHARLES GADI AWAONGOZA WAUMINI KUWAOMBEA WALIOATHIRIKA KWA KIMBUNGA FLORIDA NA TEXAS MAREKANI

 Askofu Charles Gadi  wa Huduma ya Good News for all Ministry (katikati), akiwaongoza waumini wa kanisa lake Dar es Salaam jana,wakati wa kuwaombea walioathirika kwa kimbunga katika miji ya  Florida na Texas nchini Marekani
 Askofu Charles Gadi  wa Huduma ya Good News for all Ministry (katikati), akiwaongoza waumini wa kanisa lake Dar es Salaam jana,wakati wa kuwaombea walioathirika kwa kimbunga katika miji ya  Florida na Texas nchini Marekani.

September 4, 2017

KANISA LA ABC LASIMIKA WACHUNGAJI WAKE NA KUWEKA WAKFU WAANGALIZI, LAWATAKA KUWAUNGANISHA WATANZANIA

 Askofu Mkuu wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC), Rev. Flaston Ndabila, akitoa mahubiri  katika ibada  maalumu ya kuwasimika wachungaji watano na kuwawekea wakfu wengine watano kuwa waangalizi wa kanisa  hilo katika ibada iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

 Mwangalizi  wa Kimataifa wa Makanisa ya Christ Apostolic Church (CAC), kutoka  America ya Kaskazini, Mchungaji Dk.Timothy Omolayo Agbeja akiwasalimia waumini wa kanisa hilo. Mchungaji Agbeja aliongoza ibada hiyo. Kulia ni Mtumishi wa Mungu, Zephaniah Andrew Nyambele ambaye alikuwa ni Mkalimali katika ibada hiyo. 

August 31, 2017

SABABU YA EID-AL-ADHA KUITWA 'SIKUKUU YA KUCHINJA'


Na Jumia Travel Tanzania

Eid al-Adha ni miongoni mwa sikukuu kubwa kwa waumini wa dini ya Kiislamu ukiachana na Eid- al-Fitr inayosherehekewa kila mwaka duniani kote. Kwa mwaka huu sikukuu hii inatarajiwa kusherehekewa siku ya Ijumaa ya Septemba mosi ambapo kwa waumini wa dini hiyo ni kipindi cha kujitolea, kuonyesha ukarimu kwa marafiki, familia na watu wenye uhitaji.

Kama zilivyo sikukuu nyingine kuna baadhi ya watu huwa hawajui ni kwa nini huwa zinaseherehekewa namna zinavyosherehekewa. Jumia Travel kupitia makala haya imekukusanyia mambo ya msingi kuhusu maana ya sikukuu hii na namna ya kusherehekea.

August 18, 2017

NI MLIPUKO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA, USIKOSE!

Karibu kwenye mkutano huu mkubwa wa Injili uliondaliwa na kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza. Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola atakuwa mwenyeji wa Mchungaji Mathias Roggers kutoka Marekani pamoja na waimbaji mbalimbali. Usikose!

July 23, 2017

ASKOFU GAVILLE ASEMA, KATIBA MPYA NDIYO MUAROBAINI WA UFISADI

Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Blaston Gaville (kushoto).

June 27, 2017

SWALA YA EID EL FITRI KITAIFA MKOANI KILIMANJARO

Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa akiwasili katika msikiti wa Riadha mjini Moshi kwa ajili ya Swala ya Eid el Fitri iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa aikishiriki Swala ya Idd el Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakishitiki Swala Idd.
Swala ya Idd ikifanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa,akiwa na Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Zubery ,Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu ,Said Mwema.
Mshindi wa kuhifadhi Quran tukufu ,Ibrahim Mitigo akionesha namna ambavyo alivyohifadhi Quran wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki Swala ya Idd mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ,akizungumza wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika kitaifa katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Mufti wa Tanzania na Sheakh Mkuu,Abubakary Bin Zubery akitoa nasaha zake wakati wa Swala ya Idd iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki katika Swala ya Idd El Fitry iliyofanyika mskiti wa Riadha mjini Moshi

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI imeahidi kuongeza kasi katika zoezi la ukamataji wa wahusika wa matukio ya mauaji yaliyotokea Kibiti,Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani na kuhakiksha wanafikishwa mbele ya vyombo vya sharia.
Waziri Mkuu wa Tanzania ,Kassim Majaliwa aliyasema hayo jana katika baraza la Idd lililofanyika kitaifa katika mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro lkitanguliwa na Swala ya Idd El Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha.
“Kinachofanyika sasa nikuhakikisha kwanza tunawapata waharifu halisi ilikuepuka kuingiza watu wasio husika, kama vile hao wenye hisia kwamba mauaji haya yanafanywa labda na waislamu hapana .”alisema Mh Majaliwa .
Alisemakaz kubwa inayofanywa sasa ni kuchuja na kujua nani hasa anshiriki katika mauaji hayo huku akiwashukuru watanzania ambao tayari wameanza kutoa ushirikiano kwa kuanza kueleza nani wanahusika katika tukio hilo.
“Kazi yetu ni kuwapeleleza pale ambapo tunauthibitisho wa ushiriki wao na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na kazi hiyo inaendelea vizuri.”alisema Majaliwa.
Mapema katika taarifa ya Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) iliyosomwa na kaimu katibu Mkuu,Sheakh Salim Amir Abeid alisema Bakwata imeshtushwa na matukio ya mauaji ya kutisha ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa Pwani.
Alisema kutokana na matukio hayo Baraza kuu linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika matukio hayo aliyoyataja kutokuwa na hata chembe ya kibinadamu .
“Kumekuwepo na matukio ya kutisha ya mauaji ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa Pwani,matukio ambayo yametushtua sana na kuisikitisha mioyo yetu,baraza kuu la waislamu la Tanzania kwanza kabisa linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika matukio hayo ya kinyama yasio na chembe ya kibinadamu hata kidogo.”alisema Abeid
Alisema Bakwata inasikitishwa na vitendo vyenye viashiria vya kutaka kuichafua dhima nzuri ya Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani na utulivu hasa pale matukio hayo yanapo husishwa na na Dini ya Kiislamu.
“Uislamu ni dini ya amani upendo kuvumilia na nakuishi pamoja na watu wa imani tofauti na kwamba yeyote afanyae matendo yoyote na kinyama kama hayo katu haiwakilishi uislamu na baraza linawataka waislamu kushikamana.”alisema Abeid.

June 26, 2017

RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI, ALLY HASSAN MWINYI ASHIRIKI NA WATOTO YATIMA KATIKA FUTARI ILIYOANDALIWA NA AAR INSURANCE

Rais Mstaafu awamu ya pili Mhe. Ally Hassan Mwinyi (Kushoto) akimpa maelekezo ya chakua alichokuwa anakula wakati aliposhiriki hafla fupi ya kufuturisha watoto Yatima wa kituo cha Kigogo iliyoandaliwa na Kampuni ya  Bima ya AAR  jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakipakua futari.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bima ya AAR wakiwapakulia wageni futari.
Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni ya Bima ya AAR, Agnes Batengas akiwangoza watoto kwenda kuchukua futari.
Rais Mstaafu wa Awamu ya pili, Ally Hassan Mwinyi akitoa machache mara baada ya kukaribishwa kutoa nasafa zake.
Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni ya Bima ya AAR, Agnes Batengas akitoa shukrani zake za pekee kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassan Mwinyi mara baada ya kushiriki futari na watoto yatima wa kituo cha kigogo jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Mauzo Kampuni ya AAR Insurance Tabia Masoud akiwahudumia chakula watoto Yatima kutoka kituo cha Kigogo katika hafla fupi ya kufuturisha iliyofanyika jijini Dar es salaam.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassan Mwinyi akitoa shukrani zake za pekee mara baada ya kushiriki futari na watoto yatima wa kituo cha kigogo iliyoandaliwa na kampuni ya Bima ya AAR.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Bima ya AAR, Violeth Mordichai akizungumza wakati wa hafla fupi ya kufuturisha watoto Yatima kutoka kituo cha Kigogo jijini Dar es salaam.
Rais Mstaafu awamu ya pili Mhe. Ally Hassan Mwinyi (Kulia) akimkabidhi wa zawadi na Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni ya Bima ya AAR, Agnes Batengas (Kushoto) wakati wa hafla fupi ya kufuturisha watoto yatima kutoka kituo cha Kigogo jijini Dar es salaam jana.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Bima ya AAR wakipiga picha ya pamoja na watoto Yatima mara baada ya kuwakabidhi zawadi katika hafla fupi ya kufuturisha watoto yatima kituo cha kigogo jijini Dar es salaam na kuwapa misaada ya chakula, nguo na viatu kwa ajili ya sikukuu ya Eid El Fitri.
---
Dar es salaam: Kampuni ya Bima ya AAR imefuturisha watoto yatima kutoka kituo cha kigogo Jijini Dar es salaam. Hafla hiyo iliyohudhuriwa na Raisi Mstaafu awamu ya pili Mhe. Ally Hassan Mwinyi, pamoja nawahamasishaji mbali mbali katika jamii wanaigusa jamii kwa namna tofauti tofauti. 

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Raisi Mstaafu hawamu ya pili Mhe. Ally Hassan Mwinyi alishukuru kampuni hiyo kwa hafla hiyo ya pamoja kwa kuweza kufuturu na watoto yatima na kugawa mahitaji mbalimbali ikiwemo nguo, viatu na vyakula.
“Ningependa kuwashukuru kampuni ya AAR kwa futari hii pia kuwapongeza katika kazi mbali mbali mnazofanya katika kusaidia jamii kwa ujumla uhusani kwenye swala la afya. Mwezi huu unatukumbusha kufanya yaliyo mema, kusaidia wasiojiweza, kusamehana na kukumbushana mda wa ibada.” Alisema

Aidha wakati wa hafla hiyo Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Violeth Mordichai aliwakabidhi watoto hao mahitaji hayo na kuongeza kuwa, futari hiyo ni sehemu ya mpango wake kusaidia jamii hivyo ni vyema katika kipindi hiki wakafuturu pamoja na watoto hao.

“ sisi kama kampuni ya Bima iliyojikita katika kusaidia jamii kwenye swala la afya tumeona ni jambo jema katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhani tukapata chakula cha pamoja na watoto yatima kutoka kituo cha kigogo na kuweza kusaidia kwa kuwapa msaada wa mahitaji madogo yatakayoweza kuwasaidia ,hata kipindi cha sikukuu ya Eid el fitri ” alisema

Pia aliongeza na kusema kwa wale ambao hawajajiunga na huduma zinazotolewa na Kampuni hio wajiunge ili kupata huduma bora ya afya.

June 23, 2017

MRITHI WA DKT. MDEGELA KKKT DAYOSISI YA IRINGA, MCHUNGAJI BLASTON GAVILE KUWEKWA WAKFU JUMAPILI



Askofu Mteule Mchungaji Blastone Tuluwene Gavile (kushoto) akiwa na Msaidizi wa Askofu Mteule Mchungaji Himid  John Sagga.

IBADA ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Mchungaji Blaston Tuluwene Gavile, inatarajiwa kufanyika Jumapili Juni 25, 2017 mjini Iringa.

June 22, 2017

WANAWAKE WA KANISA LA PENTEKOSTE TANZANIA WAFANYA KONGAMANO LA TATU JIJINI DAR

 Askofu Saldonie Simon Sinde akiwasalimia Wakina mama katika Kongamano la Tatu la Wanawake wa Muungano wa Makani ya Pentekoste Tanzania (UW-MMPT), lililoanza Katika Kanisa hilo Sinza Afrika Sana Dar es Salaam jana. Askofu Sinde pia alivitambulisha vitabu vyake viwili alivyoviandika.

April 30, 2017

RAIS DKT MAGUFULI AHUDHURIA IBADA YA JUMAPILI MAKANISA MAWILI TOFAUTI MJINI MOSHI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitakiana amani na mmoja wa mapadre katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi Mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Ekaristi Takatifu toka kwa Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiungana na waumini  katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Waumini wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na watawa katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya  ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya  ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
 Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na waumini wengine wakimsikiliza Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na waumini na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na waumini na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiombewa sala maalumu na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea na wananchi baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Said Meck Sadick wakati wa kuhitimisha ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongozana na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo, Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Muhagama, Askofu Mstaafu Evarist Kweka wakipata picha ya pamoja  baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu Mstaafu Evarist Kweka baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu Mstaafu Evarist Kweka na kiongozi mwingine baada ya  ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo  Aprili 30, 2017. PICHA NA IKULU