Tangazo

June 13, 2013

Maonyesho ya Kilimo cha Mseto na Shamba Darasa katika wilayani Gairo

Katibu Tawala wilaya ya Gairo mkoa wa Morogoro, Victor Nditha akipata ufafanuzi wa jambo kutoka wa Mtafiti Kiongozi wa taasisi ya serikali katika mradi wa mifumo ya kilimo endelevu ya mahindi na mikunde mashariki na kusini na kusini mwa Afrika (SIMLESA) nchini,George Iranga (mwenye kofia) akieleza jambo wakati wa maonyesho ya kilimo cha mseto na shamba darasa katika kijiji cha Msingisi wilayani Gairo ambapo mradi huo unaofadhiliwa na nchi ya Australia katika nchi tano za Afrika ikiwemo Ethiopia, Malawi Kenya, Msumbiji na Tanzania ambapo utafiti huo inalenga kuwahamasisha wakulima kulima mazao mchanganyiko ya mahindi na Mikunde yanayostahimili ukame kupitia mbegu bora zilizofanyiwa utafiti na kituo cha Ilonga kwa ajili ya kuongeza uzalishaji katika ngazi ya kaya mkoani Morogoro.

No comments: