Tangazo

September 22, 2014

AIRTEL YAZINDUA DUKA JIPYA MTWARA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda akiwa amezungukwa na wafanyakazi wa Airtel Mtwara na kukata utepe kuzindua duka jipya la kisasa la airtel mkoani Mtwara, hafla ya uzinduzi ulifanyika mwishoni mwa wiki katika mtaa wa maduka mtwara mjini.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Alfred Luanda akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua duka jipya la Airtel liliko mkoani Mtwara mtaa wa maduka mwishoni mwa wiki hii, Airtel tayari imeshazindua maduka 10 kaika mikoa tofauti tofauti kwa lengo la kubosresha huduma.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx


MTWARA


KATIBU Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda, ameipongeza kampuni ya simu za mikononi ya Airtel kwa kuboresha mazingira ya maduka yao kuwa ya kisasa na kiusalama zaidi kwa watumiaji wa huduma zao mbalimbali hususani ya Airtel Money.

Akizungumza  mwishoni mwa wiki katika uzinduzi wa duka hilo ambalo liko katika mtaa wa Maduka Makubwa mjini hapa,  Luanda, alisema kuwa kufunguliwa kwa duka hilo litawahakikishia wateja wao kwa usalama zaidi wanapofanya miamala ya fedha kupitia counter maalumi zilizowekwa kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa wateja na mali zao kwa ujumla na pia kutaleta huduma karibu kwa wateja wao kwa wakati muhafaka na .

“Tunaposema maendeleo ni matokeo lakini vichocheo hivyo vinaletwa na vitu vingi sana na leo hii tunaona ni namna gani munavyowasaidia wateja wanu…kwa mfano zamani mtu alikuwa anatoka Mtwara kwenda Kilombero huku amebebelea hela kwenye mfuko anafika njiani unakuta gari inavamiwa na majambazi na anapolwa fedha zake zote… lakini sasa hivi mtu anaweza kuwekaa tu kwenye simu anafika huko ananunua tu mpunga wake na kurudi bila kupata tatizo lolote sijui wapole mpunga lakini hii yote inatokana kwa ajili ya mabadiliko makubwa katika mitandao yetu,” alisema na Luanda na kuongeza:

“Airtel mko katika ngazi ya juu kuhakikisha kwamba mabadiliko haya yanakuwa kweli na sisi wateja wenu yatatufanya Tuwaamini sana…mimi ninachoomba sana  muitangaze sana Airtel kwa wananchi ili wajiunge na huduma yenu na wasipoelewa munawaelimisha ndio biashara na pia mpanue huduma zenu muende sehemu nyingi za vijijini kwa sababu jinsi mnavyokuwa wengi wananchi wanapata huduma kwa karibu na kwa haraka zaidi,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Huduma kwa Wateja wa Airtel Tanzania, Adriana Lyamba, alisema kuwa kufunguliwa kwa duka hilo kwa mkoani hapa litaendelea kutoa huduma mbalimbali  kwa wateja wa Airatel na wanaweza wakazipata mahari hapo kwa watu wa mikoa ya Lindi na Mtwara.

“Kama mnavyojua hivi sasa kila siku teknolojia inazidi kupanuka na imekuwa ikibadilika na la msingi tunawasisitizia wateja wetu kuendelea kutumia mtandao wetu wa Airtel kwani mpaka sasa tuna mikakati wa kuzindua maduka yetu zaidi ya kumi na moja kwa ajili ya kuwawezesha wateja wetu kupata huduma zetu mbalimbali kwa haraka na wakati muhafaka.

No comments: