Tangazo

September 30, 2014

ZIARA YA KINANA BUMBULI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wananchi wa kata ya Mbuzii (hawapo pichani).Katibu Mkuu leo alianza ziara yake katika kata ya Mbuzii ambapo alishiriki ujenzi wa ofisi ya chama sehemu ambayo inahistoria kwani ilitumika kwa kufanya mikutano ya harakati za kutafuta Uhuru na ni sehemu iliyojengwa ofisi ya kwanza ya Tanu wilaya ya Lushoto.
 Wananchi wa kata ya Mbuzi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi pamoja na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba wa ofisi ya CCM kata ya Mbuzii ,Mbuzii ndio chimbuko la TANU wilaya ya Lushoto.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiendesha bodaboda baada ya Katibu Mkuu wa CCM kumaliza kufungua shina la madereva bodaboda shina la Dule B ambapo mbunge wa jimbo la Bumbuli Mh.January Makamba alitoa pikipiki moja.
 Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mh. Majid Mganga akiendesha boda boda kuelekea kwenye uzinduzi wa shina la wajasiriamali la Maisha Plus kata ya Dule.
 Baadhi ya mazao yanayolimwa na kikundi cha ujasiriamali Maisha Plus
 Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh.January Makamba akiwasalimu wajasiriamali wa Maisha Plus wakati wa ziara ya Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Wakazi wa kata ya Dule B wakisikiliza kwa makini hotuba za viongozi wao kabla ya kuzinduliwa kwa shina la wajasiriamali la Maisha Plus.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wajasiriamali wa Maisha Plus ambapo alizindua shina la CCM wajasiriamali wa Maisha Plus katika kata ya Dule B
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupasua mawe kwenye kambi ya Maisha Plus ,jimbo la Bumbuli wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kufyatua matofali .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijiandaa kuukata muwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba
 Kazi na Dawa! Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akila muwa
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuelekeza  Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba namna ya kupiga randa .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipandisha bendera ya chama baada ya kuzindua shina la Maisha Plus lililopo Dule B ,jimbo la Bumbuli wilaya ya Lushoto.
 Maisha Plus Bumbuli.
  Katibu Mkuu wa CCM, akiwapungia wananchi mikono alipowasili kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Mponde, Jimbo la Bunburi, ambapo aliwahakikishia wananchi kulitafutia ufumbuzi tatizo la kufungwa kwa kiwanda cha chai cha Mponde wilayani Lushoto,Mkoani Tanga.

 Kinana aliwataka viongozi wote wa CCM na Serikali waliohusika kufungwa kwa kiwanda hicho na kuwasababishia adha wananchi kuwajibika wenyewe au kuwajibishwa.
 Umati wa watu ulivyofurika kwenye eneo la mkutano wa hadhara.
Meza kuu wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye alipokuwa akihutubia wakazi wa Mponde.
Katibu wa Nec Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mponde ambapo aliwaambia kuwa CCM ndio chama pekee kinachoweza kumaliza mgogoro wao wa miaka mingi na sasa ndio wakati umefika wa kulimaliza kabisa.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akijadili jambo na Mbunge wa Bumbuli Mh.January Makamba mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Mponde.
Kila kona ya uwanja watu walijazana kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa kata ya Mponde ambapo aliwaambia suala lao la matatizo katika kiwanda cha chai amelichukua na atarudi kwao baada ya mwezi mmoja akiwa na majibu.
  Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba akihutubia wananchi wa Mponde wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
  Mwenyekiti wa Kamati ya Ufutiaji kuhusu mgogoro wa kufungwa kwa kiwanda hicho muhimu.
 Abdulkarim Jambia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema kata ya Vuga akionyesha juu kadi yake ya CCM baada ya kurejea rasmi CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mponde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijionea namna mashamba ya chai yalivyogeuka vichaka . Katibu Mkuu ameongozana na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba.


No comments: