Tangazo

October 31, 2014

SKYLIGHT BAND INAKUKARIBISHA USIKU WA LEO THAI VILLAGE KWA BURUDANI YA KIPEKEE KABISA!

DSC_0159
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar huku akisindikizwa na waimbaji wenzake kutoka kushoto ni Digna Mbepera, Joniko Flower a.k.a Baba lao, Sony Masamba pamoja na Sam Mapenzi.
DSC_0007
Aneth Kushaba sambamba na Digna Mbepera wakiwapa raha mashabiki wao (hawapo pichani) kwenye show zao za kila Ijumaa ndani ya ukumbi wa maraha wa Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0012
Kifaa kipya cha Skylight Band Bela Kombo akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo ndani ya ukumbi wa Thai Village Ijumaa iliyopita.
DSC_0024
Kutoka kushoto Bela Kombo, Hashim Donode na Digna Mbepera wakiporomosha burudani kwa mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita ndani ya uwanja wao wa nyumbani Thai Village.
DSC_0057
Binti mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni Digna Mbepera kwenye hisia kali za muziki wa Live kwa mashabiki wa Skylight Band ndani ya ukumbi wa Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0026
Burudani ikiendelea.
DSC_0109
Mashabiki wa Skylight Band wakiburudika na muziki safi kabisa wa ladha na vionjo vya kila aina ikiwemo Reggae, Kwaito, Naija Flava, R&B, Zouk na zingine kibao bila kusahau sebene pale kati Joniko Flower anahusika sana sambamba na Sony Masamba njoo ufunge mwezi Oktoba na Skylight Band usiku wa leo.
DSC_0105
Anaitwa Sony Masamba akifanya yake jukwaani huku Sam Mapenzi na Joniko Flower wakipiga back vocal.
DSC_0121
Oya shake body....Oya move body....Make you ring alarm o....Oya shake body....si mwingine ni Sam Mapenzi na Naija Flava njoo leo umshuhudie kwa macho yako...Skylight Band ndio kila kitu huna haja ya kwenda disco unapata kila kitu hapa hapa...!
DSC_0126
Aaaah ni full raha wake kwa waume wakionekana kukunwa na uimbaji wa Sam Mapenzi mzee wa Naija Flava, unakosaje uhondo ndugu....Njoo tujumuike leo pamoja ndani ya Thai Village.
DSC_0132
Umati wa mashabiki wa Skylight Band wakiyarudi mangoma ya ukweli yaliyoenda shule, tukutane pale kati kuanzia saa tatu usiku.
DSC_0137
Mpiga drum wa Skylight Band Baraka akifanya yake kuhakikisha mashabiki wanapata ladha nzuri ya ala hizo za muziki huku pale pembeni Amos Kinanda naye akisababisha.
DSC_0141
Na hivi basi ndivyo wanavyochizika mashabiki wa Skylight Band kwa shangwe za aina yake mwenye kigelegele haya...mwenye mluzi haya....ni furaha si kingine.
DSC_0142
DSC_0163
Mkongwe wa muziki Joniko Flower akiwasebenesha mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar huku waimbaji wenzake wakimpa sapoti.
DSC_0089
Sam Mapenzi;……Kuna Watu Hatari, Wenye Mapenzi Zenye Siri Kali,…Letu Nalo Lina Jua Kali, Penzi Letu Serikali,….Wajua Nakupenda, Malaika…..Aneth Kushaba;…..I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I, Love You, (Aiyayaaaaa)….I'm Going Koo Koo Koo, So Koo Koo Coz I, I Love You,….(Aiyayaaaaa)...Hizi zote utazipata Skylight Band si kwingine bonge la colabo.
DSC_0115
Nyomi la mashabiki wa ukweli wa Skylight Band likiwa limefurika Ijumaa iliyopita ndani ya Thai Village.
DSC_0018
Supermodel Neema Mbuya akionyesha upendo kwa mpiga picha na busu bashasha....Santeeee!
DSC_0045
We are twin sisters......!
DSC_0117
Blogger King Kif (kushoto) akiwa na wadau wa Skylight Band ndani ya ukumbi wa Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0096
Meneja Maneno na King Kif wakimezea mate kuku choma ndani ya kiota cha Thai Village Masaki.

No comments: