Tangazo

December 24, 2014

Wateja wa Airtel Money kutuma pesa bure kwa msimu huu wa siku kuu



·  Wateja kutuma pesa bila kikomo kwenda Airtel bure bila makato yoyote.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa mara nyingi tena imewazawadia wateja wake wakatia wa msimu huu wa sikukuu na  OFA maalum itakayowawezesha  kutuma pesa bila kikomo BURE kupitia Huduma ya Airtel Money. 


Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Mawasiliano Bi Beatrice Singano Mallya alisema” Tumeona ni vyema kuwazawadia wateja wetu nchin nzima na kuwawezesha  kutuma pesa BURE wakati wa msimu huu wa sikukuu kwani tunatambua wateja wetu na watanzania wanafanya miamala ya pesa kwa wingi wakati wa kipindi hiki cha msimu wa Sikukuu za Xmass na Mwaka mpya na kusherehekea nao. kuanzia sasa wateja wetu wataweza kutuma pesa kwa ndugu jamaa na familia popote nchini Airtel –Airtel BURE kabisa. 

Hii ni nafasi pekee kwa wateja wetu na tunaamini kabisa kwamba ofa hii itawapatia wateja wetu thamani ya pesa zao na kuwawezesha kupata pesa ya akiba kwa matumizi mengine katika msimu huu wa sikukuu”

Pamoja na ofa hii pia ya Airtel Money pia tumeweza pia kuwazawadia wateja wetu Katika msimu huu wa sikukuu na Ofa kabambe ya simu za kisasa kwaajili ya wapendwa wao zinazopatikana katika maduka yetu zikiambatana na vifurushi , Ofa kabambe nchini . na uzinduzi wa Ofa hii ya Airtel Money leo ni mwendelezo wa shamrashamra za kusherehekia msimu wa sikukuu na wateja wetu.

“Sambamba  na hilo huduma yetu ya Airtel Timiza bado inaendelea, wateja wanaweza kukopa pesa na kukidhi mahitaji .Mikopo hii ni salama, haina akiba na ina riba nafuu na inapatikana katika kiganja chako cha mkono kupitia simu yako ya  mkononi. Hivyo tumewawezesha wateja wetu si kutuma pesa bure tu bali kupata pesa wakati wowote wanapohitaji.

ili kufurahia ofa hii ya Airtel Money mteja anatakiwa kupiga *150*60# na moja kwa moja utakuwa umeunganishwa na orodha ya huduma za Airtel Money na utume pesa sehemu yoyote  BURE”. Ofa hii itadumu kwa muda wa mwenzi mmoja.

No comments: