Tangazo

February 27, 2015

WASHINDI WA DROO YA TATU YA ‘AIRTEL YATOSHA ZAIDI’ WAKABIDHIWA MAGARI YAO AINA YA TOYOTA IST


Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange (kulia), akikabidhi funguo za gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 782 DCZ, kwa mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Donald Fred Baruti katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa mshindi huyo, Mtaa wa Ngala, eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia (katikati) ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando.

Mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Donald Fred Baruti akilijaribu gari lake jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 782 DCZ, baada ya kukabidhiwa na Airtel, katika hafla iliyofanyika nyumbani kwake, Mtaa wa Ngala, eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam jana.

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (kushoto), akikabidhi kadi ya umiliki wa gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 782 DCZ, kwa mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Donald Fred Baruti katika hafla iliyofanyika, Mtaa wa Ngala, eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia (wa pili kushoto) ni Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange.

Mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Donald Fred Baruti akiteremka kutoka kwenye gari lake jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 782 DCZ, baada ya kukabidhiwa na Airtel, katika hafla iliyofanyika nyumbani kwake, Mtaa wa Ngala, eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es Salaam jana.

Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange (kushoto), akikabidhi funguo za gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 464 DDD, kwa mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, ambaye ni Wakala wa Mtandao huo, John Fred Kiwale katika hafla iliyofanyika, Mtaa wa Togo, eneo la Kinondoni jijini Dar es Salaam jana. Wa (pili kushoto) ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando na (kulia) ni Mke wa mshindi huyo, Anna Kiwale na mtoto wake, Sylvia John.

Meneja Masoko wa Airtel, Upendo Nkini (katikati) akikabidhi funguo za gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 465 DDD, kwa mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, ambaye ni Kondakta wa Malori, Jastini William Dodoo katika hafla iliyofanyika katika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde.

Mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Jastini William Dodoo akiwa mwenye furaha ndani ya gari lake jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 465 DDD, baada ya kukabidhiwa na Meneja Masoko wa Airtel, Upendo Nkini (kushoto), katika hafla iliyofanyika katika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde (katikati), akifafanua jambo kwa mmoja wa washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Jastini William Dodoo (kulia), baada ya kumkabidhi gari lake jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 465 DDD, katika hafla iliyofanyika katika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

No comments: