Mkazi wa wilaya ya sengerma na mvuvi katika kisiwa
cha Yozu bwana Kijiji Gweso Jana amekabithiwa gari aina ya Toyota IST na
kampuni ya simu za mkononi ya Airtel mara baada ya kuibuka mshindi wa
promosheni ya Airtel yatosha zaidi.
Akiongea wakati wa halfa ya kukabithiwa gari lake Bwana kijiji Gweso alisema”
nilipopigiwa simu na Airtel nilipuuzia sikuamini kabisa kama nimeshinda gari
mpaka ndugu zangu waliponipigia na kunihakikishia kuwa mimi nimetangazwa
mshindi ndipo nilipoenda ofisi za Airtel na kukuta kweli nimejishindia. Mimi ni
mvuvi na mke na watoto wawili na nilinunua kifurushi cha Airtel yatosha cha mia
tano tu na furahi sana kushinda gari hili kupitia promosheni hii”
“Sijawahi kumiliki gari hivyo usafiri huu utanisaidia katika shughuli zangu za
uvuvi, za kifamilia na kiuchumi kwa ujumla, nachukua fulsa hii kuwaambia
watanzania wenzangu waamini kuwa Airtel inatoa magari na kwamba wao pia
wanaweza kuwaibuka washindi. Nawashukuru sana Airtel
kwa kuboresha maisha yangu na yawatanzania wengine walioshinda kama mimi”aliongeza
Gweso.
Akiongea wakati wa kukabithi gari kaimu katibu wa wilaya ya sengerema bwana
Aaron L Laizer alisema” nampongeza sana bwana Kijiji Gweso kwa kuibuka mshindi,
ushindi huu umetuthihirishia wakazi wa sengerema kuwa promosheni hii ya ya
ukweli na zawadi zinatolewa. Tunawashukuru sana Airtel kwa kutoa huduma
bora za mawasiliano nchini ambazo zimerahisisha shughuli za kiuchumi, kijamii
na kiusalama lakini pia kuanzisha promosheni inayowazawadia wateja wake, na kwa
wananchi wa sengerema na wa mwanza kwa jumla hii nifulsa kwetu tuendelee
kutumia huduma za Airtel na kupata nafasi ya kushinda”
Kwa upande wake Kaimu Meneja wa kanda ya Airtel Bwana David Wankuru alisema “
promosheni hii bado inaendelea mpaka sasa ni washindi 24 tumeshapatikana ,
magari bado yapo hivyo natoa wito kwa wakazi wa kanda yangu na watanzania kwa
ujumla kuweza kushiriki. Tunafurahi kuwa na washindi wane mpaka sasa kutoka
katika kanda ya ziwa washindi hawa ni pamoja na Bi Ester Mathias Mashauri muuguzi bugando, Bi Kajala kokutima said
mkulima na mkazi wa bukoba, Seleman Daudi Onesmo mkazi wa nyakato Mwanza na leo
tunamkabithi gari bwana Kijiji Gweso mkazi wa Sengerema’.
Wankuru aliongeza kwa kusema “kujishindia unatakiwa kujinga na kifurushi
chochote cha Airtel yatosha cha siku, wiki au mwenzi kwa kupiga *149*99# au
kununua vocha ya Airtel yatosha au kwa kununua kupiita huduma ya Airtel
Money, baada ya kununua kifurushi chako namba yako moja kwa moja itaingizwa kwenye droo na kupata nafasi ya kujishindia gari
aina ya Toyota IST kila siku”.
Promosheni ya Airtel yatosha Zaidi ilizinduliwa na
kampuni simu za mkononi ya Airtel Mwanzoni mwa mwenzi wa Februari, watanzania
wengi kutoka katika mikoa mbalimbali wameweza kujishindia magari na kubadili maisha
ya kupitia promosheni hii. Magari 24 yameshapata washindi toka promosheni hii
ianze hadi sasa.
No comments:
Post a Comment