Tangazo

May 31, 2015

Ujumbe wa Maofisa wa Umoja wa Benki za Akiba Duniani Kanda ya Afrika watembelea Zanzibar

Meneja wa Tawi la Benki ya Posta Zanzibar Ndg Justin S.Nandonde akisalimiana na kumkaribisha wageni wake walipotembelea Tawi hilo Zanzibar kujionea utendaji wa Benki ya Posta Tawi la Zanzibar wakiwa katika ziara yao Zenj.
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg. Sabasaba Moshingi, akitowa maelezo ya Ujumbe wa Maofisa wa Benki wa Umija wa Mabenki Duniani Kanda ya Afrika, walipotembelea Benki ya Posta tawi la Zanzibar.
Wajumbe wa Mkutano wa Wanachama wa Umoja wa Mabenki Duniani na Kanda ya Afrika wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania wakati walipofika Tawi la Benki ya Posta Zanzibar,
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg. Sabasaba Moshingi, akitowa maelezo ya Ujumbe wa Maofisa wa Benki wa Umija wa Mabenki Duniani Kanda ya Afrika, walipotembelea Benki ya Posta tawi la Zanzibar
Mkurugenzi wa Tekohama na Uendeshaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg Jema Msuya akitowa maelezo ya kiufundi kwa ujumbe huo.walipotembelea Benki ya Posta Tawi la Zanzibar Mchangani  
Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Zanzibar Ndg. Justin SNdandonde akitowa maelezo kwa ujumbe huo ulipotembelea Tawi hilo na kuagalia ufanisi wa huduma za Benki hiyo kwa wateja wao



Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg Sabasaba Moshingi akiwa na wakeni wake wakitoka katika moja ya sehemu ya historia ya Kanisa la Mkunazi Zanzibar.  
Mtembeza Watalii katika Mji Mkongwe seif Ali akitowa maelezo kwa Ujumbe huwa sehemu za historia za Mji Mkongwe wa Zanzibar. 
Maofisa wa Umoja wa Benki za Akiba Duniani Kanda ya Afrika wakiwa katika ziara yao katika mji mkongwe na kupata kuonja Ubuyu wa Kwaissa sokomuhugo Zenj wakiwa katika ziara ya siku mbili Zanzibar baada ya kumaliza Mkutano wao Dar.
Mtembeza Watalii Zenj akitowa maelezo kwa Ujumbe huo wa Maofisa wa Mabenki ya Akiba wakiwa katika ziara yao kutembelea sehemu za historia za mji Mkongwe Zanzibar wakipata maelezo ya Mlango wa Zanzibar 

WAZIRI NYALANDU KUCHUKUA FOMU ZA URAIS JUNI 7 MJINI DODOMA

Waziri wa mali asili  na utalii Lazaro Nyarandu na waumini mbalimbali baada ya Ibada ya jumapili Jijini Arusha katika Kanisa la KKKT  Diyoyosis ya Mjini Kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi .
Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu akibadilishana mawazo na Kada wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA  James Olemilia baada ya ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Diyosisi ya mjini kati Arusha ambapo Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutaja rasmi kuwa tarehe 6 mwezi ujao atachukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kuwania urais .

Mpiga picha  wa Chanell ten Arusha Aristrides Dotto na Elia Mbonea mwandishi wa gazeti la Mtanzania wakifanya mahojiano na  Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu mara baada ya ibada ya jumapili  katika Kanisa la KKKT  Diyoyosis ya Mjini kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi.
 **************
WAZIRI wa Mali Asili na Utalii, Lazoro Nyalandu ambaye alishatangaza nia ya kukiomba chama Chake cha Mapinduzi (CCM) kumteua kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, anataraji kuchukua fomu ya kutimiza adhma yake hiyo Juni 7 mwaka huu mjini Dodoma.

ametangaza rasmi kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo baada ya kutangaza nia yake miezi saba iliyopita mkoani Singida.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana, Nyalandu ambaye ni Mbunge wa Singida Magharibi, baada ya kushiriki ibada ya jumapili  katika kanisa la KKKT Usharika wa mjini Kati Arusha.

Nyalandu anaungana na makada wengine wa CCM kuingia katika kinyang’anyiro hicho ambapo anasema mpango na dhamira yake ya kuwania kuteuliwa na chama chake uko palepale huku akijinasibu kuwa dunia itaandika historia pale atakapo ibuka kidedea kwa kupeperusha bendera ya ccm katika kinyang’anyiro hicho.

 “Mpango na dhamira yangu ya kuomba ridhaa ya Chama change kuniteua kugombea urais mwaka huu upo palepale na dunia itaandika historia pale nitakapo ibuka kidedea na kuipeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa mwaka huu,” alisema Nyalandu.

Waziri Nyalandu atakungana na makada na Mawaziri wakongwe katika siasa za Tanzania katika kuwania nafasi hiyo ndani ya CCM kama akina Edward Lowassa, Steven Wasira, Bernard Membe, Samuel Sitta, na wengineo wengi ambao tayari wameshatangaza nia na dhamira yao ya kuutaka urais.

VIJANA WA KAWE WASHIRIKI JOGGING

  • Jogging zawaweka wananchi wa Kawe pamoja
  • Watumia mazoezi kama njia ya kupinga matumizi ya madawa ya kulevya
  • Kuhamasisha vijana wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura
  • Makundi zaidi ya 20 yashiriki.
 Vijana wa Kawe wakishiriki Jogging.
 Gabriel Munasa (mwenye kaptura ya pink) akishiriki jogging pamoja na vijana wa Kawe,kushoto kwake ni Elias Nawera.





 Bendera ya Taifa ikiwa juu kuashiria kuhitimisha kwa mchakamchaka huo ambao mgeni rasmi alikuwa Gabriel Munasa.
 Gabriel Munasa akishiriki mazoezi ya viungo kwenye viwanja vya michezo vya Kawe.



 Gabriel Munasa akiongea na vyombo vya habari ambapo alielezea lengo na madhumuni ya kuwasaidia vijana kupitia vikundi vya jogging na pia alitumia fursa hiyo kuwaeleza nia yake ya kugombea ubunge kwa jimbo la Kawe na kama litagawanywa atagombea jimbo la Bunju.


Burudani baada ya mazoezi.

HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WAKUTANGAZA NIA YA KUWANIA URAIS

Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa ahutubia wananchi kwenye Mkutano wa hadhara, wakati akitangaza nia yake ya kuwania Urais wa Awamu wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM.

JAMBO LEO YAICHABANGA BODABODA FC TAMASHA LA BODABODA UKONGA

 Wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakifanya mazoezi ya kupasha mwili muda mfupi kabla ya kuvaana na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Katika mechi hiyo, Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
 Kikosi cha timu ya Gazeti la Jambo Leo kilichopambana na Bodaboda FC
 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (wa pili kulia), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam jana.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.

 Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Bodaboda FC , muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam
 Silaa akitoa mawaidha kwa timu hizo kabla ya mechi kuanza


 Mchezaji wa timu ya Jambo Leo,  Frank Balile (kushoto) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya Bodaboda, Sharif Mohamed
 Mlinda mlango Maganga Benjamin wa timu ya Bodaboda Wilaya ya Ilala, akiudaka mpira katikati ya wachezaji wa timu ya Jambo Leo 'Wagumu Stars' Zahoro Mlanzi (kushoto) na Ali Salum wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa. Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
 Moja ya kizazaa langoni mwa Bodaboda FC iliyosababishwa na washambuliaji wa Jambo Leo
 Mshambuliaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, Ali Salum (katikati) akifunga bao la kwanza dhidi ya Bodaboda FC,wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
Slaa akiwasalimia wachezaji wa timu hizo mbili

LOWASSA AFUNIKA JIJINI RUSHA

 Mtangaza nia ya kuwania Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono maelfu ya wananchi waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo, wakati wa kutangaza nia yake hiyo ya kuwania Urais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mtangaza nia ya kuwania Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkono maelfu ya wananchi waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo, wakati wa kutangaza nia yake hiyo ya kuwania Urais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Mh. Kangi Lugola akisalima umati wa watanzania uliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo, kumsikiliza  Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa (kulia).
 Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Ndg. Onesmo Ole Nangole akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa, kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo.
 Mh. Lowassa akiwapungia wananchi.
 Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akihutubia katika mkutano wa hadhawa wa kutangaza nia yake hiyo,  kwenye Uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid,jijini Arusha jioni ya leo.
Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na Mkewe Mama Regina Lowassa wakati wa mkutano uliofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.
Mh. Edward Lowassa akipongezwa na baadhi ya Wabunge waliohudhulia mkutano huo, baada hotuba yake.