Tangazo

June 7, 2015

KOMREDI KINANA, NAPE WAHANI MSIBA WA JAJI MSITAAFU LWANGISA BUKOBA MJINI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya marehemu Jaji mstaafu Julius Lwangisa alipokwenda kuhani msiba nyumbani kwa marehemu Kitendagulo, mjini Bukoba leo. Kinana ambaye ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye wanaanza rasmi ziara mkoani Kagera, ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 Komredi Kinana akitoa heshima kwenye kaburi la marehemu Jaji msitaafu Samuel Lwangisa
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akitia saini kwenye kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Jaji msitaafu Samuel Lwangisa, nyumbani kwa marehemu Kitendagulo, Bukoba mjini leo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments: