Tangazo

September 16, 2015

Uzinduzi wa Kampeni za CCM Uwanja wa Gombani ya Kale ChakeChake Pemba Dk Shein

Rais wa Baraza na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwasili katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Pemba kwa ajili ya Uzinduzi wa Kampeni ya Urais Kisiwani Pemba, ufunguzi huo umefanyika leo jioni. 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia CCM akiwa na Viongozi wa CCM baada ya kuwasili katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Pemba kwa ajili ya Uzinduzi wa Kugombea Urais wa Zanzibar.
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wakiwa wamesimama baada ya kumpokea Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi,na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, alipowasili katika viwanja hivyo kwa ajili ya uzinduzi wa Kampeni ya Urais kisiwani Pemba.  
Wasanii wa Kikundi cha Macho Mane Art Group wakitowa burudani wakati wa Uzinduzi wa Kampeni za CCM katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Pemba.
Wasanii wa Yamoto Band wakitowa burudani kwa Wana CCM kisiwani Pemba wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya CCM ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Pemba.
WanaChama wa Chama cha Mapinduzi Kisiwani Pemba wakiwa katika viwanja vya gombani ya kale wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Dk Shein, akifungua Kampeni za CCM Pemba.


Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar pia ni Mgombea wa Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai baada ya kuwasili katikac viwanja vya gombani ya kale kwa uzinduzi wa kampeni ya Urais kupitia CCM kisiwani Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Jukwaa kuu wakifuatilia burudani wakati wa uzinduzi wa Kampeni za CCM Kisiwani Pemba zilizofanyika katika viwanja vya gombani ya Kale Chakechake Pemba. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai akitowa maelezo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni za CCM za Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Pemba.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Unguja Ndg Borafia Silima akizungumza na Wananchi wa Kisiwani Pemba wakati wa Uzinduzi wa Kapeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM zilizofanyika katika viwanja vya Gombani Pemba.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakimshangilia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Unguja Ndg Borafia Silima akiwahutubia katika viwanja vya Gombani Pemba leo jioni.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Unguja Ndg Borafia Silima akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimuombea Kura kwa Wananchi wa Pemba.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mhe Mohammed Aboud akiwahutubia WanaCCM kisiwani Pemba wakati wa kampeni ya Uzinduzi wa Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, na kuwataka kumpigia kura ya Ndio Dk Shein.
WanaChama wa CCM Pemba wakifuatilia uzinduzi wa mkutano huo kwa kusikiliza Sera za Chama cha Mapinduzi wakati wa Mkutano wa Kampeni zilizofanyika katika viwanja vya Gombani Pemba.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakishangilia kwa kuonesha picha za Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein. 
Mama Fatma Karume akiwa katika viwanja vya Gombani Pemba akifuatilia Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Shein katika viwanja vya gombani Pemba.
Mjumbe wa Halmashauru Kuu ya CCM Balozi Ali Karume akizungumza na Wananchi na WanaCCM kisiwani Pemba wakati wa mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM na kuwataka Wananchi kumpigia kura ya Ndio Dk Shein.
Balozi Karume akisisitiza jambo wakati akiwahutubia Wanachama wa CCM Kisiwani Pemba leo jioni.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwahutubia Wananchi na Wana CCM Kisiwani Pemba wakati wa mkutano wa Uzinduzi wa  Kampeni ya kugomgea Urais wa Zanzibar zilizofanyika katika viwanja vya gombani ya Kale Chakechake Pemba na kuwaombea Kura Mhe Magofuli na Dk Shein.
Viongozi wa CCM Jukwaa kuu wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya kugombea Tena Dk Shein, Urais wa Zanzibar kupitia CCM zilizofanyika katika viwanja vya Gombani ya Kale Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akiwahutubia Wananchi Kisiwani Pemba wakati wa mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni zilizofanyika katika viwanja vya Gombani ya Kale Chakechake Kisiwani Pemba. na kuwataka Wananchi kisiwani Pemba kikipigia Kura Chama cha Mapinduzi kwa maendeleo kwa Wananchi wake kupitia Sera za CCM na kutimiza ahadi za Ilani ya Uchaguzi.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wananchi na kuwaonesha Ilani ya CCM wakati wa mkutano huo.
Hivi  ndivyo ilivyokuwa katika uwanja wa gombani ya Kale Chakechake Pemba jinsi Wana CCM walivyojitokeza kumsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein.
Wananchi wakiwa juu ya bodi ya gari wakitaka kumuona na kumsikia Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia katika viwanja vya gombani chakechake Pemba.
Hivi ndivyo ilivyokuwa wananchi kisiwani Pemba walivyofuatilia hutuba ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein.
Twasira katika viwanja vya Gombani ya Kale Uzinduzi wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein.
Mwanachama CCM akishangilia akiwa na kipeperushi cha Mgombea wa Urais wa  CCM. Dk Ali Mohamed Shein.

Wasanii wa Kikundi cha Machomane Art Group wakimshangilia Mgombea wa Urais wa CCM Dk Ali Mohamed Shein, wakati akiwahutubia katika viwanja vya Gombani ya Kale.
Wasanii wa Yamoto Band wakitowa Burudani kwa Wananchi wa Kisiwani Pemba wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Urais kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein. 



No comments: