Tangazo

November 30, 2015

Vijana wa Iringa wawezeshwa na Airtel FURSA

Mshiriki  wa  mafunzo  ya Airtel Fursa mkoani Iringa Bi Fatuma Mkini (kushoto )  akipokea cheti cha  ushiriki  wa mafonzo hayo  kutoka kwa afisa mahusiano na  matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki mara  baada ya  mafunzo ya Airtel  Fursa kumalizika mkoani Iringa kwa vijana  zaidi ya 200 kushiriki (picha  na mpigapicha wetu )
Afisa Uhusiano na Matukio  wa Airtel, Bi. Dangio Kaniki (kulia)  akitoa mada kwa Vijana  washiriki  wa mafunzo ya siku moja ya Airtel Fursa  mkoani Iringa.  

Wawakilishi  wa vijana  zaidi ya 200 mkoani Iringa walioshiriki  kupata mafunzo ya ujasiriamali kupitia mradi wa Airtel  fursa wakiwa  katika  picha ya pamoja na Afisa Uhusiano  na Matukio  wa Airtel, Bi Dangio Kaniki na  wafanyakazi wengine wa Airtel wa mkoa huo.

Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Baada ya kukata tamaa ya maisha kwa muda mrefu baadhi ya vijana mkoani Iringa wameeleza kufurahishwa na kampuni ya simu ya Airtel Tanzania kwa kuwapatia mafunzo ya jinsi ya kuanzisha na kuendesha biashara zao kwa faida kupitia mpango wa Airtel FURSA

Wakizungumza na mara baada ya mafunzo ya siku moja ya Airtel FURSA yaliyofanyika katika ukumbi wa Highlands mjini Iringa kwa kuwashirikisha vijana zaidi ya 200,washiriki hao walisema kuwa mafunzo hayo ni ukomb0zi mkubwa kwao kwani baadhi yao walikuwa wakilazimika kushinda vijiweni kutokana na kukosa fursa ya mafunzo kama hayo .

Washiriki wa mafunzo hayo Bi Husna Sanga na Bw Okelo Kasim wakizungumza kwa niaba ya wenzao walisema kuwa mbali ya kuwa wa hatua ya kampuni hiyo ya simu ya Airtel kutoa mafunzo hayo si tu kunawasaidia kupata elimu kuendesha biashara na miradi mingine ya kiuchumi bali ni sehemu ya ukombozi kwao na familia zinazowazunguka .

Alisema Bi Sanga kuwa sehemu kubwa ya vijana hasa mabinti walikuwa wakirubunika na kujiingiza katika biashara zisizofaa kama za uuzaji wa miili yao kutokana na kutokuwa na elimu ya uanzishaji wa biashara ndogo ndogo ambao zingewakomboa kiuchumi hivyo kupitia mpango huo wa Airtel FURSA ni wazi kilio chao kimepata majibu.

"Wapo baadhi ya mabinti wenzetu ambao wanalazimika kufanya biashara ya kuuza miili yao ili kupata kipato na mwisho wa siku wanapoteza maisha kwa ugonjwa wa UKIMWI , ila kwa sisi ambao tumepata elimu hii kupitia Airtel FURSA tunaweza kuwa mfano kwa wengine ambao wanafikiri kazi ni kuuza miili yao pekee"

Huku Bw Kasim mbali ya kupongeza kampuni ya simu ya Airtel Tanzani kwa kuwakumbuka vijana bado alisema kuwa kama njia ya wao kupongeza kampuni hiyo ya simu kwa vijana wote waliopata mafunzo hayo kwenda kuonyesha mfano kwa wenzao kwa kufanya kazi ya kubuni miradi na kuendesha shughuli zao kifanisi zaidi.

Kwa upande wake afisa mahusiano na matukio wa Airtel Bi Dangio Kaniki kuwa Kutokana na mradi huo wa Airtel  FURSA   vijana wengi watanufaika zaidi na wanafaidika na mradi huo ni wale wenye miaka kati ya 18-24

Alisema kuwa mradi huo umelenga kuwafikia vijana kote nchini na hadi sasa zaidi ya mikoa tisa wamefikiwa na mradi huo wa Airtel FURSA  .

Bi Kaniki alitaja mikoa ambayo tayari imefikiwa na mradi huo Mbeya, Arusha, Dodoma, Mtwara, Mwanza, Mtwara, Dar es Salaam , morogoro, Tanga, Tabora na Iringa kuwa hadi sasa zaidi ya vijana 1700 wamefikiwa.

Alisema kuna njia mbili za kuwawezesha vijana njia ya kwanza kupatiwa Mafunzo ya ujasiriamali na njia ya pili kupatiwa vitendea Kazi .

Hivyo aliwataka vijana wote nchini ambao watasikia taarifa ya kuwepo kwa Airtel Fursa katika Mkoa wao basi kuweza kuchangamkia Fursa hiyo ambao hutolewa bure.

Alisema ili kijana aweze kufaidika au kushiriki kwenye Airtel  FURSA   atatakiwa kutuma ujumbe mfupi kwenda kwa namba 15626 na kuweka maelezo yafuatayo:- Jina, Umri, aina ya biashara na eneo. Pia wanaweza kutuma maombi yao kwa kupitia barua pepe airtelfursa@tz.airtel.com ambapo watatakiwa kutuma jina kamili, umri, na aina ya biashara.

Maelezo kuhusu program ya Airtel FURSA pia yanapatikana kwenye tovuti ya Airtelwww.airteltanzania.com   

Alisema kuwa Airtel Fursa inawalenga vijana ambao wapo katika biashara na wale ambao hawana shughuli na wanataka kuanzisha shughuli pia kwao ni fursa kwao .

Aidha alisema kuwa tayari baadhi ya vijana wamepata kunufaika na mradi huo ambao umelenga kuwainua vijana na kuongeza kuwa mradi huo ulioanza mwaka huu utakuwa ni mradi endelevu.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Iringa youths empowered by Airtel FURSA

After losing hope in life for a long time youth in Iringa have expressed appreciation to the Airtel for providing youth empowerment entrepreneur training on how to establish and run their businesses profitably through Airtel FURSA program.

Speaking immediately after the one-day workshop of Airtel FURSA which took place at the Highland hall in Iringa which involved more than 200 youth, the participants said that the workshop is a great rescuer for them as this is not the time to stay idle when there are such opportunities, we must engage in different activities that will make us benefit from this program. We thanked Airtel today for showing us another way of changing our lives.

Participants of the training Ms. Husna Sanga and Mr Okelo Kasim talking on behalf of their colleagues said that apart from Airtel to provide training to them,  not only helps them acquire knowledge to run a business and other projects but part of redemption their families around them.

 Ms. Sanga said that most of the young people especially girls were hoodwinked into getting into relationships with men and engage in business discomforting as the sale of their bodies due to lack of knowledge of the establishment of small businesses which will redeem them economically. So through the initiative of Airtel FURSA now they can change their lives.

"There are some other girls who are forced to do business of selling their bodies to earn, by the end of the day they are killed by AIDS, but for us who have received this knowledge through Airtel FURSA we can be an example to others who think the job is to sell their bodies particular”

And Kasim, thanked Airtel for caring for youth in the country and be part of this great initiative. He promised to be an example to others by working hard and run their businesses more efficient.

On her part Airtel Tanzania public relations and events officer Dangio Kaniki commented that through Airtel FURSA more youth between the age of 18-24years old, will benefit. The initiative is a lifetime opportunity to sustainably nurture business ideas, serve communities and reduce unemployment in the country.”

She said that the project aims at providing opportunities for youth who own and run businesses with relevant business skills and support for sustainable growth.

Ms. Kaniki cited regions which have already reached  with Airtel FURSA program so far are  Mbeya, Arusha , Dodoma , Mtwara , Mwanza , Mtwara, Dar es Salaam, Morogoro , Tanga, Tabora,  and Iringa that so far and  more than 1700 young people have been touched.

She said there are two ways to enable youth, first by providing entrepreneurship education training and second by providing tools to bust their businesses.

So she called all the young people in the country hereby urge the youth to take advantage of this opportunity and make the most of it as it is provided for free.

She said that in order for the youth to benefit from or participate in Airtel FURSA will be required to send SMS to 15626 with the following details: - name, age, type of business and location. Alternatively interested youth can submit their applications through FURSA email airtelfursa@tz.airtel.com

Airtel details about the program is available on the Airtel website www.airteltanzania.com
“This programme targets young, energetic and enthusiastic business start-ups that are ready to take up the challenge and grow their businesses.  As Airtel we aim at empowering people’s lives”, added Kaniki.


In addition she said that already some of youth around the country have received grants from the program which aims to lift up their lives, adding that the project was started this year in May and will be an ongoing project.

No comments: