Tangazo

April 5, 2016

HEKTA 5000 ZA ARDHI YA KIJIJI CHA LUHANGA WILAYANI MBARALI ZARUDISHWA KWA WANANCHI KUTOKA WAWEKEZAJI

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makala akizungumza na wananchi wa kijiji cha Luhanga Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya kwa lengo la kutoa tamko la serikali juu ya ulejeshwaji wa ardhi ya wananchi hao hekta 5000 ambazo zilichukuliwa na wawekezaji.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makala akisisitiza jambo katika Mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu huyo wa Mkoa kwa lengo la kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Luhanga (Hawapo Pichani)Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya .
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Luhanga Mbarali Mkoani Mbeya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu huyo wa mkoa kwa lengo la kulejeshewa ardhi yao iliyochukuliwa na wawekezaji .
Mkutano ukiendelea katika kijiji cha Luhanga Mbarali katika ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na Wananchi wa kijiji hicho ambao walikuwa katika mgogoro mkubwa wa ardhi na wawekezaji.
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mbeya Guram Shekifu akimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala mara baada ya kumaliza mgogoro huo.
Wananchi wakifuatilia Mkutano.
Baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbarali Mbeya wakichukua kumbukumbu za Mkutano huo.

SERIKALI Mkoni Mbeya, imezirejesha hekta 5000 za ardhi ya kijiji cha Luhanga Wilayani Mbarali, zilizokuwa zimetolewa kwa wakulima zaidi ya 200 wa chama cha Luhanga (Luhanga AMCOS), huku ikiuagiza uongozi wa halmashauri kuwachukulia hatua watendaji wote walihusika na mchakato wa ugawaji wa ardhi hiyo.

Akikabidhi ardhi hiyo leo, kwa wananchi wa Kata ya Luhanga, Wilayani humo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amosi Makala, alisema serikali imefikia uamuzi huo baada ya kubaini kwamba zoezi hilo lilifanyika kinyume  na sheria na kanuni za ardhi za vijiji zinavyoelekeza.

Amesema, sheria  mama namba 5 ya ardhi ya mwaka 1999, imebainisha kwamba halmashauri ya kijiji haina mamlaka ya kugawa ardhi zaidi ya ekali 20 au 50 lakini wao wamegawa ardhi zaidi ya hekta 5000.

Mkuu huyo ameongeza kuwa mbali na zoezi hilo kughubikwa na ukiukwaji wa sheria lakini pia, wawekezaji hao wameonekana ni wababaishaji  kutokana na kushindwa kutimiza ahadi za maendeleo walizokuwa wamezitoa kwa wananchi wa eneo hilo.

 Aidha, Makala, aliwatahadharisha wananchi hao, kujiepusha na walaghai wa ardhi na kuacha kugawa ardhi ovyo kwani rasilimali hiyo haiongezeki ukilinganisha na mahitaji ya watu, ambao kila siku wanaongezeka idadi.

Amesema serikali inaweza kufanya uparesheni ya kuwataka vijana wafanye kazi lakini kama wananchi au viongozi wanauza ardhi zoezi hilo haliwezi kufanikiwa . 

Amesema mkoa wa mbeya unajulikana kwa kuongoza kwa migogoro ya ardhi hususani wilaya ya mbarali hivyo yeye kama mkuu wa mkoa  atahakikisha anashughulika vyema na suala hilo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka jamii za wafugaji wa kimasai kuhakikisha wanaachana na tabia ya kuozesha watoto wa kike katika umri mdogo badala yake wawalitihishe katika elimu ambayo ndio mkombozi kwao.
XXXXXXX
Habari hii imeandaliwa na mtandao wa kijamii wa www.jamiimoja.blogspot.com-0759406070 Mbeya.

No comments: