Tangazo

July 14, 2016

HALMASHAURI ZA WILAYA KYERWA NA BIHARAMULO ZAANZA UTEKELEZAJI WA MRADI WA UIMARISHAJI MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA

Mwakilishi wa Shirika la Misaada la Kimataifa la Makani (USAID), Moses Busiga akizungumza wakati wa kikao cha kwanza cha maofisa watendaji wa Halmashauri mbili za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo mkoani Kagera kilichofanyika leo ikiwa ni kuanza kwa utekelezaji wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za umma (PS3) Mkoani Kagera. Source:Father Kidevu Blog
 Kiongozi wa timu ya Uzinduzi wa Mradi wa PS3 Mkoani Kagera, Abdul Kitula akizungumza

Washiriki wakisikiliza kwa makini mada
Washiririki walikaa katika makundi na kuainisha wadau mbalimbali wa maendeleo walioko katika halmashauri zao na namna ambavyo wanashirikiana katika kuimarisha mifumo ya sekta za umma.
Wataalam wa masuala ya Utawala nao walishiriki kuhakikisha mambo yanaenda vizuri.
 Afisa Mipango wa Halamashauri ya Wilaya ya Kyerwa, Johansen Karugaba akiwasilisha taarifa ya Wilaya yake.
 Dk Rest Lasway wa mradi wa PS3 akitoa mapendekezo yake.
 Afisa Maenendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Sebastian Kitiku akitoa mapendekezo.
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, Kashunju Runyogote akitoa maoni yake.
  Afisa Mipango wa Halamashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Andambike Kyomo akiwasilisha taarifa ya kundi lake.
 Mmoja wa washiriki akichangia maoni
Mtaalam wa masuala ya Rasilimali watu kutoka Taasisi ya Benjamin Mkapa (BMF), Remmy Moshi akiwasilisha mada.
 Afisa Elimu wa Halamashauri ya Wilaya ya Kyerwa akifafanua jambo.
 Ofisa wa PS3, Desderi Wenger akizungumza wakati wa uwasilishaji wa taarifa za vikundi.
 Mratibu wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Berha Swai akizungumza.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, Kashunju Runyogote akitoa neno la shukrani.

No comments: