Tangazo

November 22, 2016

Airtel yaja na “WADATISHE INTANETI’ Ofa ya msimu wa sikukuu

Meneja Mawasiliano na Nembo wa Airtel,  Arnold Madale (kulia) pamoja na Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando  (wa pili kushoto)na Meneja wa huduma za Intaneti, Erick Daniel  wakionyesha bango la offa mpya ijulikanayo kama “Wadatishe””  itakayowawezesha wateja wa Airtel kupata ofa kambambe  ya  Intaneti pamoja na vifaa nafuu vinayotumia intaneti  kwa gharama nafuu zaidi wakati huu wa msimu wa sikukuu
Xxxxxxxxxx

DAR ES SALAAM
                                                                                Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua Kampeni ya “Wadatishe Intaneti”  yenye OFA kabambe maalum kwa wateja wake nchi nzima ili waweze kufurahia huduma bora za Intaneti pamoja na kujipatia vifaa nafuu vinayotumia intaneti kwa matumizi binafsi au kwa kuwanunulia zawadi ndugu jamaa na marafiki katika msimu huu wa sikukuu

Akiongea wakati wa Uzinduzi Wadatishe Intaneti OFA Meneja wa huduma za Intaneti Bw, Erick Daniel alisema  “Wadaitishe Intaneti” ni ofa ya kipekee kwa kuwa inatoa uhuru kwa kila mteja  kujichagulia kifurushi nafuu kinachoendana na kifaa anachotumia. Vipo vifurushi vya “Wadatishe Intaneti kwa siku, Wiki au Mwezi vya gharama nufaa ya hadi shilingi 500 kwa kupiga *149*99# na kuchagua Yatosha Intaneti. Vilevile mteja ataweza kujichangulia  Wadatishe intaneti OFA  nyingine kabambe kwa kupitia huduma ya Airtel Money kwa kupiga *150*60#  na kuchagua ofa kabambe kisha  Wadatishe Intaneti ambapo kwa shilingi 1000 tu utapata GB 1 ya intaneti na kwa shilingi 2000 tu pia utaweza kupata GB 2.5 papo hapo na kuanza kufurahia intaneti bora ya Airtel”

Kwa kuongezea, Mteja yeyote ukienda na kununua kifaa chochote kinachotumia intanent kama vile simu za smartiphone, Modem za maajabu wingle, au home Wi-FI katika duka lolote la Airtel nchini utafaidi pia ofa ya punguzo bei la hadi shilling 79,000 na utaunganishwa na OFA ya intaneti kwa miezi 6 kuanzia sasa” alisema Erick

Kwa Upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando
alisema “Airtel tunaendelea na  dhamira yetu ya kuhudumia wateja wetu kwa kuwapa kipaumbele kwa kila huduma yetu, hii ndio sababu kubwa inayotufanya tuwape wateja wetu nchini Uhuru mkubwa wa kujichagulia, kuanzia leo kupitia ofa za ‘Wadatishe intaneti’  tunaamini zitatoa unafuu mkubwa kwa  kuwaunganisha  ndugu, rafiki,  na familia kuwasiliana katika msimu huu wa sikukuu”

Ofa zetu mwaka huu zinatoa punguzo kubwa sana kwa vifaa vinavyotumia Intaneti kama vile Home Wi-Fi  sasa utaipata kwa shilingi 79,000 tu badala ya shilingi 200,000 na utapewa Home Wi-Fi yako hiyo ikiwa na kifurushi cha GB 40 BURE. Kwa watakaonunua simu kama Magnus Z11 itaipata kwa shilling 79,000 tu ikiwa na ofa ya GB 12 kwa muda wa miezi 6. Vilevile kwa kupitia ushirika wetu na wadau wetu Techno na Huawei katika maduka yetu simu zao zote zitauzwa kwa bei za punguzo nafuu zaidi ya ilivyozoeleka.  Pia ili kukuongeze furaha kwa ofa tunazotoa kwa watumiaji wa Airtel msimu huu wa sikukuu utafaidi pia ofa mbalimbali za SMS za bure au muda wa maongezi wa ndani na nje ya mtandao” alieleza Nchunda 

Tunawahimiza wateja wetu kutembelea maduka yetu yote ya Airtel nchi nzima ili kujinunulia vifaa origino vya intaneti na kujiunganisha na huduma yetu bora kabisa ya Intaneti  kwa kupiga *149*99# na kuchagua Yatosha Intaneti ili kufurahia Wadatishe Intaneti Ofa” alimalizia kwa Kusema Bw, Mmbando


No comments: