Tangazo

November 30, 2016

Airtel yazindua Huduma za Mawasiliano Lindi Vijijini

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (kushoto), akielezea huduma zitakazotolewa na mnara wa Airtel uliojengwa kijiji cha Cheleweni kwa  Mkuu wa wilaya Lindi,  Shaibu Ndemanga (wa pili kulia), baada ya kuzindua mnara huo. Katikati ni Meneja wa Airtel Lindi, Saleh Safy.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxx
·  Mtandao wa Airtel kutumika kuhimiza elimu ili wazazi kuandikisha watoto Lindi vijijini
LINDI
KATIKA juhudu za kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia maeneo ya pembezoni mwa nchi, kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua mnara wake wa mawalisiliano na kuanzisha hduma za simu kwa mara ya kwanza katika kijiji cha cheleweni mkoa wa Lindi.

Huduma hizi mpya za mawasiliano zitawafikia wakazia wa vijiji vya Ng’apa ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo yanayowazunguka vijiji hivyo kwa kuwahakikishia wakazi wote wa Lindi vijijini huduma za mawasiliano za uhakika, huduma za kifedha kwa njia ya mtandao Airtel Money na hatimae kuendesha shughuli zao za kila siku kiuchumi na kijamii

Akiongea wakati wa uzinduzi, Mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga alisema “ tunayofuraha kupata huduma za mawasilino hapa cheleweni na vijiji vya jirani.  Airtel kwa kuzindua mnara huu, serikali tunaungano jitiada hizi za kuboresha mawasiliano huku vijiji kwa sasa wakazi wa vijiji hivi mtaweza kutumia huduma ya mawasiliano kwa kufany a biashara zenu za nazi kwa kujitafutia masoko sehemu nyingine lakini pia itasaidia kuondoa tatizo lakutembe na fedha nyingi pale mnapofanya biashara kwa kuwa mtatumia huduma za kifedha za Airtel Money kujichukulia fedha zenu wakati wowote


Mkuu wa wilaya aliongeza kwa kusema “Mawasiliano haya yatasaidia sana wilaya yangu katika kukuza elimu kwa kuwa nitaweza kuwawasiliana na watendaji wangu wote wakati wowote. Sasa nitoe tamko kwamba nimeongea na Airtel ili kutuma ujumbe wa meseji kwa wazazi wote kwa kuwa ndio mtandao unaotumika na wengi hapa katika vijiji vyetu vya ng’apa ng’apa  kuhusu kuandikisha watoto wote waliomaliza shule za msingi waende sekondari,  Airtel wamenikubalia sasa ikiwa  mzazi atakaidi kuitikia wito nitamchukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfunga”.

Nataka kuona  huduma hii ya Mtandao wa Airtel tunayoizindua leo inaleta tija katika shughuli za uchumi kama vile uzalishaji wa korosho, kusaidia biashara ndogo za kati na kubadilisha maisha ya jamii kwa ujumla.  Napenda kuchukua fursa hii  kuwahasa wakazi pia kuilinda miundombinu ya mawasiliano haya ili yaduma. Alimalizia kusema Mh,  ……

Kwa upande wake Meneja Mauzo wa Airtel, Saleh Saphy “Tunayofuraha kutoa huduma za uhakika na gharama nafuu nchi nzima, kwa wakazi wa Lindi , tunawahakikishia ofa kabambe za msimu huu wa sikukuu kupitia ofa yetu maalumu ya “Wadatishe” ambayo mnaweza kupata simu orijino kwa gharama nafuu hadi ya shilingi 79,000 tu.-. vilevile wateja wanaweza kupata vifurushi vya intaneti vya 1G kwa shilingi 1000 wakati huu wa msimu wa sikukuu .

Kupitia huduma ya mawasiliano wateja wataunganishwa na huduma za intaneti, huduma za kifedha za Airtel Money kutuma na kupokea pesa, kupiga simu wakati wowote, kusajili simu zao na pia kupata nafasi ya kusoma masomo ya ufundi ya VETA kupitia simu zao. Hizi ni baadhi tu za huduma zetu hivyo natoa wito kwa wakazi wa cheleweni, Ng’apa na Michee kujiunga na timu ya  Airtel SIBANDUKI na kufurahis huduma zetu.” Alisisitiza Saphy. 

No comments: