Tangazo

December 9, 2016

NAMNA YA KUSHEREHEKEA MIAKA 55 YA UHURU WA TANZANIA

Na Jumia Travel Tanzania

Ijumaa hii ya Desemba 9, 2016 Watanzania nchini na duniani kote watakuwa wakiadhimisha miaka 55 ya Uhuru uliopatikana kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza mnamo mwaka 1961 chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Shamrashamra hizi ambazo zimeambatana na msimu wa sikukuu, Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukushauri kwamba unaweza kusherehekea kwa namna tofauti kabisa kwa kutembelea na kujivinjari katika hoteli za mikoa ya Dar es Salaam, Zanzibar na Arusha ambapo zimetoa punguzo la zaidi ya 40%.

Zanzibar

Zanzibar ni visiwa mojawapo vilivyobarikiwa kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii barani Afrika ambavyo vinakupa fursa ya kujifunza na kufurahia mengi endapo utatembelea. Kila sehemu ya visiwa hivi ni sehemu ya utalii kuanzia majengo yake, watu wake na tamaduni zao, vyakula pamoja na hoteli nzuri na fukwe safi za kuvutia zilizopo kila kona.

Sehemu kubwa ya watu na watalii wanafurika katika visiwa hivi hususani kuelekea msimu huu wa sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya. Kinachovutia zaidi ni hoteli nyingi kutoa ofa za kipekee kwa wageni ambao watapenda kutembelea huko kama vile malazi ambapo watu wengi hudai kwamba ni ya ghali sana.

Hoteli nyingi zimeshusha bei za malazi kwa kiasi kikubwa mpaka kufikia zaidi ya 40% kwa mfano kama ukitembelea hoteli za Ras Nungwi Beach Resort, Mazsons Hotel, Paradise Beach Resort (https://travel.jumia.com/en-gb/tanzania/o21502/paradise-beach-resort-uroa), Ras Mishamvi Beach Resort na Karamba Zanzibar.

Arusha

Mji wa Arusha uliopo Kaskazini mwa Tanzania umekuwa ni ndoto ya watu na watalii wengi kutembelea katika maisha na hii ni kutokana na hali nzuri ya hewa pamoja na vivutio kadhaa vya kitalii kama vile Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mlima Meru ambao una asili ya volcano na pia umepakana na njia ya kuelekea ulipo Mlima Kilimanjaro.

Mbali na kuwa na vivutio vya kitalii pia mji huu hupendwa kutumiwa na mashirika pamoja na makampuni mbalimbali nchini na duniani kwa ajili ya vikao mbalimbali kutokana na utulivu ulionao. Kwa mfano Arusha imepewa heshima kubwa ya kuwa na ofisi ya Mahakama ya Umoja wa Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (UN - ICTR).

Kipindi hiki cha kusherehekea miaka 55 ya uhuru ambapo pia ni msimu wa sikukuu unaweza kutembelea na kufurahia vyote hivi huku ukiwa huna wasiwasi wa malazi kutokana na ofa kadha wa kadha zenye punguzo kwa zaidi ya 40% katika hoteli kama vile Ngorongoro Serena Safari Lodge, Arusha Center Inn & Tours, City Link Pentagon Hotel, Lush Garden Hotel (https://travel.jumia.com/en-gb/tanzania/o5079/lush-garden-hotel-arusha) na The Charity Hotel International.  

Dar es Salaam

Mji huu unachukuliwa kama kitovu cha biashara nchini Tanzania kutokana na kuwa na mashirika na makampuni kadhaa ya ndani na nje ya nchi kuwekeza. Wakazi wa Dar es Salaam siku zote wanakuwa wako kwenye pilikapilika za kutafuta riziki ili kuendana na gharama za maisha ambazo kwa kiasi kikubwa ni ghali.

Hali hiyo lakini haizuii kulifanya jiji hili kuwa na sehemu nyingi za kustarehe kwani sio watu wote ambao wanatoka nje ya mkoa huu kipindi hiki cha msimu wa sikukuu.

Kama utabakia jijini Dar likizo hii na hauna mpango wa kusafiri basi ni wakati wako wa kutembelea mtandao wa Jumia Travel na kujionea ofa kamambe za hoteli kama vile; Skippers Haven (https://travel.jumia.com/en-gb/tanzania/o26035/skippers-haven-dar-es-salaam-city-center), Q Bar and Guest House, ShaMool Hotel, Hotel De Mag Deluxe na Ramada Encore ambazo zimetoa punguzo kubwa huku kukiwa na huduma lukuki ndani yake.

Maadhamisho ya miaka 55 ya kusherehekea uhuru ni mingi na inahitaji namna pekee ya kuisherehekea, inawezekana akili na nguvu nyingi za watu zimeelekezwa kwenye sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya lakini siku hii ina umuhimu mkubwa kuienzi.

No comments: