Tangazo

April 25, 2017

Airtel yazindua Duka la kisasa Babati Mkoani Manyara

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Massawe akizungumza  baada ya kuzindua duka la Airtel Mkoani Manyara hivi karibuni, Anayeshuhudia Meneja wa Airtel mkoa wa Manyara Peter Kimaro.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

-  Jumla ya maduka matatu kuzindualia katika maeneo ya Babati mjini Dareda center na Riloda  mkoani humo

Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel imezindua duka mjini Babati kwa ajili ya kutoa huduma kwa wateja wanaoishi katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa Manyara ikiwa ni mwendelezo wa mpango wake wa kufungua maduka ya kutoa huduma kwa wateja wake nchi nzima.

Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara,Fransic Masawe,ndiye aliyezindua duka hilo ambaye amesema litasadiai kutoa huduma kwa wakati lakini pia lisaidia kutoa ajira kwa vijana na kuwawezesha wakulima wa mazao ya  kupata huduma za kifedha kwa urahisi zaidi

 “Nawapongeza Airtel kwa kusogeza huduma karibu na wateja  na kuongeza kuwa duka hilo litakuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa mji wa Babati  pamoja na maeneo jirani. Napenda kuchukua fursa hii kuwa kuwaasa wakazi wa hapa hususani vijana kuchangamkia fursa za ajira zilizopo kupitia duka hilo ajira kwa lengo lakujiongezea kipato”, Alisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Fransic Masawe.

 Kwa Upande wake Meneja wa Airtel mkoa wa Manyara,Peter Kimaro,amesema duka hilo linalenga kusogeza huduma karibu na jamii kwani kipindi cha nyuma wananchi walikuwa wanapata tabu kupata huduma za uhakika lakini pia hatua hiyo inatoa mwanya wakuongeza maduka mengine mengi katika maeneo ya mkoa huo ikiwemo wilaya  ya Katesh

Pia amesema huduma ya mawasiliano ni chachu ya maendeleo kwani inasaidia uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kuwawezesha huduma za kifedha kupatikana kirahisi ambapo kwa sasa watu wengi hutumia Airtel Money kufanya miamala pamoja na kupata mikopo kupitia huduma ya Airtel Timiza ambayo imekuwa ni mkombozi kwa wajasiriamali wadogo wadogo kupata mitaji ya kuendesha biashara zao.

Tunatoa wito kwa wateja wetu kutembelea maduka haya ambayo tunayafungua nchi nzima ili kupata huduma hapa manyara tayari tunayo maduka matatu ambayo moja tunalizindua hapa na mengine mawili yapo katika maeno ya Dareda center na Riloda .aliongeza Kimaro.

Baadhi ya wananchi wamesema kufunguliwa kwa duka hilo kutaongeza ajira kwa vijana pamoja na kutoa huduma za uhakika za miamala ya fedha na mawasiliano kwa ujumla tofauti na kipindi cha nyuma ambapo walikuwa wanalazimika kufuata huduma umbali mrefu kidogo.

Kampuni ya Airtel inampango wakuongeza maduka mengine katika mkoa huo wa Manyara ili kuendelea kusogeza huduma zake kwa wateja kwa urahisi hususani katika maeneo ya vijijini.


No comments: