Tangazo

April 18, 2017

KIPINDI CHA CLOUDS 360 KILIPORISHWA MUBASHARA KUTOKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Gari Maalumu la kurusha matangazo ya moja kwa moja la kituo cha Luninga cha Clouds likiwa katika eneo la Serengeti kwa ajili ya kurusha matangao ya moja kwa moja ya kipindi cha Clouds 360.
Watangazaji wa Kipindi cha Clouds 360 ,Sam Sasali na James Tupatupa wakifungua kipindi katika eneo ambalo ni makazi ya Viboko ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.
Watangazaji wa Clouds 360 ,Sam Sasali na James Tupatupa wakiongea na Meneja Mawasilino wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akizungumza jambo na watangazaji hao wakati wakifanya mahojiano.
Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa akizungumza jambo na Mtangazaji Sam Sasali.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti William Mwakilema akizungumzia sifa za hifadhi hiyo ya pili kwa ukubwa .
Mwekezaji katika Sekta ya Utalii,Wily Chamburo (wa pili toka kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Ibrahim Musa (aliyevaa koti) pamoja na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ,Wiliam Mwakilema (kushoto) na Meneja Mawasiliano wa TANAPA ,Pascal Shelutete.(kulia).
Watangazaji Baby Kabaye na Hassan Noma wakifanya mahojiano na Mwekezaji katika Sekta ya Utalii,Wily Chamburo wakati kipind cha Couds 360 kiliporushwa moja kwa moja kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Watangazaji Baby Kabaye na Hasan Ngoma wakifanya mahojiano na Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa wakati kipindi cha Clouds 360 kiliporushwa moja kwa moja kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mtangazaji wa Sport 360 katika kipindi cha Clouds 360 ,James Tupatupa akifanya mahojiano na Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete wakati akizungumzia Utalii wa kimichezo pamoja na namna TANAPA inavyoshiriki katika kukuza Michezo mbalimbali nchini.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akitoa neno la Shukrani wakati kipindi cha Clouds 360 kilipokuwa kikihitimisha ziara yake katika Hifadhi ya Taifa za Serengeti.
Wadau waliokuwepo katika shughuli nzima ya urushwaji wa kipindi cha Clouds 360 wakifuatilia kwa karibu matukio yaliyokuwa yakiendelea.
Watangazaji wa Kipindi cha Clouds 360 wakiwa katika picha ya pamoja na Wadau mara baada ya kuhitimisha ziara ya urushwaji wa kipindi hicho katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: