Tangazo

June 13, 2017

DC KASESELA: TUTAUFUNGA MGODI WA NYAKAVANGALA HALI IKIENDELEA HIVI

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na blog hii juu ya kitu kinachiendelea kwenye mgodi wa nyakavangala.

Na Fredy Mgunda, Iringa

Wachimbaji wa madini katika mgodi wa nyakavangala wamefukiwa na mchanga kutokana na wachimbaji hao kuingia kinyume cha makubaliano yaliyowekwa baina ya wachimbaji na Mkuu wa Wilaya ya Iringa  Richard Kasesela.

Akizungumza na blog hii Kasesela alisema kuwa Jana mida ya saa 1 jioni Duara la mgodi mmoja ulioko Nyakavangala uliporomoka na kufukia wachimbaji 4 . 

"Inasemekana wachimbaji hao walikuwa wameingia kuiba kwani duara hilo ni kati ya maduara ambayo Mkuu Wa wilaya ya Iringa  Mhe Richard Kasesela aliifungia ili ijengwe nguzo na ngao" alisema Kasesela

Kasesela alisema kuwa Watu 4 waliingia mgodini baada ya mafundi  Wa ujenzi Wa ngao kupumzika kwa vile ni usiku ndipo wachimbaji nao wakaingia mgodini bila ruhusa

"Hadi sasa tumefanikiwa kuokoa 3 mpaka sasa huyo mmoja hajaokolewa bado yupo ndani ya mgodi kutokana na changamoto za uokoaji ili Juhudi zinaendelea za kumuokoa huyo mmoja" alisema Kasesela

Kasesela alisema kuwa changamoto ilikuwa ni namna ya kumuokoa kwani sehemu iliyokuwa imejifukia juu mwamba mwingine ulionekana kuwa na dalili za kushuka.ikawapasa kujengea kwanza eneo hilo kazi iliyochukua mda mrefu na ndipo waaze kuokoa.kwahiyo tunasubiri hatua nyingine sasa.

"Naendelea kuwaonya wachimbaji wasiendelee na uchimbaji eneo la chini maarufu kama kwenye "vein" mpaka wajenge ngao ili wasihatarishe maisha yao. Wakiendelea na kiburi tutaamua tufunge mgodi" alisema Kasesela

No comments: