Tangazo

August 17, 2017

SHAKA:JUKUMU LA KULETA MAENDELEO PEMBA NI LA WOTE

 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akisalimiana na viongozi wa chama mkoa wa kaskazini unguja akiwa katika ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akipokelewa na viongozi ofisi za CCM wilaya ya micheweni  katika ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 vijana wakiburudisha kwa kupiga dufu wakati wa mapokezi ya  Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shakaalipowasili ofisi za CCM wilaya ya micheweni  katika ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka wa pili kulia pamoja na mkuu wa idara ya Uchumi uwezeshwaji na fedha (UVCCM)Dorice Obedi wakisain Vitabu vya wageni walipowasili wasili katika ofisi za CCM Wilaya ya micheweni ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akizungumza jambo pamoja na mwl,Ally khatibu Hassan Mkuu wa shule ya msingi Michekweni wakati akikagua jengo la Ujenzi wa maktaba pamoja na madarasa ya Shule ya Msingi Micheweni. wakati wa ziara ya kikazi  visiwani pemba.
 Wanafunzi wa Darasa la kwanza Issa Haji (wa kwanza kulia) pamoja na Abdulwahid abdallah wakisalimiana na  Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka wakati  alipokwenda kukagua jengo la Ujenzi wa maktaba pamoja na madarasa ya Shule ya Msingi Micheweni.
  Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akimfunga Vifungo vya shati Mwanafunzi wa Darasa la kwanza Shule ya Msingi Micheweni Abdulwahid abdallah wakati  alipokwenda kukagua jengo la Ujenzi wa maktaba pamoja na madarasa ya Shule ya Msingi Micheweni.
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akiwa Shumba mjini akikagua sehemu itakayo jengwa jeti
 Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akigagua ujenzi wa ofisi ya ccm tawi la njuguni inayojengwa na mwakilishi Jimbo
 Afisa mipango wa halmashauri ya konde (pili kushoto)akitolea ufafanuzi juu ya ujenzi wa soko la mboga mboga la samaki pamoja na mbogamboga kwa Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akiwa katika ziara ya kikazi  visiwani pemba.
  Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na Viongozi na wanachama wa CCM na Jumuiya zake Tawi la kuiyu Mbuyuni akiwa katika Ziara ya Kikazi Mkoa wa Kaskazini pemba .
 Wanachama Wa CCM na Jumuiya zake wakishangilia katika mkutano wa ndani uliofanyika Skuli ya Michekweni.Mkoa wa Kaskazini Pemba.
 Ustadh,Abdul mohammed akifungua kwa Kusoma quran Tukufu katika ukumbi wa Skuli ya Michekweni  Mkoa wa Kaskazini Pemba.
  Mkuu wa Idara ya Uchumi Uwezeshaji na Fedha (UVCCM) ndg:Dorice Obed akizungumza katika Mkutano wa ndani  wa Wanachama na Viongozi wa CCM na Jumuiya zake Wilaya ya Michekweni Mkoa wa Kaskazin pemba.
 Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mhe:Abeid Juma Ally akizungumza
  Kaimu katibu mkuu wa umoja wa Vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akizungumza katika Mkutano wa ndani  wa Wanachama na Viongozi wa CCM na Jumuiya zake Wilaya ya Michekweni Mkoa wa Kaskazin pemba.
 Wanachama na Viongozi wa CCM na Jumuiya zake Wilaya ya Michekweni wakifuatilia kwa Umakini mkutano huo.
 Mkuu wa Idara ya Uchumi Uwezeshaji na Fedha ndg:Dorice Obed akicheza nyimbo ya CCM pamoja na wanachama na Viongozi wa CCM na Jumuiya zake Wilaya ya MichekweniMkoa wa Kaskazin Pemba

''Shaka ni kijana jasiri mwenye kujenga hoja na kushambulia wapinzani kwa Vielelezo hamofii Seif,Sumaye Lowasa na wengine,wala kingunge,anwajibu kwa ushahidi na Vielelezo''Alisema Dady faki Dady msaidizi wa Rais SIASA Pemba wakati akizungumza katika mkutano wa ndani uliofanyika Skuli ya Michekweni.Mkoa wa Kaskazini Pemba.(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)


...................................................................................................................................................................

Na Mathias Canal, Kaskazini Pemba


Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema kuwa Jukumu la kuleta maendeleo ya kiuchumi katika jamii ni la kila mwananchi sio jukumu la serikali pekee.


UVCCM imesema kuwa jukumu la serikali ni kuwaonyesha wananchi fursa zilipo na namna bora ya kuzichanganua ikiwa ni pamoja na kufanya kazi ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla wake sambamba na kuwezeshwa kupata mikopo katika vikundi vyao vya ujasiriamali.


Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 16, 2017 alipokuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake katika mkutano wa ndani uliofanyika katika ukumbi wa Jamhuri Wilayani Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.


Alisema kuwa vijana ni nguvu kazi ya Taifa hivyo wanapaswa kutumia nguvu zao vizuri kwa kufanya kazi ili kujikwamua kiuchumi katika familia zao badala ya kukaa maskani kujadili mambo yasiyokuwa na tija kwao.


Aliongeza kuwa UVCCM inaunga mkono vijana kukaa maskani kwa maslahi mapana ya mjadala wa Maendeleo yatakayopelekea kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kujiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali.


Shaka alisema kuwa  Kila mwananchi kwa nafasi yake anatakiwa kuwajibika kwa nafasi aliyonayo ndani ya chama ama serikali kwani wananchi wanataka maendeleo ya uchumi wao sio ahadi hewa za majukwaani.


Aidha, alisema kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli ipo pamoja na watanzania wote ambao ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi ama wale ambao sio wanachama wa vyama vya siasa kwani mchakato wa maendeleo hauangalii itikadi za vyama vya siasa.


Alisema wananchi wanatakiwa kutumia Tunu ya amani, umoja na mshikamano uliopo nchini kufanya shughuli za maendeleo na kujiepusha na maneno ambayo yataleta chokochoko za kuondoa mshikamano katika jamii.


Shaka alisema kuwa vijana wanatakiwa kujiajiri katika ujasiriamali kwa kuchukua hatua za makusudi za kujiajiri kwani kusubiri ajira za serikali zitawachelewesha na pengine kufikia hatua ya uzee pasina kuajiriwa kutokana na uchache wa ajira serikalini na wingi wa vijana.


Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana UVCCM ameanza ziara ya kikazi jana Agosti 15, 2017 visiwani Pemba ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya ushindi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020.

No comments: