Tangazo

January 23, 2018

Takribani wanafunzi 10,000 wajiandikisha na masomo ya ufundi ya VSOMO

Meneja Miradi Airtel Tanzania Jane Matinde akizungumza wakati wa semina kwa vijana kuhusu umuhimu wa kusoma kwa kutumia mtandao kupitia aplikesheni ya VISOMO inayotumiwa na VETA kwa kushirikiana na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel katika makao makuu ya kampuni hiyo Morocco, Dar es Salaam.
Dar es Salaam
Takribani wanafunzi 10,000 tayari wameshajiandikisha na masomo ya ufundi ya VETA kupitia application ya VSOMO  ili kusoma kozi mbalimbali za ufundi nchini. Mafunzo hayo ya ufundi ya VSOMO yanapatikana kupitia simu za mkononi kwa ushirikiano kati ya kampuni ya simu za mkononi ya Airtel na mamlaka ya mafunzo ya ufundi stadi (VETA)  yamekuwa nikichocheo kikubwa katika upatikanaji wa elimu kwa njia ya mtandao na kuongeza idadi ya wanafunzi wanataraji na wanaosoma masomo ya ufundi katika nyanja mbalimbali nchini.
 Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu program hiyo, Kaimu Mkuu wa chuo cha ufundi cha VETA Kipawa, Bw. Harold Mganga alisema mafunzo ya ufundi ya muda mfupi yamekuwa yakitolewa na katika vyuo cha VETA kwa miaka mingi na hivyo idadi ya wanafunzi kuongezeka kila mwaka.
Aidha alisema kuwa kwa kuliona hilo VETA ikaona ni vyema kutanua wigo kwa kushirikiana na Airtel ili kutoa mafunzo haya kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha vijana katika maeneo mbalimbali hususani maeneo ya pembezoni au walio katika shughuli zao za kazi  kupata nafasi ya kusoma masomo ya nadharia kupitia simu zao mahali popote wakati wotote kisha kufanya mafunzo ya vitendo katika vyuo vyetu vya VETA mara baada ya kafaulu mitihani yao. 
“Najisikia fahari kusema kuwa ushirikiano wetu na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel umekuwa na tija kubwa katika kuwafikishia watanzania wote mafunzo haya kwa urahisi na ufanisi mahali popote nchini”, alisema Bw. Mganga.
 Mpaka sasa wanafunzi 9975 wamejiandikisha kupata mafunzo haya na Zaidi ya watanzania elfu 33 wameshapakuwa application ya VSOMO kupitia simu zao za mkononi. Kwetu sisi haya ni mafanikio makubwa na tuaamini kuwa mapinduzi haya ya elimu kupitia mtandao ndio yatakayoleta tija na kutuwezesha kuwa na nguvukazi yenye uledi ili kwenda sambamba na mahitaji ya nchi katika kufikia uchumi wa viwanda kwani nguvukazi ni moja kati ya nguzo muhimu katika kuendesha viwanda hivyo.
 Kwa upande wake Meneja Mradi wa VSOMO Airtel, Bi Jane Matinde alisema “ Tunayo mikakati mingi mwaka huu itakayowezesha watanzania wengi hususani vijana kuvutiwa na kujiunga na masomo haya ikiwemo kuongeza idadi ya kozi, kutoa elimu kwa uma juu ya upatikanaji wamasomo haya, kuboresha namba yetu ya kituo cha simu cha VSOMO ya 0699859573 na0699859572  na masaa ya kupata huduma na vilevile  kutanua wigo wa upatikanaji wa huduma hii na kuboresha malipo ya ada pamoja na mikakati mingi zaidi.
 Lakini  pia mkakati tulionao mpaka kufikia mwezi wa februari mwisho mwaka huu  tutazindua kozi tano mpya  ambazo ni pamoja na kozi ya usafi, kutengeneza Keki,  kuoka mikate, ufugaji wa kuku pamoja na upambaji wamaua.
Mpaka sasa tunazo kozi kumi na moja ambazo tayari tumeshazizindua na zinapatikana katika application hiyo ya VSOMO ambazo ni pamoja na kozi ya Huduma ya chakula na mbinu za kuhudumia wateja, Matengenezo ya kompyuta,umeme wa viwandani, ufundi Bomba wa Majumbani, Umeme wa magari, kutengeneza na kupamba keki, ufundi wa simu, ufundi pikipiki, Utaalamu saluni na urembo, ufuni wa kuchomelea pamoja na ufundi wa Aluminium.
 Tunaamini upatikanaji wa kozi mbalimbali kutawezesha watanzania wengi kujiunga na kusoma masomo haya na kutanua wigo wa wanafunzi wengi zaidi kusoma na kupata vyeti kila mwaka. Tunatoa wito kwa vijana , wazazi na walezi kutumia mfumo huu kujiendeleza nakupata ujuzi zaidi aliongeza Matinde

 Mpaka sasa mikoa minayoongeza kwa kuwa na mwitikio mkubwa wa wanafunzi kujiandikisha ni pamoja na Dar es saalam, Mwanza , Arusha, Morogoro na Dodoma huku vijana toka mikoa 26 nchini wamejiandikisha na mafunzo haya.

1 comment:

Anonymous said...

Namba zenu na mm natafuta chuo hicho