Tangazo

February 22, 2018

MWIJAGE MGENI RASMI KONGAMANO LA VIWANDA KESHO MWALIMU NYERERE


Na Humphrey Shao, Globu Ya jamii
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage anataraji kufungua kongamano kuhusu Maendeleo ya Viwanda Tanzania   litakalo fanyika katika chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere  February 23 Mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo  Afisa Habari wa chuo Hicho 

Evelyn Mpasha amesema kuwa Kongamano hilo kubwa litawaleta karibu wadau mbalimbali wa masuala ya maendeleo ya Viwanda nchini.

“Kongamano hili litaangazia Masuala ya Maendeleo ya Uchumi , Uwekezaji Endelevu  katika Viwanda, Ujasiliamali katika Uwekezaji katika Viwanda kwa mfumo wa ushirikiano kati ya sekta ya Umma na sekta binafsi” amesema Mpasha.

 Kwa upoande mmoja wa watoa mada katika kongamano hilo Binto Mawazo amesema kongamano hili ni sehemu ya juhudi za chuo kushiriki katika kuunga mkono juhudi za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuipeleka Tanzania katika uchumi wa Viwanda .


Binto amesema kuwa MNMA kama chuo ni wadau Muhimu sana katika kukiwezesha wananchi kufika malengo ya Rais kuipeleka nchi katika  uchumi wa kati. 

No comments: