Tangazo

June 4, 2018

UMEME NI NISHATI MBADALA ILIYO NAFUU KWA MATUMIZI YA NYUMBANI: KAMOTE

 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea kwenye banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya Nishati Mbadala yanayokwenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Juni 4, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limesema hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuogopa kutumia nishati ya umeme kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani kwani ni nafuu mno ukilinganisha na nishati nyingine.
Afisa Mazingira wa Shirika hilo, Bw.Yusuf Kamote, amesema hayo kwenye maonesho ya Nishati mbadala ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayoendelea kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Juni 4, 2018, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkaa ni ghali tutumie Nishati mbadala”.
“Siku zote tunasema umeme wa TANESCO ni umeme wa bei nafuu, jambo la msingi ambalo wananchi wanapaswa kuelewa ni matumizi sahihi ya vifaa vya umeme kulingana na mahitaji.” Alisema.
Alisema kwa mfano mtu anatumia kifaa kinachohitaji WATI 100 (100watts) kwa saa moja lakini anatumia kifaa cha WATI 200 (200Watts) kwa saa na kwa mahitaji yanayofanana, bila shaka hayo sio matumizi bora ya umeme.
Bw. Kamote pia alishauri, wananchi wanapotaka kununua vifaa vya umeme, wanapaswa kukague kiasi cha umeme kinachohitajika kwenye kifaa husika anachotaka kununua na vifaa hivyo hupimwa kwa kutumia WATI (Watt ).
“Ukitumia pasi ya umeme ya WATI 1000 (1000Watts), kwa saa moja ni sawa na kutumia Unit 1 ya umeme kwa hivyo hakuna sababu ya kununua pasi ya umeme ya WATI2000 (2000Watts), kwa matumizi ya kawaida kwani pasi ya aina hiyo kwa matumizi sawa na ile ya WATI1000, matumizi yake yataongezeka, kutoka unit 1 hadi uniti 2.” Alifafannua.
Akieleza zaidi Bw. Kamote hakuna sababu tena ya kutumia mkaa kama nishati ya kupikia kwani hivi sasa yapo majiko ya umeme ambayo yanasaidia kudhibiti matumizi yaumeme yasiyo sahihi kwani.
“Kinachohitajika mpishi unatakiwa kuandaa vyakula unavyotaka kupika kabla ya kuwasha jiko lako la umeme, vyakula vikiwa tayari hapo ndipo unatakiwa kuwasha jiko lako tayari kwa kupika.” Alisema na kuongeza
Maonesho hayoyakliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais,  yalizinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita na yanatariwa kufungwa na Rais John Magufuli, Jumanne Juni 5, 2018.

 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu na wataalamu wa TANESCO (Kushoto).
Afisa Mazingira wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Bw. Yusuf Kamote, (kulia), akimsikiliza Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Bi. Samia Chande.


 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya nishati ya umeme walipotembelea banda la Shirika hilo leo Juni 4, 2018.
 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akimsikiliza mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la Shirika hilo kupata elimu ya umeme.

1 comment:

eddyshaw9272711 said...

I'm often to running a blog and i really admire your content. The article has really peaks my interest. I'm going to bookmark your website and maintain checking for brand new information. gsn casino slots