Tangazo

September 23, 2011

T-MOTO WAINGIA STUDIO KUKAMILISHA ALBAM

Wasanii wa Kundi  jipya la Muziki wa Taarab la Tanzania Moto Modern Taarab (T-Moto), Mosi Suleiman (kushoto) na Hassan Ally, wakiwa katika Studio za Makunde Production Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, wakati wakirekodi nyimbo zao mpya zitakazokamilisha albam yao ya kwanza ya Aliyeniumba Hajanikosea.
Baadhi ya wasanii wa Kundi jipya la Muziki wa Taarab, la Tanzania Moto modern Taarab (T-Moto), wakiwa katika Studio za Makunde Production Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.
Msanii chipukizi katika miondoko ya Taarab, aliyeibukia katika michuano ya BSS, Mrisho Rajab, aliyejiunga na kundi jipya la Taarab la Tanzania Moto Modern Taarab (T-Moto) akiimba kwa hisia wakati akirekodi kibao chake cha Mchimba Kaburi Sasa Zamu yake Imefika, katika Studio za Bakunde Production zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam jana. Wimbo huo ni miongoni mwa nyimbo zinazokamilisha albam yao ya kwanza ya Aliyeniumba Hajanikosea.
Kunsi jipya la Taarab la Tanzania Modern Taarab (T-Moto) linalotarajia kuzinduliwa Oktoba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam, limeingia Studio za Bakunde Production zilizopo Kinondoni jijini jana kuanza kurekodi nyimbo zake mpya zilizokamilika ili kukamilikamisha albamu.

No comments: