Tangazo

October 10, 2011

Wakazi wa Kinyenze Morogoro bado walia na Uzio wa Mwekezaji

Mkazi wa Kitongoji cha Kinyenze, Mary Nathan akipita katika njia ndogo iliyofunguliwa na mwekezaji raia wa kigeni alinayemiliki ardhi katika eneo la kitongoji hicho kilichopo Kijiji cha Kipera Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro. Mwekezaji huyo analalamikiwa na wakazi wa kijiji hicho kufunga njia na kuvamia mashamba yao. Wakazi hao bado wanalalamika kuwa njia hiyo licha ya kufunguliwa lakini imetengenezwakama ya kupitisha mifugo kwani ni nyembamba na hairuhusiwi kupitisha gari wala pikipiki jambo ambalo bado ni kero kubwa kwa wakazi hao. (Picha na Mroki Mroki)
Mkazi wa Kitongoji cha Kinyenze, Nuru James  akipita na baiskeli yake kwa shida katika njia ndogo iliyofunguliwa na mwekezaji raia wa kigeni alinayemiliki ardhi katika eneo la kitongoji hicho kilichopo Kijiji cha Kipera Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro. (Picha na Mroki Mroki)

No comments: