Tangazo

November 1, 2012

JK azindua nyumba za waathirika wa Maporomoko ya 2009 Mamba Miamba

 Rais Jakaya Kikwete akizungumza jambo mara baada ya kuweka jiwe la msingi na kukagua ujenzi wa nyumba wa nyumba 8 za waathirika wa maporomoko yaliyotokea katika Kijiji cha Goha Kata ya Mamba Miamba Wilayani Same mkoani Kilimanjaro mwaka 2009 ambapo ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa kwao kama ubani wa serikali. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama.
 Rais Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa nyumba 8 za waathirika wa maporomoko yaliyotokea katika Kijiji cha Goha Kata ya Mamba Miamba Wilayani Same mkoani Kilimanjaro mwaka 2009 ambapo ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa kwao kama ubani wa serikali. Kushoto ni Mkuu wa Wila ya Same Herman Clement Kapufi na katikati ni Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango Malecela.
 
Moja ya nyumba hizo zinazojengwa kwaajili ya waathirika hao wa maporomoko. Ina vyumba vitatu vya kulala na sebule. 
Rais Jakaya Kikwete akipita kukagua ujenzi wa nyumba wa nyumba 8 za waathirika wa maporomoko yaliyotokea katika Kijiji cha Goha Kata ya Mamba Miamba Wilayani Same mkoani Kilimanjaro mwaka 2009 ambapo ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa kwao kama ubani wa serikali. Rais Kikwete aliweka jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba hizo juzi.

No comments: