Tangazo

October 17, 2013

MAKAMU WA RAIS DK. BILAL AITAKA TBA KUINGIA UBIA UJENZI WA NYUMBA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga, wakati akikagua ramani za ujenzi wa Makazi ya Nyumba 851  za Watumishi wa Umma zinazojengwa katika eneo la Bunju B, Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam, wakati wa sherehe hiyo liyofanyika leo. Picha na OMR 
 *******************************
NA ELIPHACE  MARWA - MAELEZO

MAKAMU wa  Rais Dkt. Mohamed Ghalib Bilal  ameutaka  Wakala wa Majengo Tanzania(TBA) kuangalia jinsi ya kutumia fursa amabayo Serikali imeruhusu taasisi za Serikali kuingia ubia ba sekta binafsi(PPP)katika kufanikisha miradi ya ujunzi wa nyumba za watumishi wa  umma.

Kauli  hiyo ilitolewa leo na Makamu wa Rais wakati  sherehe  za uweka ji  wa jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 851 za watumishi wa umma katika eneo la Bunju B, wilaya ya kinondoni Jijini Dar es Salaam.

“ Wakala mnatakiwa  muangalie jinsi ya mtakavyoweza kutumia  wabia wa ndani na wa nje katika kutekeleza mradi maalum wa ujenzi wa nyumba 10,000 kwa kipindi cha miaka mitano  ambao unatazamiwa kutatua kero ya makazi ya watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla,” alisema Dkt. Bilal.

 Makamu wa Rais  aliongeza kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kazi bora inayofanywa na watumishi wake ndiyo maana inawaonesha kuwajali  kwa kuwajengea nyumba bora .

Aidha  aliupongeza  wakala  huo, kwa kuanzisha mradi huo wa kujenga nyumba hizo,ambapo  gharama ya nchini  inaanzia milioni 25 hadi kufikia milioni 50.

Naye Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akielezea changamoto mbalimbali  ambazo wakala huo, unaakabiliana nazo   kuwa  ni  gharama kubwa za uwekaji miundombinu ya maji safi na nishati.

 Alizitaja changamoto  nyingine ni kutozwa  riba kubwa za mikopo zinazotolewa na benki za hapa nchini, pia   baadhi ya halimashauri kutokuwa na viwanja vya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.

“ Naomba  Makamu wa Rais  na ofisi yako inisaidie kuhakikisha  wale wote ambao wanadaiwa mikopo ya nyumba wawe wamelipa ndani ya mwezi mmoja ikiwa watashindwa kulipa wanyang’anywe nyumba hizo na kuuziwa watu wengine ili kutoa fursa kwa wakala kujenga nyumba nyingine , ambapo hadi sasa watu 2500 bado hawajamaliza kulipa madeni yao,” alisema Waziri Magufuli.

Aidha   wakala  huo, utajenga nyumba nyingine 1400 katika mkoa wa Dares Salaam na  nyumba 2500  katika mikoa 12 ya Tanzania Bara kwa kipindi cha mwaka huu wa fedha wa 2013/2014 na kumalizia nyumba zilizo baki ndani ya miaka mitatu, ambapo Makamu wa Rais alitaka ujenzi huo usisimame ili kufikia lengo la nyumba 10,000 na zaidi.

No comments: