Afisa
 Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens kulia akisisitiza jambo kwa 
wananchi waliofika kwenye banda lao kupata elimu ya mpango wa kujiunga 
na bima ya Afya
 Katibu
 Tawala wa mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akiwa na tisheti 
akijiandaa kuwapa watoto zawadi wakati alipotembelea banda hilo kushoto 
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Ally 
Mwakababu
 Katibu
 Tawala wa mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akiwa na tisheti 
akijiandaa kuwapa watoto zawadi wakati alipotembelea banda hilo kushoto 
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Ally 
Mwakababu 
sehemu ya watoto waliojiunga na mpango wa Toto Afya kadi
NA MWANDISHI WETU, TANGA. 
WATANZANIA wametakiwa kujiunga na 
mpango wa bima a Afya ili waweze kunufaika na huduma za matibabu ya 
uhakika wakati wanapokuwa wakiugua na hivyo kuwapunguzia mzigo wa 
kuingia gharama kubwa. 
Hayo yalisemwa leo na Afisa Masoko na 
Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) Makao Makuu Hawa
 Duguza wakati akizungumza kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga 
kunakoendelea maonyesho ya biashara ya kimataifa. 
Licha ya mfuko
 huo kutoa elimu juu ya umuhimu wa mpango wa bima lakini pia wanaendelea
 kutoa huduma za upimaji wa afya na kutoa ushauri kwa wananchi ambao 
wamekuwa wakifika kwenye banda lao lililopo kwenye maonyesha hayo. 
Alisema
 mpango wa bima ni mzuri kutokana na kuwapa uhakika wa matibabu wakati 
wanapokuwa wakikumbana na maradhi mbalimbali na hivyo ni muhimu kujiunga
 nao ili waweze kuona manufaa makubwa wanayoweza kuyapata. 
Aidha
 pia aliwahamasisha kujiunga na mpango wa kikoa na toto Afya kadi ambazo
 ni muhimu kwa ajili ya kuweza kupata huduma nzuri kipindi ambacho 
wanapatwa na changamoto za kuugua hususani watoto wadogo wakati wa 
ukuaji wao. 
“Ndugu zangu maradhi huwezi kujua yanakuja lini hasa
 kwa watoto wadogo wakati wa ukuaji wao hivyo niwasihi muone njia nzuri 
ya kuwawekea akiba ya matibabu kwa kuwaingiza kwenye mpango huu wa toto 
afya kadi kwani hii ni kumuhakikisha mtoto wako huduma wakati wote 
wanapougua”Alisema. 
Alisema pia jamii haiwezi kupata maendeleo 
ikiwa watakuwa hawana afya bora hivyo ni muhimu kuendelea kuhamasishana 
kujiunga na mpango huo kwa lengo la kuweza kunufaika na huduma za 
matibabu (habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)
 
 


 
No comments:
Post a Comment