Tangazo

July 5, 2012

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AKABIDHI VIFAA ZAHANATI YA KIMARA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Iddi akimkabidhi vifaa vya huduma na tiba, Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Kata ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda katika hafla maalum iliyofanyika jana, kwenye Zahanati hiyo, Kimara, Dar es Salaam. Vifaa hivyo vya sh. milioni 5.1, vimepatikana kutokana na michango ya wanachama na viongozi wa Jumuia ya Wazazi Tanzania. Wengine katika picha ni baadhi ya viongozi wa Jumuia ya Wazazi, Katibu Mkuu Hamis Dadi (kulia) Katibu Wilaya ya Kinondoni, Stanley Mkandawile (wapili kulia), na katikati ya Makamu na Mganga Mfawidhi ni Kaimu Mwenyekiti wa Jumuia hiyo, Dogo Mabrouk. (Picha na Bashir Nkoromo)


Wana-CCM Kata ya Kimara wakishangilia wakati wa hafla hiyo.

Baadhi ya wanachama wa Jumuia ya Wazazi waliohudhuria sherehe hiyo.

No comments: