Tangazo

October 15, 2012

Mtoto Rashid Athuman Hamisi amepotea



 Mtoto Rashid Athumani Hamisi 12 pichani, amepotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya kutoweka nyumbani kwao Kiwalani Minazi Mirefu anakoishi na Bibi yake Bi. Zamoyoni.

Rashidi ni mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi kisutu jijini Dar es Salaam. Tunaomba msaada wa jamii, mtu yeyote atakayemuona atoa taarifa katika kituo cha polisi Kiwalani Minazi Mirefu au katika msikiti wa eneo hilo.


Pia kwa mawasiliano ya simu 0713972201, 0783165655, 0762944781 na 0784531188. Rashid ni motto wa Mhariri wa Picha wa kampuni magazeti TSN, Athumani Hamisi, aliyepata ajali ya gari 2008.


No comments: