Tangazo

January 26, 2013

Helmet zinatusaidia sana kwa usalama wetu lakini vipi kuhusu maambukizi ya magonjwa ya ngozi? Kwa kuwa hazifuliwi wala kubadilishwa.!


Na. Lemmy Hipolite-Mo Blog.

Kofia ngumu za kusaidia kuokoa kichwa dhidi ya majanga mbalimbali iwe ni katika maeneo ya ujenzi au katika vyombo vya usafiri ni muhimu sana kwetu tunapokuwa katika mazingira hayo.

Tunaishukuru serikali kwa kutumia idara zake husika kuhimiza matumizi ya kofia hizi hasa kwa madereva wa usafiri wa pikipiki maarufu kama Bodaboda.

Kama inavyojulikana mtu ni afya na pia tunafahamu kuna baadhi ya magonjwa ya kuambukiza kwa njia ya kugusana, kutumia kitu kimoja watu wawili au zaidi na mengine kwa njia ya maji, hewa, mbu, kujamiiana na kadhalika.

Hapa kwenye hili la kofia ngumu bado hainiingii akilini vizuri jinsi gani twaweza kukwepa magonjwa ya ngozi na mba japo sio lazima tuyapate wala hatuyaombei ila tunaangalia uhalisia wa matumizi ya kofia hizi.

Ndugu zangu wataalamu wa magonjwa ya ngozi na tiba hili likoje katika uhalisia wake? Sichokonoi ila naomba kufahamu tu kwamba tuwe tunazifua? Au hakuna neno? Mzingatie pia je zitakauka?

Wadau sijasema msivae helmet la hasha nimeulizia tu ili woote tupate fahamu.
Karibu uchangie maoni yako kwa kubofya hapa

No comments: