Tangazo

July 7, 2013

SMILE COMMUNICATION YAWAKARIBISHA KATIKA BANDA LAO KWENYE VIWANJA VYA SABASABA

 Mmoja wa Wafanyakazi wa Kampuni ya Smile Wauzaji wa Router kwaajili ya matumizi ya intaneti akiwa na tabasamu la nguvu kama jina la kampuni anayoifanyia kazi katika banda lao lililopo katika Viwanja Vya Sabasaba
 Bwa Deogratias Kabeho, Meneja wa Mauzo wa Kampuni ya Smile (Wa kwanza Kushoto) akiwa katika Picha ya Pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake katika banda lao lililopo Katika Viwanja Vya Sabasaba barabara ya Kilwa Jijini Dar Es Salaam.
 Wafanyakazi wa Smile wakiwahudumia wateja waliofika katika banda lao kwaajili ya kupata maelezo juu ya kufungiwa router za smile ambazo zina spidi ya hali juu kabisa kuliko mitandao mingine ya intanet hapa nchini,nyuma yao ni runninga inayoonyesha video za muziki unaochezwa katika laptop iliyounganishwa na intanet ya Smile yenye Spidi ya 4G LTE
Wafanyakazi wa Kampuni ya Smile inayohusika na ufungaji na uuzaji wa router za intanet zenye spidi ya 4G LTE wakimuelekeza mteja wao aliyefika katika banda lao lililopo katika viwanja vya sabasaba kwaajili ya kupata huduma ya kufungiwa intanet na kampuni ya Smile ambayo ina spidi ya hali ya juu ya 4G LTE.Picha na Josephat Lukaza wa http://josephatlukaza.blogspot.com
..............
Smile ni Moja ya Kampuni inayotoa huduma za ufungaji wa Intanet kwa kutumia router ambazo unaweza kuunganisha mpaka kompyuta sita hadi 10 na zaidi na kwa spidi ya juu kabisa ya 4G LTE.
Smile ndio kampuni pekee ya inayotoa huduma ya kufunga intanet yenye spidi ya juu ya 4G LTE peke yake nchini Afrika Mashariki.
Vilevile Smile wanauza router zao kwa bei nafuu kabisa ambapo mteja akinunua router pamoja na modem zaoo anapata kifurushi cha GB 20 ambacho mteja ataweza kuperuzi mitandao mbalimbali kwa spidi ya Juu kabisa ya 4G LTE.
Watembelee katika banda lao lililopo sabasaba kwaajili ya kupata maelezo na vilevile kujipatia modem na router zao ili uweze kupata huduma nzuri na bei nafuu kuliko zote nchini Tanzania.

No comments: