Tangazo

August 26, 2014

FAINALI YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) KUFANYIKA TAREHE 30 AUGUST 2014 NDANI YA UKUMBI WA MLIMANI CITY

 Mc Pilipili Akiongea mbele ya Waandishi wa habari wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kuhusiana na fainali kubwa ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) litakalofanyika tarehe 30 August 2014 katika Ukumbi wa Mlimani City kuanzia Mida ya Saa 7:30 PM (Usiku) huku viingilio vikiwa ni Elfu Hamsini (50,000/=) kwa V.I.P na Elfu thelethini (30,000/=) kwa Kawaida. Wapili Kushoto ni Meneja Mradi TMT Joshua Moshi, Julieth Samson "Kemmy" ambae ni Mwalimu wa Nidhamu na Afisa Uhusiano TMT, Josephat Lukaza.
 Washiriki kumi bora Ambao wameingia kwenye fainali ya Kuwania Shilingi Milioni 50 za kitanzania ambayo fainali itafanyika tarehe 30 August 2014 katika Ukumbi wa Mlimani City  huku viingilio vikiwa ni Elfu Hamsini (50,000/=) kwa V.I.P na Elfu thelethini (30,000/=) kwa Kawaida.
 Mmoja wa washiriki walioingia Kwenye fainali ya TMT, Mwanaafa Mwinzago akiongea na waandishi wa habari leo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi za Proin zilizopo Mikocheni.
Baadhi ya washiriki na waandishi wa habari waliofika katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika ofisi za Proin zilizopo Mikocheni.
BAADA ya mchakato wa kuzunguka mikoani kwa ajili ya kusaka wasanii wenye vipaji vya uigizaji, hatimaye fainali za Tanzania Movie Talents  ( TMT) zitafanyika  Jumamosi ya Agosti 30 mwaka huu  katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa shindano hilo atajinyakulia kitita cha shilingi milioni 50 wakati burudani itadondondoshwa  na Christian Bella na mchekeshaji MC Pilipili.

No comments: