Tangazo

September 8, 2014

CFAO MOTORS WAWEZESHA WAPENZI WA FORMULA ONE DAR KUONA GEMU

DSC_0009
Kukiwa na wanawake warembo katika magari yanayomeremeta, waliovikwa na nguli wa mavazi Ally Rhemtulla kwa ajili ya kupokea wageni kwenye hafla ya kuona mashindano ya magari ya Formula One iliyoandaliwa na kampuni ya CFAO Motors kwa mashabiki wa mchezo huo na wateja wake.

Na Mwandishi wetu

JUMAPILI wakati kiwanja cha mbio za magari za Formula One cha Monza Italia kinawaka moto, wapenzi wa mchezo huo jijini Dare s salaam walipata uhondo wa kuona mkali wa injini na udereva, katika skrini kubwa iliyowekwa makao makuu ya CFAO Motors Tanzania, Barabara ya Nyerere, Dare s salaam.

Katika hekaheka hiyo iliyochukua takribani saa moja na kumaliza lap zote 53 mchuano mkali ulikuwa kwa timu ya Merceders Benz ambapo gari zake mbili zikiendeshwa na Hamilton na nyingine Rosberg zilichuana vikali.

Wakiandaa kwa mara nyingine hafla ya kuona mashindano ya magari ya Formula One, CFAO Motors iliwapeleka Watanzania na wageni waliokusanyika hapo Italia kwa staili ya aina yake na gemu ilipoanza ilikuwa mshikemshike.

Wakati watanzania hao wakisubiri majira ya Italia ya kuanza kwa mchuano huo, walipata burudani kutoka kwa madame Emilie na Madame Otilie kwa dansi la nguvu ambalo liliwaacha wageni waalikwa na miguno ya raha.
DSC_0052
Wageni wakipokelewa na wafanyakazi wa CFAO Motors wakati wa halfa hiyo.

Huku vinywaji na vitafunwa vikiendelea katikia ukumbi uliosukwa vyema na Irene wa DSM Treasue, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh, alielezea hafla yake na maana kwa timu nzima CFAO Motors Tanzania ambao ndio wawakilishi pekee wa Mercedes Benz.

Alisema ni hafla iliyolenga kuwaleta pamoja wapenzi wa mchezo na wadau wengine wa CFAO Motors kama sehemu ya kujuana na kuona mali mpya iliyoingia sokoni kwa lengo la kuwasaidia Watanzania kujiamini zaidi.

Alisema mwaka huu wamezindua kitu kipya mtaani cha S-Class ambacho ubora wake ni matokeo ya kazi kubwa ya Mercedes katika kuhakikisha inawapatia wananchi na wateja wake kitu bora zaidi.

Kukiwa na wanawake warembo katika magari yanayomeremeta, waliovikwa na nguli wa mavazi Ally Rhemtulla tukio la kuangalia mchuano wa timu mbalimbali za magari , kama ilivyokuwa ikitokea Monza lilijaa ushababi wa aina yake uoliofanya wengi waliofika kuifurahia Jumapili yao.
DSC_0375
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh akisoma risala kwa wageni waalikwa kwenye hafla ya kuona gemu ya mashindano ya magari ya Formula One iliyoandaliwa CFAO Motors usiku wa kuamkia leo jijini Dar.

Kama ilivyotokea Monza, Italia ambapo Lewis Hamilton alipambana vikali kuwa katika fomu baada ya kuanza vibaya kipenga kilipoanzisha mbio na baadae kushika usukani , kushinda na kumwagiwa shampeni, bahati nasibu ndogo iliyochezeshwa CFAO Motors baada ya mbio zile iliwapatia shampeni na cha juu Kamili Delaware kama mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Kauthar Mukhtar na wa tatu MaCarrie Dickin.

Tukio la kuangalia mashindano ya magari ya Monza liliongezwa nakshi na Tanzania Breweries kwa vinywaji vyao, MMI pia kwa vinywaji ambapo pia waliwapa nafasi wadau kuonja Patron tequila na Azam ambao walileta vinywaji na vipozo koo vya washangiliaji, ashkrimu.

CFAO wakitumia tukio hilo kuonesha pia bidhaa zao mpya walikuwa na kila sababu za kuelezea ubora wa magari ya Mercedes Benz ma huduma zake kuanzia magari ya familia hadi malori makubwa ya kibiashara, hasa baada ya timu za Mercedes benz kutwaa ushindi katika mashindano ya Monza.

Mshindi wa pili alikuwa Nico Rosberg (wa Mercedes pia) ambaye alishindwa kuhimili presha kubwa aliyokuwa akipumuliwa na Hamilton katika mbio hizo.

Ilikuwa ni katika lapu ya 29 wakati Rosberg, alipofanya kosa lililompokonya pointi 22 katika mbio za kuwania ubingwa wa Formula One.
DSC_0376
Pichani juu na chini ni baadhi ya wageni waalikwa wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh (hayupo pichani).
Pamoja na hilo Mercedes ilishangilia kutokana na kuwa na nafasi mbili za ushindi ambazo hawajawahi kuzipata tangu tukio la Austria Juni mwaka na sasa wamepata ushindi wa saba katika michuano 13 iliyokwishafanyika.
Aliyeshika namba tatu ni Mbrazil Felipe Massa akiwa katika timu ya Williams inakuwa ni ushindi wake wa kwanza tangu mei 2013.
Rosberg, ambaye sasa anapointi 238 dhidi ya 216 za Hamilton huku ikibaki michuano 6 ya bara la Ulaya katika mahojianoi alikiri kosa lakini akasema kwamba Lewis alikuwa na kasi kubwa.
"Unajisikia vibaya kupoteza ushindi namna ile, lakini Lewis alikuwa na kasi kubwa katika mchezo mzima.Alikuwa anakuja kama roketi na ilikuwa lazima nijisukume zaidi,kisha likaja kosa," alisema.
Kuanza vibaya kwa Hamilton kulitokana na tatizo la kiufundi katika gari lake baada ya kuchelewa kuanzisha mfumo.
DSC_0411
Bottas katika michuano hiyo alishika nafasi ya nne baada ya kufanya kazi ya akili ya kuyapita mgari mengine hasa baada ya kuchemsha katika lapu ya kwanza ambapo aliimaliza akiwa wa kumi.

Dereva wa Ferrari, Fernando Alonso alilazimika kuondoka nje ya mashindano kwenye lapu ya 29 baada ya gari lake kupata hitilafu kwenye mfumo wa nishati, ikiwa ni mara ya kwanza kukumbwa na tatizo la aina hiyo katika mbio 86 alizoshiriki mpaka sasa na Kimi Raikkonen alimalizia wa tisa.

Mfiniland huyo alimalizia akiwa wa kumi lakini alipanda baada ya dereva wa McLaren, Kevin Magnussen kuchapwa penati kwa kumuondoa barabarani Bottas .

Hadi Jumapili hii, Alonso ni dereva pekee ambaye amekuwa akipata pointi katika kila mbio.
DSC_0696
Wadau wa CFAO Motors na mashabiki wa mashindano ya magari ya Formula One wakila pozi.

MuAustralia, Daniel Ricciardo, ambaye amshinda mbio nyingine mbili za awali, alikuwa na siku nzuri na timu yake ya Red Bull kwa kumalizia wa tano. Kazi ya kuyapita magari mengine aliyafanya katika hali ya mshangao mkubwa akiwapita madereva mbalimbali akiwemo Sebastian Vettel (mshindi mara nne) ambaye alimalizia wa sita.

Mmexico Sergio Perez alikuwa wa saba akifanyia kazi timu ya Force India kibarua kizito kwa jinsi walivyokuwa wanagombvania nafasi yeye na dereva wa timu ya McLaren, Jenson Button ambaye alishika nafasi ya nane.
Kwa mujibu wa Mtangazaji michuano hiyo sasa inaelekea viwanja vya Mashariki ya mbali vya Singapore na Japan.
DSC_0460
Karen Emilie Asla (kushoto) na Anette Otilie Pettersen kutoka Maendeleo Dance Group wakitoa burudani kwa wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
DSC_0478
Meneja Masoko wa CFAO Motors, Tharaia Ahmed (mwenye sketi ya kijani) akifurahi jambo na baadhi ya wageni waalikwa.
DSC_0581
Karen Emilie Asla kutoka Maendeleo Dance Group akichagua namba za bahati nasibu iliyochezeshwa maalum kwa wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya kuona gemu ya mashindano ya magari ya Formula One iliyoandaliwa CFAO Motors kwa ajili ya wateja wake na wadau mbalimbali ambayo imefanyika makao makuu ya ofisi za kampuni hiyo. Wa tatu kushoto ni Meneja Masoko wa CFAO Motors, Tharaia Ahmed na Wa pili kushoto ni MC Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh. Kulia ni Mwakilishi kutoka kampuni ya mmi Tanzania (Maritime and Merchantile International Tanzania Ltd.) ambao ni wauzaji na wasambazaji wa vinywaji vikali na mvinyo.
DSC_0589
Meneja masoko kwa kampuni ya CFAO Motors, Tharaia Ahmed (wa tatu kulia) akikabidhi zawadi kwa mmoja wa wageni waalikwa aliyeibuka mshindi wa tatu MaCarrie Dickinson (wa pili kulia) kwenye bahati nasibu hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh.
DSC_0605
Meneja masoko kwa kampuni ya CFAO Motors, Tharaia Ahmed akikabidhi zawadi kwa mshindi wa pili wa bahati nasibu hiyo Bi. Kauthar Mukhtar(katikati).
DSC_0616
Meneja masoko kwa kampuni ya CFAO Motors, Tharaia Ahmed akikabidhi zawadi ikiwemo chakula cha usiku kwa watu wawili kwenye hoteli ya Hyatt Regency - The Kilimanjaro mshindi wa kwanza Bw. Kamil delaware (kulia) huku Mwakilishi kutoka kampuni ya mmi Tanzania (Maritime and Merchantile International Tanzania Ltd.) ambao ni wauzaji na wasambazaji wa vinywaji vikali na mvinyo.
DSC_0618
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh ( katikati) akitoa shukrani kwa wageni waalikwa na wadhamini waliofanikisha sherehe hiyo wakati wa hafla ya kuona mashindano ya Formula One kupitia Big screen kubwa iliyowekwa ukumbini hapo kwenye makao makuu ya ofisi za CFAO Motors jijini Dar.
DSC_0486
Pichani juu na chini ni baadhi ya wateja na wadau wa CFAO Motors wakishuhudia mashindano ya Formula One kupitia Big screen iliyokuwepo ukumbini hapo kwenye makao makuu ya ofisi hizo.
DSC_0573
DSC_0173
Wageni waalikwa wakijipatia vinywaji mbalimbali vikiwemo vinywaji vya Azam.
DSC_0254
Mvinyo na vinywaji vikali kutoka kampuni ya mmi Tanzania (Maritime and Merchantile International Tanzania Ltd.) navyo vilikuwepo.
DSC_0296
Muhudumu akiwasikiliza wageni waalikwa kwenye huduma za vinywaji.
DSC_0300
Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya CFAO Motors Bw. Aldo Pagan (kulia) akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
DSC_0718
Tender Manager wa CFAO Motors Bw. Marco Kahabi (wa pili kulia) akisalimiana na mmoja wa wageni waalikwa. Kulia ni Meneja Masoko wa CFAO Motors, Tharaia Ahmed.
Kwa picha zaidi ingia hapa

No comments: