Tangazo

October 14, 2014

VITABU VYA AIRTEL VYAIBUA ARI YA WANAFUNZI GUNGU SEKONDARI KIGOMA

Meneja wa Huduma za Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto),akikabidhi sehemu ya vitabu kwa Afisa Elimu vifaa na Takwimu wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Bwana Yalagwila Gwimo. 
Wanafunzi wa shule ya sekondari Gungu akifurahia kupokea vitabu vya masomo ya sayansi kutoka kwa kamouni ya simu za mkononi ya Airte.


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
KIGOMA



Meneja huduma za Jamii wa Kampuni ya simu za Mkononi ya Airtel Tanzania Bi Hawa Bayumi amesema nguvu kazi ya wananchi wenye ujuzi na elimu inahitajika nchini, hivyo wanafunzi wa shule za sekondari wana wajibu wa kuitumia elimu kama ngazi ya kuliwezesha taifa kuwa na maendeleo.


Bayumi aliyasema hayo wakati akikabidhi vitabu vya masomo ya Sayansi kwa Afisa Elimu vifaa na Takwimu wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bwana Yalagwila Gwimo kwa ajili ya shule ya Sekondari ya Gungu Mkoani Kigoma, Bayumi amesema serikali haiwezi kufanya kila kitu,wanafunzi wanatakiwa kutumia fursa hii kupanua uelewa wao kupitia vitabu vinavyotolewa na kampuni yake.



“Sisi kama Airtel tumetekeleza jukumu letu la kutoa vitabu kwa shule za Sekondari na tunatarajia wanafunzi mtasema kufeli sasa basi baada ya kuwekewa mazingira mazuri ya kupata vitabu vya kiada na ziada”…Alisema Bayumi.



Amesema taifa bado halijafikia kiwango cha kujivunia cha kuwa na wasomi wengi wa fani ya Sayansi, hivyo Airtel inasisitiza wanafunzi wafanye jitihada katika masomo hayo “Tunapotengeneza mazingira mazuri kwa mwanafunzi pia tunatengeneza mazingira mazuri kwa waalimu kwa kutoa vitabu vya kufundishia ambavyo vinakubalika na wizara ya elimu”Alisema Bayumi.



Kwa upande wake Mwalimu Mkuu  wa Shule ya Sekondari Gungu Bwana Alberto Dobeye mbali na kuishukuru kampuni ya Airtel chini ya mpango wa “Shule Yetu” kwa kutoa vitabu hivyo ameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa maabara shuleni hapo.



“Tunawashuru sana Airtel kwa vitabu hivi…lakini mkubuke kupata vitabu ni jambo moja na maabara ni jambo jingine,serikali ijitahidi kujenga maabara hapa shuleni ili wanafunzi wasome na kufanya majaribio ya Vitendo” Alisema Mwalimu Dobeye.



Kwa upande wake Afisa Elimu vifaa na Takwimu wa Manispa ya Kigoma Ujiji Bwana Yalagwila Gwimo amesema vizuri wanafunzi wakajikita kusoma vitabu kwa lengo la kupanua ulewa wao na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kuongeza ufaulu.


 Nao Wanafunzi Kassim Abdallah, na Rosemary Christopher kwa  kwa niaba ya wenzao wameipongeza kampuni ya simu ya Airtel kwa msaada huo na kwamba vitabu hivyo vitachochea Ari za wanafunzi kuongeza bidii katika masomo ili kufikia lengo la ufaulu kwa kupata alama za juu.

Msaada huo wa Vitabu vilivyotolewa ni mwendelezo wa shughuli za huduma kwa jamii zinazotelewa na Airtel kupitia mradi maalumu wa Shule yetu unaoziwezesha shule mbalimbali kutapa vitabu vya kiada na kiada, mpaka sasa shule zaidi ya 1000 zimeshafaidika na mpango huo.

No comments: