Tangazo

November 5, 2014

BENKI YA CRDB YASHIRIKI KONGAMANO LA VIJANA LA BIASHARA LILILOANDALIWA NA TAASISI YA AIESEC JIJINI ARUSHA

Jumla yaVijana 150 kutoka ndani na nje ya nchi wameudhuria Kongamano la Biashara kwa Vijana lililofanyika jijini Arusha ambapo Benki ya CRDB wakiwa ni miongoni mwa wadhamini wa  kongamani hilo.

Kongamano hilo lilihudhuriwa na Vijana kutoka katika Vyuo Vikuu vya nchi za Afrika Mashariki na kuandaliwa na Taasisi ya AIESEC ambalo hujihusisha na ubunifu wa vipaji vya uongozi miongoni mwa vijana lililofanyika jijini Arusha hivi karibuni katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Hall CDTI- TENGERU, Arusha ambalo lilihudhuriwa na wanafunzi 150 kutoka nchi tofauti za kimataifa na 150 kutoka vyuo vya elimu ya juu ndani ya Tanzania.

Benki ya CRDB kama miongoni mwa makampuni yaliyodhamini kongamano hilo, ilialikwa kuweza kutoa elimu juu ya “Teknolojia na Ubunifu” ambapo  Mkurugenzi wa mikakati na ubunifu wa Benki ya CRDB, Bw. Goodluck Nkini aliweza kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi walengwa.

 Katika kongamano hilo washiriki walipata nafasi ya kuelemishwa kuhusu huduma za kibenki kwa njia ya kieletroniki zilizotolewa na Mangire Kibanda (Meneja huduma za kibenki kwa njia ya kielektroniki) ambaye alitoa elimu kuhusu huduma za kibenki kwa njia ya simu (SimBanking), kwa njia ya Internet (Internet Banking), mashine za mauzo (Pos), Wakala wa Benki (FahariHuduma).
Mkurugenzi wa Mikakati na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Bw. Goodluck Nkini akitoa mada kuhusu teknolojia  na ubunifu.
Mkurugenzi wa Mikakati na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Bw. Goodluck Nkini akitoa mada.
Mkurugenzi wa Mikakati na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Bw. Goodluck Nkini akijibu maswali ya wanafunzi.
Ofisa Masoko wa Benki ya CRDB, Alma Ally (kushoto) akifafanua jambo kuhusu akaunti ya Scholar ambayo ni maalumu kwa wanafunzi.
Baadhi ya wanafunzi wakipata elimu kuhusu huduma za kibenki.
Meneja wa Huduma za Kibenki za Kieletroniki, Bw. Mangire Kibanda (kulia) akitoa elimu kuhusu huduma za kibenki za kielectroniki kwa njia ya simu (SimBanking), kwa njia ya Internet (Internet Banking), mashine za mauzo (Pos), Wakala wa Benki (FahariHuduma) kwa wanafunzi waliohudhuria kongamano hilo.
Baadhi ya wanafunzi wakipata elimu kuhusu huduma za kibenki zitolewazo na Benki ya CRDB.
Wanafunzi kutoka vyuo vya nchi za Afrika Mashariki na Kati wakisikiliza mada kutoka kwa Mkurugenzi wa Mikakati na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Bw. Goodluck Nkini (hayupo pichani).
Ofisa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Bw. Petro Kasindya (kulia), akitoa ufafanua kwa walengwa kuhusu mfumo wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB. 

1 comment:

Mwalimu said...

CRDB wanajitoa sana siku hizi, inapendeza na hii huinua hali ya ufahamu kwa wajasiriamali